Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatano, 23 Aprili 2014

elimu ya awali ndio msingi wa elimu bora

tujifunze kutokana na makosa tuliyoyatenda mda mrefu kwa kutokuwekeza kwenye elimu ya awali, sasa ndio muda muafaka wa kuwekeza kwa nguvu zetu zote kuinua elimu ya awali . elimu ya awali ndio msingi wa elimu ya msingi kila mmoja wetu lazima sasa tujitahidi kuhakikisha tunasaidia juhudi za upatikanaji wa elimu bora ya awali kwa watoto wetu.
kikubwa tuhakikishe tunapata walimu bora wa kufundisha madarasa ya awali, watoto wapate chakula shuleni  ikiwa ni pamoja na kuwajengengea  wanafunzi wa madarasa ya awali miundo mbinu rafiki itakayowafanya wapende elimu.
kwa pamoja tunaweza kuinua sauti za wanyonge