Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatano, 2 Oktoba 2013

Serikali kutoa ruzuku kwa shule binafsi

Serikali inatafakari uwezekano wa kutanua wigo wa kutoa ruzuku hadi kwa shule zinazomilikiwa na watu binafsi, ikiwa ni sehemu ya azma ya kuzipunguzia gharama za uendeshaji.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene, amesema hayo wakati akizungumza kwenye mahafali ya darasa la saba katika Shule ya St. Anne Marie Academy jijini Dar es Salaam jana.Alisema shule nyingi za binafsi zinafungwa kutokana na kushindwa kujiendesha miongoni mwa sababu kubwa ikiwa ni kupanda kwa gharama za uendeshaji.

Simbachawene alisema kuziacha shule binafsi `zife’ kutokana na sababu iliyo ndani ya uwezo wa nchi kuitatua, ni hasara kwa taifa na kwamba njia pekee ya kuzisaidia kwa kuzipa ruzuku ili ziweze kujiendesha.

Kwa mujibu wa Simbachawene, shule binafsi zimesaidia kwa kiasi kikubwa kuinua kiwango cha elimu, hivyo kupunguza idadi na kasi ya Watanzania kupeleka watoto wao kusoma nje ya nchi.Alisema: "Ukiacha shule kama hii (St. Anne Marie) ikafa ni hasara kwa taifa, serikali inaangalia kuona namna bora ya kuzisaidia kwa kuzipatia ruzuku ili kuzipunguzia gharama za uendeshaji.”

Kwa upande mwingine, Simbachawene aliwaasa vijana kuwa makini katika kukabiliana na kuzishinda changamoto zilizo katika jamii, ikiwamo maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) na matumizi ama usafirishaji wa dawa za kulevya.

Meneja wa shule hiyo, Jasson Rweikiza, alisema serikali imekuwa na kigugumizi katika mambo mbalimbali katika sekta ya elimu, hali inayosababisha  kudumaa kwa sekta hiyo na watoto kukosa ufaulu mzuri.

Kwa mujibu wa Rweikiza ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba Vijijini, mpaka sasa mitaala ya elimu na sera za elimu hazipo wazi, hali inayosababisha walimu wakose mwongozo wa kufundishia.

Alisema wadau wa elimu hususani wamiliki wa shule binafsi, wanakabiliwa na kazi kubwa ya uendeshaji, huku kukiwa na changamoto kadhaa kama vile matumizi ya mitaala isiyoeleweka.

Pia alisema sera zinazohusiana na elimu hazipo wazi, na kutoa mfano kuwa sera haielezi kama ni kosa ama si kosa inapotokea kuwapo mwanafunzi asiyejua kusoma.
“Maendeleo hayawezi kwenda bila kuboresha sekta ya elimu...tunaiomba serikali isimame imara katika kuinusuru sekta ya elimu nchini,” alisema.

Rweikiza alisema wahitimu wa darasa la saba wanapaswa kuondokana na dhana inayowafanya kujiona wamemaliza shule, bali kiwango hicho kuwa msingi wa safari ndefu inayowakabili maishani.

ippmedia.com

Walimu 344 wafukuzwa kazi 2008- 2013

Walimu 344 nchini wamefukuzwa kazi kutoka mwaka 2008 hadi mwaka huu kutokana na makosa mbalimbali ikiwamo kuwapa mimba wanafunzi.Hayo yalisemwa na Katibu Msaidizi wa  Ajira na Maendeleo ya Watumishi (TSD), Christina Hape, jijini Dar es Salaam jana.

Hape alisema mwalimu anatakiwa kuwa kama mlezi wa wanafunzi, lakini suala la kuwapa mimba linapokuja ni kosa la jinai na kwamba ni lazima wapelekwe polisi kwa ajiri ya kuchukuliwa hatua.Kwa upande wake, TSD pamoja na Tume ya Utumishi wa Umma wanaweza kuwafukuza kazi walimu.

Alisema  katika kipindi cha mwaka 2008 hadi 2009 wamefukuzwa walimu  40, mwaka 2009 hadi 2010 walimu 20 , mwaka 2010 hadi 2011 walimu 13  na mwaka 2011 hadi  2012 walimu 11 walifukizwa.Aliongeza kuwa mpaka sasa walimu 84 walifukuzwa kazi baada ya kubainika makosa yao ya kuwapa mimba wanafunzi.

Hata hivyo, alisema ugumu unakuja pale wazazi wanapokosa kutoa ushirikiano kwa serikali kwa kutohudhuria mahakamani na kuamua kulimaliza baada ya mtuhumiwa huyo kuwashawishi kwamba atamuoa binti yao.

Kwa upande wa makosa ya utoro kwa mwaka 2011 hadi 2012 walimu 152 na mwaka 2012 hadi 2013 walimu 157 walifukuzwa kazi .Alisema kwa wastani walimu wapatao 260 mpaka sasa wamefukuzwa kazi kutokana na utoro wa maeneo ya kazi.

Naibu Katibu Tume ya Utumishi wa Umma, Idara ya Utumishi wa Walimu, Edwini Mokongoti, alisema ili kuwezesha ufanisi katika utekelezaji wa masuala ya kiutumishi wakuu wa vyuo vya ualimu, vyuo vya maendeleo ya jamii, wakuu wa shule na walimu wakuu wanatakiwa kuwajibika katika kuwaelimisha walimu taratibu za masuala ya ajira katika maeneo mbalimbali ikiwamo kupandishwa vyeo, ajira na usajili.

Alisema pia wakuu hao watashughulikia makosa madogo madogo ya kinidhamu na kutoa adhabu, ambayo kwa mujibu wa kanuni namab 118 ya kanuni za utumishi wa umma ya mwaka 2003 zitakuw a, onyo, kusimamisha nyongeza ya mshahara kufidia hasara au sehemu ya hasara ambayo mtumishi itaisababishai serikali kutokana na uzembe wake.

ippmedia.com

mabunge ya wanafunzi yanawajengea wanafunzi uwezo wa kujieleza