Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumamosi, 24 Agosti 2013

KUTOKA KWA MARAFIKI WA ELIMU DODOMA

Hiki ni kibao kinacho wakumbusha wanafunzi wa shule ya sekondari Changaa kutumia lugha ya Kiswahili badala ya Kirangi wawapo shuleni hapo. Ajabu ni kuwa Ofisa Elimu Mkoa wa Dodoma eti kamshusha cheo Mkuu wa shule hiyo. Kwa maoni yangu nadhani kushushwa cheo kwa Mkuu huyo wa shule kumekuwa faraja kwake kwani wanafunzi wake hawaongei kiingereza wala Kiswahili badala yake wanatumia KIRANGI.