Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Ijumaa, 1 Agosti 2014

Waziri mkuu aagiza kumalizwa kwa tatizo la madawati

Waziri mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda ameagiza wakuu wa mikoa kote nchini kuhakikisha wanamaliza tatizo la uhaba wa madawati katika shule za msingi ifikapo juni 31 mwakani ikiwa ni kabla ya kumalizika kwa mwaka huu wa fedha ili serikali inapoanza mwaka mpya wa fedha shule zote nchini ziwe na madawati ya kutosha.
Waziri mkuu Mizengo Pinda ambaye amewasili jijini Mbeya kwa ajili ya kuhudhuria kongamano ya uwekezaji katika mikoa ya nyanda za juu kusini ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa ya mkoa wa Mbeya ambayo imeonyesha kuwa kuna tatizo kubwa la uhaba wa maawati katika shule za msingi.
 
Aidha waziri mkuu ameonyesha kutoridhishwa na ufaulu wa wanafunzi wa shule za msingi katika mkoa wa Mbeya, ambao mwaka jana wanafunzi wake wamefaulu kwa asilimia 48.5 ikiwa ni chini ya lengo la taifa la ufaulu wa asilimia 60, hivyo akatoa agizo kwa mkoa huo kuhakikisha unaweka mikakati itakayowezesha mwakani wanafunzi kufikia kiwango cha ufaulu ambacho kimewekwa kitaifa.

Waziri mkuu aagiza kumalizwa kwa tatizo la uhaba wa madawati

Waziri mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda ameagiza wakuu wa mikoa kote nchini kuhakikisha wanamaliza tatizo la uhaba wa madawati katika shule za msingi ifikapo juni 31 mwakani ikiwa ni kabla ya kumalizika kwa mwaka huu wa fedha ili serikali inapoanza mwaka mpya wa fedha shule zote nchini ziwe na madawati ya kutosha.
Waziri mkuu Mizengo Pinda ambaye amewasili jijini Mbeya kwa ajili ya kuhudhuria kongamano ya uwekezaji katika mikoa ya nyanda za juu kusini ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa ya mkoa wa Mbeya ambayo imeonyesha kuwa kuna tatizo kubwa la uhaba wa maawati katika shule za msingi.
 
Aidha waziri mkuu ameonyesha kutoridhishwa na ufaulu wa wanafunzi wa shule za msingi katika mkoa wa Mbeya, ambao mwaka jana wanafunzi wake wamefaulu kwa asilimia 48.5 ikiwa ni chini ya lengo la taifa la ufaulu wa asilimia 60, hivyo akatoa agizo kwa mkoa huo kuhakikisha unaweka mikakati itakayowezesha mwakani wanafunzi kufikia kiwango cha ufaulu ambacho kimewekwa kitaifa.