Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatano, 16 Julai 2014

SHULE YA ISANGO ILIYOKUWA IKIMILIKIWA NA JUMUIYA YA WAZAZI CCM YAUZWA KWA BEI CHEE

Photo: shule ya sekondari Isango iliyoko Kinesi Wilaya ya Rorya mkoa wa Mara imeuzwa kwa bei sawa na bure ya sh. milioni 125

wakizungumza kwa nyakati tofauti mwenyekiti wa ccm na mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wilaya ya Rorya kupitia kituo cha radio Victoria Vfm wamedai kuwa shule hiyo imeuzwa kijanja janja kwani tangu mwenyekiti huyo wa wazazi aingie madarakati hakuwahi kuambiwa juu ya uwepo wa deni lililopelekea kuuzwa shule hiyo.
mwenyekiti huyo wa jumuiya ya wazazi alienda mbali zaidi na kusema kitendo hicho kimefanywa makusudi kwa lengo la kumharibia uwajibikaji wake kwani kadai aliyeinunua shule hiyo ni mtoto wa aliyekuwa Mwenyekiti wa wazazi ccm mkoa wa Mara.
pia kasema kuwa dalali alionyesha wazi muenendo wa rushwa, kwa kugonga nyundo ya mwisho wakati bado wateja wengine wakiendelea kupandisha dau.

baada ya hapo ametoa wito kwa wananchi kumuunga mkono ili kuhakikisha shule hiyo inarejeshwa kwa wananchi baada ya kuwaambia wananchi hao kuwa tayari wamekwisha fungua kesi mahakama ya rufaa na hivi karibuni atakwenda kuonana na katibu mkuu wa chama cha mapinduzi ili kuhakikisha shule hiyo inarejeshwa mikononi mwa wananchi.shule ya sekondari Isango iliyoko Kinesi Wilaya ya Rorya mkoa wa Mara imeuzwa kwa bei sawa na bure ya sh. milioni 125

wakizungumza kwa nyakati tofauti mwenyekiti wa ccm na mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wilaya ya Rorya kupitia kituo cha radio Victoria Vfm wamedai kuwa shule hiyo imeuzwa kijanja janja kwani tangu mwenyekiti huyo wa wazazi aingie madarakati hakuwahi kuambiwa juu ya uwepo wa deni lililopelekea kuuzwa shule hiyo.
mwenyekiti huyo wa jumuiya ya wazazi alienda mbali zaidi na kusema kitendo hicho kimefanywa makusudi kwa lengo la kumharibia uwajibikaji wake kwani kadai aliyeinunua shule hiyo ni mtoto wa aliyekuwa Mwenyekiti wa wazazi ccm mkoa wa Mara.
pia kasema kuwa dalali alionyesha wazi muenendo wa rushwa, kwa kugonga nyundo ya mwisho wakati bado wateja wengine wakiendelea kupandisha dau.

baada ya hapo ametoa wito kwa wananchi kumuunga mkono ili kuhakikisha shule hiyo inarejeshwa kwa wananchi baada ya kuwaambia wananchi hao kuwa tayari wamekwisha fungua kesi mahakama ya rufaa na hivi karibuni atakwenda kuonana na katibu mkuu wa chama cha mapinduzi ili kuhakikisha shule hiyo inarejeshwa mikononi mwa wananchi.