Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatatu, 28 Oktoba 2013

maafisa elimu watakiwa kuthamini michango ya walimu

mkuu wa wilaya ya Arusha
Mkuu wa Wilaya ya Arusha, John Mongella, amesema mabadiliko ya haraka katika elimu yanaweza kutokea iwapo walimu watawezeshwa kitaaluma na kuwahimiza maafisa elimu kutoa motisha na kutambua mchango wa anayefanya vizuri ili kuwajengea zaidi morali.

Mongella aliyasema hayo katika hafla maalum ya kutoa zawadi na vyeti kwa wanafunzi wa kidato cha tatu waliofanya vizuri mitihani ya majaribio kwa  mikoa ya Arusha na Kilimanjaro katika masomo ya Hisabati, Elimu viumbe, Kemia, Fizikia na Kiingereza iliyoandaliwa na asasi ya Asante Africa Foundation , Africaid na Chuo Kikuu cha Elimu cha Mwenge kilichopo mjini Moshi.

 “Kuendelea kwa nchi yoyote ile ni pale inapokuwa na wana sayansi wengi zaidi…mwanasiasa gani utaendesha nchi ambayo haina wanasayansi?” alihoji.
Alisema maofisa elimu wanaweza kuanzisha mradi kama huo wa kufanya majaribio ya mitihani kwa wanafunzi wa sekondari zilizopo kwenye mikoa yao au kwa kushirikiana na mikoa mingine.

“Hii ni changamoto kwa maofisa elimu, wanaweza kutenga hata Sh. milioni 10 kwa ajili ya walimu wa masomo hayo na kama wanafunzi watakuwa wamefanya vizuri wanaweza kuzawadiwa,” alisema.

Mongella alisema  hata katika programu  ya ‘Matokeo makubwa sasa’ inahitaji walimu waongezewe uwezo ili wanafunzi waweze kufanya vizuri zaidi na inawezekana kuwa hivyo kwa kuwashindanisha.

Kwa upande wake, meneja wa mradi huo wa uwezeshaji walimu wa shule za sekondari, Sokoro Munubi, alisema malengo yao yanaendana na mpango wa serikali unaosisitiza 'matokeo makubwa sasa' katika sekta ya elimu.

“Kwanza tunawajengea uwezo walimu kwa kuwapatia mafunzo ya mara kwa mara pamoja na kufanya ufuatiliaji wa mafunzo yanayotokana na walimu wao wenyewe katika maeneo ya shuleni.

Akizungumzia mafanikio ya mradi huo tangu kuanzishwa kwake, alisema umekwisha kufundisha walimu 80 wa sekondari 40 zilipo wilaya tisa za mikoa ya Kilimanjaro na Arusha.

Alisema walimu 560 kutoka shule hizo nao wamekwisha kufundishwa na walimu wenzao katika maeneo ya shule zao na pia mradi umefadhili mitihani ya majaribio kwa wanafunzi wa kidato cha tatu na kwamba wanafunzi 4,500 walishiriki kufanya mtihani huo.
Alisema kuanzia mwakani mradi huo unatarajia kuongeza mikoa miwili lengo likiwa kufikia mikoa sita kwa baadaye.
chanzo. ippmedia.com & nipashe

madudu yagunduliwa tume ya pinda

Ripoti ya Tume ya Kuchunguza Matokeo ya Kidato cha Nne iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda mapema mwaka huu, iliibua madudu mengi ambayo hayajawekwa hadharani.
Wajumbe waliounda kamati hiyo kwa nyakati tofauti waliliambia gazeti hili hivi karibuni kuwa waligundua mambo mengi yanayodhihirisha udhaifu mkubwa katika uendeshaji wa sekta ya elimu nchini. Sehemu kubwa ya matokeo ya uchunguzi huo inasemekana yamejikita zaidi katika kuzitupia lawama taasisi za Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET).
Udhaifu wa kiutendaji kati ya taasisi hizo mbili unadaiwa umechangia kwa wanafunzi wengi kufanya vibaya kwenye mitihani ya Kidato cha Nne mwaka jana kiasi cha kuilazimisha Serikali kuunda tume kuchunguza tatizo kutokana na kilio kikubwa cha wadau wa elimu na wananchi.
Viongozi watatu waandamizi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi hawakupatikana kuzungumzia uchunguzi huo jana. Simu ya Waziri wa wizara hiyo, Dk Shukuru Kawambwa haikupatikana kabisa pale ilipopigwa.
Naye Naibu wake, Philipo Mulugo alijitetea kwamba alikuwa na shughuli nyingi na hivyo hakuwa na muda wa kuzungumzia suala hilo wakati Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Sifuni Mchome hakupokea kabisa simu yake.
Matokeo hayo ya mtihani wa Kidato cha Nne uliofanyika mwaka jana yanaonyesha kuwa watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 walipata sifuri, huku wanafunzi 23,520 tu ambao ni sawa na asilimia 5.16 ndiyo waliofaulu na wengine 103,327 sawa na asilimia 26.02 wakiwa wamepata daraja la nne. Katika mtihani huo, watahiniwa 397,136 walikuwa wa shule na 68,806 wa kujitegemea.
Kutokana na hali hiyo, Waziri Mkuu Pinda aliamua kuunda tume iliyoanza kufanya kazi kuanzia Machi hadi Juni mwaka huu. Tume hiyo iliyokuwa inaongozwa na Profesa Mchome ilimkabidhi Waziri Mkuu ripoti Juni 15, mwaka huu.Hata hivyo, ripoti hiyo haijawahi kutolewa hadharani baada ya tume kumaliza kazi yake.
Badala yake imeshuhudiwa Profesa Mchome, ambaye alikuwa Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Vyuo Vikuu Tanzania akipandishwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Huku kwa upande mwingine, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (Necta), Dk Joyce Ndalichako akichukua likizo ya muda mrefu ya mapumziko.
Madudu yaliyogunduliwa na tume
Wajumbe wa tume hiyo walisema kuwa matokeo ya uchunguzi wao yalibaini kuwa, maswali na mitihani iliyotungwa ilikuwa ni ile yenye kuzingatia maudhui badala ya kuzingatia kujenga maarifa na ujuzi.
“Tulitegemea kwa vile tangu mwaka 2006, mihutasari ya elimu ya Tanzania ilibadilika kutoka ile inayozingatia maudhui, kwenda kwenye ile inayozingatia kujenga maarifa na ujuzi basi na mtihani ungekuwa na mwelekeo huo,” alisema mmoja wa wajumbe wa tume ile.
Pia uchambuzi wa kamati ile uligundua kuwa hakukuwapo mawasiliano kati ya Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na Baraza la Mitihani la Taifa (Necta).TET, ambao ndio wasimamizi wa mitalaa ya elimu walitakiwa kuhakiki mitihani ile baada ya kutungwa na Necta, lakini hilo halikufanyika.
Chanzo kingine kililiambia gazeti hili kuwa tume hiyo ilibaini katika uchunguzi wake kuwa Necta ilitumia wataalamu wasio na juzi wa kutosha kutunga na kuhakiki mitihani. Uchunguzi huo ulibaini baadhi ya mitihani kama ya masomo ya Hisabati, Kemia na Fizikia ilikuwa na maswali yaliyohitaji muda mwingi wa kuyajibu kuliko uliopangwa.
“Hii ilifanya wanafunzi kushindwa kukamilisha kujibu maswali yote yaliyotakiwa kujibiwa kwenye mitihani hiyo. Pia tulibaini kwamba baadhi ya maswali katika mitihani ya masomo ya Fizikia na Kemia yalikuwa nje ya mihutasari iliyotumika kuwaandaa wanafunzi,” aliongeza mjumbe mwingine.Mjumbe mmoja aliongeza pia kuwa mitihani ilikuwa na misamiati migumu na hata kuwasumbua walimu walioisahihisha.
Hali hii inaweza kuwa imechangia, kwa kiasi kikubwa, kuongeza ugumu wa mitihani hiyo na hili linaweza kuchangia wanafunzi kushindwa kuelewa vizuri maswali wanayoulizwa kwenye mitihani.
Wajumbe wa tume hiyo walieleza hali hiyo imefanya imani kujengeka kuwa mitihani ya Tanzania ni migumu kuliko ya nchi nyingine.Huku kwa upande mwingine, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (Necta), Dk Joyce Ndalichako akichukua likizo ya muda mrefu ya mapumziko.
Madudu yaliyogunduliwa na tume
Wajumbe wa tume hiyo walisema kuwa matokeo ya uchunguzi wao yalibaini kuwa, maswali na mitihani iliyotungwa ilikuwa ni ile yenye kuzingatia maudhui badala ya kuzingatia kujenga maarifa na ujuzi.
“Tulitegemea kwa vile tangu mwaka 2006, mihutasari ya elimu ya Tanzania ilibadilika kutoka ile inayozingatia maudhui, kwenda kwenye ile inayozingatia kujenga maarifa na ujuzi basi na mtihani ungekuwa na mwelekeo huo,” alisema mmoja wa wajumbe wa tume ile.
Pia uchambuzi wa kamati ile uligundua kuwa hakukuwapo mawasiliano kati ya Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na Baraza la Mitihani la Taifa (Necta).TET, ambao ndio wasimamizi wa mitalaa ya elimu walitakiwa kuhakiki mitihani ile baada ya kutungwa na Necta, lakini hilo halikufanyika.
Chanzo kingine kililiambia gazeti hili kuwa tume hiyo ilibaini katika uchunguzi wake kuwa Necta ilitumia wataalamu wasio na juzi wa kutosha kutunga na kuhakiki mitihani.Uchunguzi huo ulibaini baadhi ya mitihani kama ya masomo ya Hisabati, Kemia na Fizikia ilikuwa na maswali yaliyohitaji muda mwingi wa kuyajibu kuliko uliopangwa.
“Hii ilifanya wanafunzi kushindwa kukamilisha kujibu maswali yote yaliyotakiwa kujibiwa kwenye mitihani hiyo. Pia tulibaini kwamba baadhi ya maswali katika mitihani ya masomo ya Fizikia na Kemia yalikuwa nje ya mihutasari iliyotumika kuwaandaa wanafunzi,” aliongeza mjumbe mwingine. Mjumbe mmoja aliongeza pia kuwa mitihani ilikuwa na misamiati migumu na hata kuwasumbua walimu walioisahihisha.
Hali hii inaweza kuwa imechangia, kwa kiasi kikubwa, kuongeza ugumu wa mitihani hiyo na hili linaweza kuchangia wanafunzi kushindwa kuelewa vizuri maswali wanayoulizwa kwenye mitihani. Wajumbe wa tume hiyo walieleza hali hiyo imefanya imani kujengeka kuwa mitihani ya Tanzania ni migumu kuliko ya nchi nyingine.
mwananchi.co.tz

mwanafunzi achalazwa viboko zaidi ya 100

Mwanafunzi wa shule ya sekondari Idodi wilayani Iringa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa kwa madai ya kupigwa viboko zaidi ya 100 na mtu anayedaiwa kuwa ni mwalimu wa shule hiyo na kufungiwa katika bweni kwa siku 3 ili kuificha siri hiyo.
Tukio hilo linakuja wakati harakati mbalimbali za kijamii na asasi za kiraia zikipiga kelele kupinga vitendo vya ukatili wakati jeshi la Polisi likianzisha dawati la jinsia kwa ajili ya kutokomeza masuala hayo.
Ni mwanafunzi Lusinde Nyaulingo, wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Idodi, ambaye anaugulia maumivu makali katika Hospitali hii ya rufaa ya mkoa wa Iringa, word namba tano ya majeruhi, kutokana na ukatili uliosababisha majeraha sehemu mbalimbali za mwili wake, hasa maeneo ya mapaja, makalio na mgongo, baada ya kupigwa kwa tuhuma za kuchukua simu ya mwanafunzo mwenzie, jambo linalomfanya mwanafunzi huyu apoteze muda mwingi wa masomo wakati akipatiwa matibabu ili kurudisha afya yake.
Lusinde anasema baada ya kuangushiwa kipigo hicho kikali, kilichodumu kwa zaidi ya masaa tatatu, alipoteza fahamu na kisha kufungiwa katika bweni kwa siku tatu, huku wanafunzi wenzie wakipigwa marufuku kufikisha taarifa ya ugonjwa kwa wazazi wa Lusinde.
Hata hivyo jeshi la polisi kupitia kamanda wake mkoa wa Iringa ACP Athmani Mungi limesema kuwa wanafuatilia tukio hilo ili kuhakikisha haki inatendeka, kwa kumchukulia hatua za kisheria mtuhumiwa ikiwa ni pamoja na kumfikisha Mahakamani. 
http://bongoleotz.blogspot.com

Jumatano, 23 Oktoba 2013

ripoti ya tume ya Pinda ni kitendawili haionekani




Tumeghadhabishwa na hatua ya Serikali ya kuendelea kuficha Ripoti ya Tume ya Kuchunguza Matokeo ya Kidato cha Nne iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda mapema mwaka huu. Tunasema hivyo kutokana na ukweli kwamba Tume hiyo iliundwa ikiwa ni hatua ya dharura kwa lengo la kutoa majibu ya haraka kuhusu sababu za wanafunzi wengi waliomaliza kidato cha nne mwaka jana kufanya vibaya katika mtihani huo na kuamsha vilio kote nchini.
Katika matokeo hayo, watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 waliambulia sifuri, wakati watahiniwa 23,520 ambao ni asilimia 5.16 wakiwa wamefaulu, huku watahiniwa wengine 103,327 sawa na asilimia 26.02 wakiwa wamepata daraja la nne. Katika mtihani huo, watahiniwa 397,136 walitoka katika shule mbalimbali, huku wengine 68,806 wakiwa wa kujitegemea.
Idadi kubwa ya wanafunzi hao kufeli mitihani kiasi hicho lilionekana kama janga la kitaifa na ndiyo maana wananchi wa rika zote, wakiwamo wabunge walipaza sauti wakiishinikiza Serikali itegue kitendawili kuhusu sababu za matokeo hayo ya kutia fedheha na aibu kwa taifa letu. Ndipo Serikali ilipounda Tume ya watu 15 Machi mwaka jana na kuitaka kuwasilisha ripoti yake serikalini miezi mitatu baadaye.
Tume hiyo ilimaliza kazi yake katika muda uliopangwa na kukabidhi ripoti hiyo Juni 15, mwaka huu. Jambo la kushangaza ni kuwa, pamoja na kupita zaidi ya miezi minne tangu ripoti hiyo iwasilishwe serikalini bado Serikali imeificha makabatini kwa sababu inazozijua yenyewe. Habari zinasema kwamba Serikali inajua umuhimu wa kuitoa ripoti hiyo hadharani haraka, lakini inasita kwa sababu mengi ya matatizo yaliyoainishwa na Tume hiyo yanaonyesha bayana kwamba Serikali pia ni sehemu ya tatizo.
Hata hivyo, tunapata shida kuelewa kwa nini Serikali inaendelea kuatamia ripoti hiyo wakati ikijua kwamba Watanzania wanasubiri ripoti hiyo kwa shauku kubwa kwa mategemeo kuwa, hatua za kurekebisha makosa yaliyotokea zingechukuliwa na mamlaka zote husika kwa kuwa muda siyo mrefu wanafunzi watafanya tena mitihani ya kidato cha nne mwaka huu.
Ukimya wa Serikali unaendelea kusababisha madhara mengine kadhaa, kwa maana ya baadhi ya wajumbe wa Tume hiyo kuchoka kuisubiri Serikali iweke hadharani ripoti ya Tume hiyo. Jana gazeti hili lilichapisha habari kuhusu baadhi ya vipengere vilivyo katika ripoti ya Tume hiyo, ambapo baadhi ya wajumbe waliounda Tume hiyo walisema katika nyakati tofauti hivi karibuni kwamba waligundua mambo mengi yanayodhihirisha udhaifu mkubwa katika uendeshaji wa sekta ya elimu hapa nchini.
Hata hivyo, baadhi ya wajumbe wanasema sehemu kubwa ya matokeo ya uchunguzi huo inajikita zaidi katika kulaumu Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), badala ya kujielekeza zaidi katika kupendekeza nini kifanyike ili kurekebisha mfumo mzima wa sekta ya elimu nchini ambao umedhihirika kuwa mbovu. Tatizo hapa pengine ni muundo wa Tume hiyo yenye idadi kubwa ya watumishi wa umma na wabunge wa chama tawala.
Wajumbe hao wamesema ripoti ya Tume hiyo ni ndefu na ingefaa Serikali iiweke wazi sasa ili ifanyiwe kazi. Sisi tunaungana na wajumbe hao kuishauri Serikali kufanya hivyo sasa. Madhara ya kuendelea kuihodhi ripoti hiyo ni makubwa pengine kuliko Serikali yenyewe inavyofikiri.

souce . mwananchi

Ijumaa, 18 Oktoba 2013

wizara ya elimu na mchakato wa upangaji wa alama za maendeleo ya wanafunzi sekondari

Ikiwa yamebaki majuma machache wanafunzi wa kidato cha nne waanze mtihani wa wa taifa, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi iko kwenye mchakato wa kubadilisha mfumo wa upangaji za mitihani ya sekondari na matumizi wa alama za maendeleo ya mwanafunzi (Continuous Assessment (CA). Mfumo huo ambao unatarajiwa kuanza kutumika kwenye Mtihani wa taifa wa kidato cha nne mwaka huu, unakuja ikiwa ni miezi michache tangu Tume ya Waziri Mkuu iliyoundwa kuchunguza chanzo cha kufeli kwa maelfu ya wanafunzi waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012.
Akizungumzia mchakato huo, Kamishna wa Elimu Profesa Eustella Bhalalusesa alisema kwamba hatua hiyo imechukuliwa ikiwa ni sehemu ya kuboresha elimu na kuwa haina uhusiano na taarifa ya tume iliyoundwa na Waziri Mkuu ambayo mpaka sasa haijawekwa hadharani.
“Mambo yanakwenda yanabadilika hata binadamu yeyote anabadilika kila siku, mfumo unaotumika sasa hivi ni wa siku nyingi,” alisema.Alisema kuwa, ili kuweza kuboresha vyema mfumo huo wameshirikisha wadau mbalimbali zikiwamo shule za sekondari.
“Kama unataka kuboresha lazima upate maoni, lengo letu ni kushirikisha shule zote za sekondari za Tanzania, ila siwezi kukuhakikishia kama zote zitashiriki kwa kuwa tunawatumia zaidi maofisa elimu mkoa na wilaya. Tumeweka pia dodoso kwenye mdandao ili watu zaidi washiriki.
Kuhusu tume ya Pinda hapa haihusiki kabisa, ile ilikuwa na mambo yake, hata bila ile tume sisi hii tungefanya tu,” alisema Profesa Bhalalusesa. Alisema kuwa, mpaka sasa wameshapokea zaidi ya asilimia 60 ya maoni hayo kutokana na lengo walilo jiwekea.
Dodoso hilo ambalo pia Mwananchi imefanikiwa kuliona, linasema kuwa serikali inakusanya maoni ya wadau wa elimu kuhusu Upangaji wa Viwango vya Alama (Grade Ranges) katika mitihani ya kuhitimu kidato cha nne na cha sita pamoja na matumizi ya ‘Alama Endelevu ya Mwanafunzi [Continuous Assessment (CA)].
“Serikali imeamua kukusanya maoni haya kwa sababu kwa muda mrefu sasa upangaji wa viwango vya alama vinavyotumika katika mitihani ya kuhitimu kidato cha nne na kidato cha sita havifanani pamoja na kwamba mitihani hiyo yote ni ya elimu ya sekondari.Pia mfumo wa elimu ya sekondari umekuwa na miundo tofauti ikiwemo ule unaotumika shuleni na ule wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta),” sehemu ya dodoso inasema.
Dodoso hilo linafafanua kuwa, muundo wa kwanza ni ule wa shule ambao alama mgando (Fixed Grade Ranges) ambao alama zinazotumika kupanga madaraja: A = 81 – 100; B = 61 – 80; C = 41 – 60; D = 21 – 40 na F = 0 – 20. Muundo wa pili ulioidhinishwa kutumiwa na Necta kuanzia mwaka 2012 ni Upangaji wa Alama Mgando usiobadilika (Fixed Grade Range).Kwa kidato cha nne alama zilizotumika ni A = 80 – 100, B = 65 – 79, C = 50 – 64, D = 35 – 49 na F = 0 – 34.
Kwa upande wa kidato cha sita alama zilizotumika ni A = 80 – 100; B = 75 - 79; C = 65 – 74; D = 55 – 64; E = 45 – 54; S = 40 – 44 na F = 0 – 39. Kwa mujibu wa dodoso hilo, alama zinazopendekezwa ni A = 81 – 100, B = 61 – 80, C = 41 – 60, D = 21 – 40 naF = 0 - 20.
Utaratibu mwingine ambao washiriki wanapaswa kuchagua ni A = 80 – 100, B = 65 – 79, C = 50 – 64, D = 35 – 49 na F = 0 – 34 huku utaratibu wa tatu ukiwa A+ = 91 – 100, A = 81 – 90, B+ = 71 - 80, B = 61 - 70, C+ = 51 – 60, C = 41 – 50, D+= 31 – 40, D = 21 – 30, E = 11 – 20 na U = 0 – 10.
Akisoma Kauli ya Serikali Bungeni kuhusu Taarifa ya Awali ya Tume ya Taifa ya Kuchunguza Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka 2012, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Wiliam Lukuvi alisema kuwa matokeo yaliyotangazwa awali na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi yafutwe na yapangwe tena kwa kutumia mfumo uliobadilika mwaka 2011 kama ilivyopendekeza tume ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Hata hivyo, baada ya kufutwa kwa matokeo hayo na kupangwa upya, Waziri wa Elimu Dk Shukuru Kawambwa alisema kuwa utaratibu uliotumika kupanga matokeo hayo mapya ni uleule uliotumika kuandaa matokeo yaliyofutwa wa Fixed Grade Ranges.
“Kuanzia sasa matokeo ya mtihani ya kidato cha nne na sita yatachakatwa kwa kutumia Fixed Grade Ranges na Standardization (alama zisizobadilika na kuuwisha alama za mitihani),” alisema Kawambwa.
chanzo.Mwananchi.co.tz

Jumatatu, 14 Oktoba 2013

mshahara wa Rais milioni 32 kwa mwezi

 

Igunga. Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe amesema sababu ya kutaja mishahara ya viongozi wakuu wa nchi ni kuzuia mianya ya watu wachache kuiibia nchi kutokana na usiri wa jambo hilo.
Zitto alitoa kauli hiyo jana mjini Igunga, wakati akitangaza mshahara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa mujibu wa Zitto, kwa mwaka kiongozi huyo wa nchi analipwa Sh384 milioni ambazo ni wastani wa Sh32 milioni kwa mwezi bila kukatwa kodi.
Hatua ya Zitto ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya kudumu ya Hesabu za Mashirika ya Umma (PAC), kutaja mshahara wa rais inakuja wiki moja baada ya kutaja mshahara wa Waziri mkuu kuwa ni Sh26 milioni kwa mwezi pasipo kukatwa kodi
Zitto alisema hoja ya msingi si kiasi wanancholipwa viongozi hao walioajiriwa na wananchi bali ni usiri unaofanywa juu ya kiwango hicho. Alisemaha ni jambo la kusikitisha kuona mwalimu anayelipwa mshahara wa Sh200,000 kwa mwezi ukikatwa kodi huku viongozi wa kuchaguliwa wakiwa wanapokea mishahara mikubwa pasipo kukatwa kodi.
Alisema katiba ya sasa Ibara ya 43(1), inaeleza kuwa rais atalipwa mshahara na malipo mengine huku ibara hiyo hiyo kifungu cha pili ikizuia mshahara na marupu rupu kupunguzwa, hali aliyoelezea kuwa ni muhimu katiba mpya ikabadilisha sheria hizo kwa manufaa ya nchi.
“Kwa hiyo hata kesho kama Dk Slaa akiwa Rais na akataka kupunguza mshahara wake kwa katiba hii hawezi na hili jambo si sahihi kwani viongozi wa ngazi hizi wanapata kila kitu bure kutoka Serikalini,” alisema Zitto.
Zitto alisema kuwa kitendo cha Serikali kuyafungia magazeti ya Mwananchi na Mtanzania, hakikuzingatiwa kulingana na uwazi uliowekwa kwa kuandika uwazi wa viwango vya mishahara.
Alisema kuwa waziri aliyehusika kufunguia magazeti hayo hakufikiria kwa makini kutokana na kuwa na uelewa mdogo na kuongeza kuwa hakuna kosa lolote linalopelekea kufungiwa magazeti hayo kutokana na ukweli ulioandikwa.

chanzo. mwananchi.com

Serikali yashauriwa kuruhusu walimu wa jumuiya ya Afrika Mashariki ili kukabiliana na upungufu wa walimu

Serikali  imeshauriwa kufungua milango kwa walimu wanaotoka katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kufanya kazi nchini kwa masharti nafuu.

Hali hiyo imeelezwa kuwa itachagiza kasi ya kukabiliana na upungufu wa walimu uliopo nchini na  hivyo kuboresha sekta ya elimu.

Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari ya Brilliant ya jijini Dar es Salaam, Jasson Rweikiza, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa mahafali ya tatu ya shule hiyo.

Rweikiza ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba Vijijini (CCM), alisema pamoja na jitihada za uboreshaji wa elimu nchini, bado uhaba wa walimu umekuwa tatizo sugu linalokwamisha azma hiyo.

 “Tunaweza kuboresha mazingira yote katika sekta ya elimu, lakini kama hatutakuwa na walimu wa kutosha, ni dhahiri kwamba ufundishaji utakwama na azma ya kupata matokeo bora ya wanafunzi haitafikiwa,” alisema.  Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Mbunge wa Sengerema (CCM), William Ngeleja.

Rweikiza alisema mazingira yaliyopo sasa yanakabiliwa na vikwazo katika kupata vibali kwa walimu hasa wanaotoka nchi za EAC kufanya kazi nchini.  Kwa mujibu wa Rweikiza, gharama za kibali kwa mwalimu mmoja kutoka nje, zinakadiriwa kufikia Shilingi milioni mbili.

Akizungumza katika halfa hiyo, Ngereja, pamoja na mambo mengine alisema wakati umefika kwa serikali kutilia mkazo namna bora za kukabiliana na changamoto zilizopo katika sekta ya elimu.

Alisema changamoto hizo ikiwamo wa ukosefu wa walimu, zinakwamisha ama kurudisha nyuma jitihada za maendeleo ya nchi na raia wake.

Alitoa mfano kuwa hata ufanisi katika kufikia Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) utapatikana ikiwa sekta ya elimu itaboreshwa na kuwezesha kupatikana kwa wataalam.

ippmedia.com

Jumapili, 13 Oktoba 2013

je kuna athari za kumrusha mtoto madarasa

Kuna wazazi (wakishirikiana na walimu) hurusha watoto wao madarasa (mfano anamaliza darasa la 3 anarushwa kuendelea na la 5)

- Je, unadhani ni kuna athari yoyote (kielimu, mahusiano yake na wanafunzi wenzake au kisaikolojia)?
- Unadhani kuna faida kufanya hivi?




Jana nilipeleka kijana kufanya mtihani wa kuanza kidato cha kwanza, wakati niko pale kukawa na akina mama wengine. Katika maongezi mama mmoja akasema kaleta binti yake wa darasa la sita kufanya mtihani huo, akifaulu anaruka la saba na kuanza kidato cha kwanza.

Na kuwa wakati, kuna mama mmoja tunafanya naye kazi alimrusha binti yake toka darasa la tatu na kuingia la tano, maana yake hakusoma darasa la nne kabisa.

Sasa mie nataka kujua kutoka kwa wadau.

  1. Unapomrusha mtoto darasa hakuna hasara yeyote? iwe kielimu, mahusiano yake na wanafunzi wenzie na saikolijia nzima ya mtoto(Ukizingatia mchana na usiku anakula ugali-kuna sred niliona mtu kasema ugali unasababisha mtu awe kilaza)
  2. Kuna faida yeyote kurusha mtoto darasa?
souce. jamii forums
Kuna wazazi (wakishirikiana na walimu) hurusha watoto wao madarasa (mfano anamaliza darasa la 3 anarushwa kuendelea na la 5)

- Je, unadhani ni kuna athari yoyote (kielimu, mahusiano yake na wanafunzi wenzake au kisaikolojia)?
- Unadhani kuna faida kufanya hivi?

Fuatilia mjadala huu => http://bit.ly/1gz2VIm


Jumamosi, 12 Oktoba 2013

DAWATI NI ELIMU

The "Dawati ni Elimu"” charity walk was held on 12 October from Mnazi Mmoja to Bunge Primary School led by the first lady of United republic of Tanzania Mama Salma Kikwete.
“The First of its kind mayoral ball aims to raise TZS 4.98 Billion towards providing 30,487 desks to primary and secondary schools in Ilala Municipality by end of financial year 2013/14. 100% of all funds shall proceeds towards realization of this project.
Dawati Ni Elimu is a project by Hon Jerry Silaa, Mayor of Ilala Municipal council toward the build up of the annual Mayors ball.
The Charity walk was sponsored by TSN Group, Eventlites, Continental Outdoor, A1outdoor and Vodacom and Managed by 361 degrees.
ABOUT DAWATI Ni ELIMU.

DAWATI Ni ELIMU is a project towards the Mayors ball that aims to solve the issue of shortage of desks in primary and secondary schools in Ilala municipality where by currently there is a lack of 30,487 desks. The project is an initiative under the office of the mayor of Ilala Municipal Council, this project seeks to raise a sum of 4.98 Billion Tanzanian shillings with the emphasis that the society can contribute and make change to solve the challenges by calling upon organisation and individuals to contribute to this noble cause.
 

Sasa kwa nini elimu ikumbwe na ufisadi hivi?


Ufisadi shuleni haukumbi tu Afrika bali Ulaya pia kuna tatizo hilo
Ufisadi katika sekta ya elimu, ni tatizo sugu na bila shaka unahujumu hadhi ya elimu na uwepo wa shule na vyuo vikuu kote duniani . Hii ni kwa mujibu wa taarifa za ripoti ya kimataifa.
Shirika la kimataifa la Transparency International limechapisha utafiti unaoonyesha kuwa mwanafunzi mmoja katika kila wanafunzi sita, alilazimika kulipa rushwa ili apokee huduma za elimu.
Katika baadhi ya sehemu za Kusini mwa jangwa la Sahara na barani Asia, ufisadi unaowalazimisha wazazi kulipa kiwango kidogo cha pesa kwa nafasi ya shule ambayo alipaswa kuipata bila malipo.
Nako barani Ulaya hasa Mashariki mwa Ulaya, watu wanalazimika kulipa rushwa ili waweze kupata nafasi katika chuo kikuu.
Shirika hilo la mjini Berlin linalojulikana , kwa kuchunguza viwango vya pesa zinazotozwa kwa njia isiyo halali katika zaidi ya nchi 100, ilizingatia zaidi ya nyumba
114,000 kwa mahojiano.
Katika baadhi ya nchi ripoti hiyo inasema kuwa karibu thuluthi tatu ya watu nchini Cameroon na Urusi, wanaona mfumo wao wa elimu kama uliokumbwa na ufisadi si haba.
Hali halisi za shule barani Afrika
Nchini Urusi ufisadi umekithiri katika mfumo wake wa elimu
Madai ya ufisadi yalichocheza maandamano ya walimu nchini Brazil.
Matokeo ya utafiti yanaonyesha viwango vya juu sana vya rushwa katika sekta ya elimu.
Na nchini Pakistan, kulikuwa na onyo la maelfu ya shule hewa bila ya wanafunzi ingawa zilikuwa zinazopokea ufadhili wa kuwalipa walimu hewa.
Mapengo katika sekta ya elimu Kenya yalisababisha kupoteza kwa vitabu milioni 11. Nachini Tanzania , katika utafiti wa shule 180, iligunduliwa kuwa ufadhili haukuwafikia wanafunzi na shule husika.
Nchini Ugiriki, kulikuwa na tatizo la mapendeleo katika kutoa nafasi za kazi na watu kupandishwa cheo katika vyo vikuu.

Sasa kwa nini elimu ikumbwe na ufisadi hivi?

Wazazi wanawataka watoto wao wapate elimu nzuri na wanaweza kuhadaiwa na maafisa wanaodhibiti mifumo ya elimu hasa katika mataifa ya kiafrika ambako nafasi zaidi zinahitajika za watoto kusoma.
Nchini Nigeria dola milioni 21 zilipotea kwa miaka miwili
Pia yote haya yanahusu pesa nyingi za serikali zinazotolewa kwa shule za serikali. Nchini Nigeria ripoti hiyo imesema kuwa dola milioni 21 za kimarekani zilizonuiwa kwa matumizi ya shule, zilipotea kwa kipindi cha miaka miwili.
Lakini ni tatizo tu kwa mataifa yanayostawi au wale wanaotoa huduma muhimu za shule.
Hitaji la nafasi nyingi kusoma katika vyuo vikuu pia imekuwa fursa kwa watu kujipatia pesa nyingi sana kwa kutoza ada zisizohitajika.
Kutokana na pesa nyingi zinazohitajika, watu wanalazimika kununua hati bandia za kuonyesha kuwa wamefuzu shahada na tatizo hilo liko nchini Marekani na pia katika mataifa ya kiafrika ikiwemo Kenya.
Shirika la kimataifa la Transparency International linasema kuwa ufisadi umeathiri pakubwa elimu na hata kushusha hadhi ya elimu wanayopokea wanafunzi siku hizi kote duniani.
Hata hivyo kuna habari njema kwenye ripoti hiy: juhudi za kupambana na uifisadi shuleni.
Nchini Chile mafunzo ya kupambana na rushwa yamejumlishwa kwenye mtaala wa shule na nchini Bangladesh walimu hulazimika kuapa kuwa na maadili mema.
Kuwepo kwa simu za mkononi pia kumesaidia watu kuweza kuripoti visa vya ufisadi shuleni.
Pia kuna juhudi za kimataifa kuchunguza matumizi ya pesa za shule.
Lakini ufisadi ungali unaathiri sana bajeti za shule.

chanzo. bbcswahili.com

Jumatano, 9 Oktoba 2013

Mishahara ya viongozi tunaowachagua ni changamoto kupatikana kwa elimu ya bure nchini



HATIMAYE Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, ameweka wazi mshahara wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Zitto ameutaja mshahara huo wa Pinda anayejitambulisha kama ‘mtoto wa mkulima’ juzi mjini Mpanda na jana wilayani Sikonge wakati akihutubia mikutano ya hadhara katika ziara ya Kanda ya Magharibi kwa ajili ya ujenzi wa chama.

Alisema Pinda anapokea jumla ya sh milioni 26, ambazo ni kiasi kikubwa kulinganisha na uchumi wa nchi.

Akichanganua alisema Pinda anapokea sh mil. 11.2 kama mbunge, sh mil. 8 kwa nafasi ya waziri na kiasi kinachosalia kufikia sh mil. 26 kwa nafasi yake ya uwaziri mkuu.

Alisema sababu hiyo ya mishahara mikubwa isiyokatwa kodi ndiyo huwafanya viongozi wa serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa wakali pale vyombo vya habari vinapotaka kuwafahamisha wananchi namna watumishi wao wanavyojilipa.

“Nimeanza na mshahara wa waziri mkuu pia siku zijazo nitataja na wa rais, kwa kuwa amesaini makubaliano na Serikali ya Marekani kuendesha nchi kwa uwazi, na moja ya uwazi ni kwa muajiri kujua kiasi anachomlipa mwajiriwa wake,” alisema Zitto.

Hatua ya Zitto imekuja baada ya kuwapo mvutano mkubwa kuhusiana na kile kinachodaiwa ‘usiri’ wa mishahara ya watumishi wa umma, wakati ni haki ya walipa kodi kujua kile wanachowalipa walioomba kuwaongoza.

Kodi ya laini za simu

Akizungumzia sakata la kodi katika laini za simu, Zitto alisema CCM ina ajenda ya kisiasa kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2015.

Alisema serikali baada ya kubaini watu wengi wanapeana taarifa kwa njia ya ujumbe mfupi, hususan katika masuala ya kisiasa, wakaona njia sahihi ya kudhibiti ni kuwatoza kodi ya laini ili kupunguza hatari ya mawasiliano hayo kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu ujao.

“Sikuwepo bungeni wakati wabunge wa CCM wanapitisha kadhia hiyo ya kuwanyonya wananchi, wenzangu wakaniambai tukasema hapana, kwa maana tuliona hii leo kuna Watanzania wengi wasio na uwezo wa kuhudumia simu kwa kiasi cha sh 1,000 kwa mwezi,” alisema Zitto.

Akijibu maswali ya wananchi mjini Mpanda waliotaka kujua sababu ya kupunguza makali bungeni, Zitto alisema hakuna makali yaliyopungua bali ni mitazamo ya watu.

Alisema kwa kushirikiana na wabunge wenzake wa upinzani wamekuwa wakisimamia hoja zenye manufaa kwa wananachi huku wabunge wanaojipambanua kuwa majasiri kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakiwaunga mkono wazi wazi.

Akiwa wilayani Sikonge, Zitto alisema Watanzania hawawezi kujivunia uhuru huku mama zao, watoto wao na wazee wao wakiwa hawana uhakika wa kupata huduma bora ya afya, elimu na maji safi.

Alisema kwa sasa Tanzania ni taifa moja lililogawanyika katika nchi mbili za wenye fedha na wasio na fedha.

Alisema nchi ya wenye fedha, familia zao husoma katika shule bora, zenye mazingira bora na walimu wazuri, hutibiwa katika hospitali zenye hadhi na huduma muhimu na ikibidi nje ya nchi, huku nchi ya wasio na fedha familia zao wakiishi kwa shida, kusoma katika majengo ya shule na walimu wasiopata mishahara ya kuridhisha na hospitali zisizokuwa na huduma muhimu licha ya kuchangia kiasi cha fedha kwa ajili ya bima ya afya.

(chanzo Tanzania daima)

wanafunzi kidato cha pili wafanya mtihani

Dar es Salaam. Jumla ya watahiniwa 531,457 wa kidato cha pili wanatarajia kufanya mtihani utakaoanza kesho Oktoba 7 hadi 21 mwaka huu.Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome  alisema mitihani hiyo itafanyika kwa wiki mbili.
Alisema kati ya idadi hiyo, wasichana ni 270,734  sawa na asilimia 50.9 na wavulana ni 260,723 sawa na asilimia 49.1.Mchome alisema katika taarifa yake kwamba idadi ya shule na vituo vilivyosajiliwa kufanyia mtihani huo mwaka huu ni 4,437  ikiwa ni ongezeko la vituo 140 sawa na asilimia 3.3 ikilinganishwa na vituo 4,297 vilivyosajiliwa mwaka 2012.
Alisema watahiniwa waliojiandikisha wanajumuisha makundi maalum yenye uoni hafifu, ambao ni 89 na wasioona 93.ìKaratasi za mtihani wa watahiniwa wenye mahitaji maalum zimeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji yao kama vile kutumia karatasi za maandishi yenye nundu kwa wasioona na kuongeza ukubwa wa maandishi kwa wenye uoni hafifu,î alisema.
Mchome alisema umuhimu wa mtihani huo ni kupima kiwango cha maarifa na ujuzi alioupata mwanafunzi kutokana na mada alizojifunza katika kidato cha kwanza na cha pili.
Pia alisema mtihani huo unatoa changamoto zinazosaidia wanafunzi, walimu, wizara na wadau wa elimu kutambua mapungufu yaliyopo katika ufundishaji ili yaweze kufanyiwa marekebisho kwa lengo la kuboresha elimu.
chanzo. mwananchi.co.tz

Wanafunzi 2,446 hawapati chakula cha WFP






IMEELEZWA kuwa wanafunzi 2,446 waliopo katika shule za msingi za wilayani Bahi, mkoani Dodoma, hawapati chakula kinachotolewa kwa msaada na Shirika la Chakula Duniani (WFP) kutokana na shule hizo kukosa majengo ya kuhifadhi chakula.

Hayo yalibainishwa jana na Ofisa Elimu wa Shule za Msingi Bahi, Mary Mathew.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Mary alisema ukosefu wa majengo unatokana na wazazi kutokuwa tayari kujitolea kujenga.

Alisema msimamo wa WFP uko wazi kwamba hawako tayari kutoa chakula kwenye shule zisizo na majengo ya kuhifadhiwa chakula.

Alieleza kuwa katika Wilaya ya Bahi, kuna shule za msingi 72 na kati ya hizo shule saba hazipati chakula cha mchana kutokana na wazazi kutoitikia mwito wa kujitolea.

Ofisa Elimu huyo alisema hali ya kukosekana kwa huduma ya chakula kwenye shule hizo imesababisha utoro kwa wanafunzi.

Shule ambazo hazipati chakula cha mchana ni pamoja na Nholi, Bakolo, Chikopelo Nhinyila, Tinai, Mgondo na Bahi Misheni.
 
Chanzo. Marafiki wa elimu dodoma

Jumapili, 6 Oktoba 2013

KAMATI YA SHULE YAONYESHA MFANO WA UWAZI,UWAJIBIKAJI NA DEMOKRASIA

Mwenyekiti wa kamati ya shule pamoja na diwani
Ramani ya choo inavyoonekana
Wajumbe wakimsikiliza diwani

Alhamisi, 3 Oktoba 2013

Wanaorudia mitihani kidato cha pili watahadharishwa


 Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome
 
Wanafunzi 136,923 wa kidato cha pili wanaorudia mitihani, wapo hatarini kutimuliwa shuleni na kurudi mitaani ikiwa watashindwa kufaulu kwa mara ya pili baada ya serikali kuwapa nafasi ya mwisho mwaka huu 2013 kurudia.

Kati ya wanafunzi hao, wavulana ni 74,020 na wasichana ni 62,903, ambao mwaka jana walifeli mitihani ya kidato cha pili na serikali kuamua kuwapa nafasi ya mwisho ili wajaribu tena mwaka huu.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome, alisema jana kuwa mwaka huu mitihani ya pili itafanyika kati ya Oktoba 7 hadi 21 na kwamba, jumla ya watahiniwa 531,457 wataifanya, wakiwamo wa shule binafsi na za serikali.

Alisema vituo vilivyosajili watahiniwa ni 4437, ikiwa ni ongezeko la vituo 140 sawa na asilimia 3.3 ikilinganishwa na vituo 4,497 vilivyosajiliwa mwaka jana.

Alisema sera ya wizara yake inasema mwanafunzi anayefeli mara ya pili mitihani hiyo ataondolewa shuleni kwa maana ya kuendelea na mfumo rasmi na kwamba, msimamo huo hautabadilika.

Ikiwa serikali itaendelea na msimamo huo, wanafunzi 136,923 waliofeli mwaka jana ikiwa pia mwaka huu watafeli watalazimika kurudi nyumbani kwa kuwa serikali haitawapokea katika mfumo rasmi wa elimu.

Profesa Mchome alisema wanafunzi watakaofeli kwa mara ya pili, labda wajaribu kujisomea wenyewe ili wafanye mitihani ya QT, ambayo mara nyingi hufanywa na watu wazima ama waende katika vyuo vya ufundi ikiwa Veta.

Watahiniwa wa mwaka huu, wasichana ni 270,734 (sawa na asilimia 50.9) na wavulana 260,723 (sawa na silimia 49.1), wakiwamo wanafunzi wenye ulemavu wa kuona.

chanzo. ippmedia.com

Jumatano, 2 Oktoba 2013

Serikali kutoa ruzuku kwa shule binafsi

Serikali inatafakari uwezekano wa kutanua wigo wa kutoa ruzuku hadi kwa shule zinazomilikiwa na watu binafsi, ikiwa ni sehemu ya azma ya kuzipunguzia gharama za uendeshaji.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene, amesema hayo wakati akizungumza kwenye mahafali ya darasa la saba katika Shule ya St. Anne Marie Academy jijini Dar es Salaam jana.Alisema shule nyingi za binafsi zinafungwa kutokana na kushindwa kujiendesha miongoni mwa sababu kubwa ikiwa ni kupanda kwa gharama za uendeshaji.

Simbachawene alisema kuziacha shule binafsi `zife’ kutokana na sababu iliyo ndani ya uwezo wa nchi kuitatua, ni hasara kwa taifa na kwamba njia pekee ya kuzisaidia kwa kuzipa ruzuku ili ziweze kujiendesha.

Kwa mujibu wa Simbachawene, shule binafsi zimesaidia kwa kiasi kikubwa kuinua kiwango cha elimu, hivyo kupunguza idadi na kasi ya Watanzania kupeleka watoto wao kusoma nje ya nchi.Alisema: "Ukiacha shule kama hii (St. Anne Marie) ikafa ni hasara kwa taifa, serikali inaangalia kuona namna bora ya kuzisaidia kwa kuzipatia ruzuku ili kuzipunguzia gharama za uendeshaji.”

Kwa upande mwingine, Simbachawene aliwaasa vijana kuwa makini katika kukabiliana na kuzishinda changamoto zilizo katika jamii, ikiwamo maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) na matumizi ama usafirishaji wa dawa za kulevya.

Meneja wa shule hiyo, Jasson Rweikiza, alisema serikali imekuwa na kigugumizi katika mambo mbalimbali katika sekta ya elimu, hali inayosababisha  kudumaa kwa sekta hiyo na watoto kukosa ufaulu mzuri.

Kwa mujibu wa Rweikiza ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba Vijijini, mpaka sasa mitaala ya elimu na sera za elimu hazipo wazi, hali inayosababisha walimu wakose mwongozo wa kufundishia.

Alisema wadau wa elimu hususani wamiliki wa shule binafsi, wanakabiliwa na kazi kubwa ya uendeshaji, huku kukiwa na changamoto kadhaa kama vile matumizi ya mitaala isiyoeleweka.

Pia alisema sera zinazohusiana na elimu hazipo wazi, na kutoa mfano kuwa sera haielezi kama ni kosa ama si kosa inapotokea kuwapo mwanafunzi asiyejua kusoma.
“Maendeleo hayawezi kwenda bila kuboresha sekta ya elimu...tunaiomba serikali isimame imara katika kuinusuru sekta ya elimu nchini,” alisema.

Rweikiza alisema wahitimu wa darasa la saba wanapaswa kuondokana na dhana inayowafanya kujiona wamemaliza shule, bali kiwango hicho kuwa msingi wa safari ndefu inayowakabili maishani.

ippmedia.com

Walimu 344 wafukuzwa kazi 2008- 2013

Walimu 344 nchini wamefukuzwa kazi kutoka mwaka 2008 hadi mwaka huu kutokana na makosa mbalimbali ikiwamo kuwapa mimba wanafunzi.Hayo yalisemwa na Katibu Msaidizi wa  Ajira na Maendeleo ya Watumishi (TSD), Christina Hape, jijini Dar es Salaam jana.

Hape alisema mwalimu anatakiwa kuwa kama mlezi wa wanafunzi, lakini suala la kuwapa mimba linapokuja ni kosa la jinai na kwamba ni lazima wapelekwe polisi kwa ajiri ya kuchukuliwa hatua.Kwa upande wake, TSD pamoja na Tume ya Utumishi wa Umma wanaweza kuwafukuza kazi walimu.

Alisema  katika kipindi cha mwaka 2008 hadi 2009 wamefukuzwa walimu  40, mwaka 2009 hadi 2010 walimu 20 , mwaka 2010 hadi 2011 walimu 13  na mwaka 2011 hadi  2012 walimu 11 walifukizwa.Aliongeza kuwa mpaka sasa walimu 84 walifukuzwa kazi baada ya kubainika makosa yao ya kuwapa mimba wanafunzi.

Hata hivyo, alisema ugumu unakuja pale wazazi wanapokosa kutoa ushirikiano kwa serikali kwa kutohudhuria mahakamani na kuamua kulimaliza baada ya mtuhumiwa huyo kuwashawishi kwamba atamuoa binti yao.

Kwa upande wa makosa ya utoro kwa mwaka 2011 hadi 2012 walimu 152 na mwaka 2012 hadi 2013 walimu 157 walifukuzwa kazi .Alisema kwa wastani walimu wapatao 260 mpaka sasa wamefukuzwa kazi kutokana na utoro wa maeneo ya kazi.

Naibu Katibu Tume ya Utumishi wa Umma, Idara ya Utumishi wa Walimu, Edwini Mokongoti, alisema ili kuwezesha ufanisi katika utekelezaji wa masuala ya kiutumishi wakuu wa vyuo vya ualimu, vyuo vya maendeleo ya jamii, wakuu wa shule na walimu wakuu wanatakiwa kuwajibika katika kuwaelimisha walimu taratibu za masuala ya ajira katika maeneo mbalimbali ikiwamo kupandishwa vyeo, ajira na usajili.

Alisema pia wakuu hao watashughulikia makosa madogo madogo ya kinidhamu na kutoa adhabu, ambayo kwa mujibu wa kanuni namab 118 ya kanuni za utumishi wa umma ya mwaka 2003 zitakuw a, onyo, kusimamisha nyongeza ya mshahara kufidia hasara au sehemu ya hasara ambayo mtumishi itaisababishai serikali kutokana na uzembe wake.

ippmedia.com

mabunge ya wanafunzi yanawajengea wanafunzi uwezo wa kujieleza