Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumamosi, 19 Julai 2014

Waliohitimu la 7 Vijibweni waitwa kuchukua vyeti



BAADA ya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Vijibweni, Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, Mathew Jasembe kutuhumiwa kupoteza vyeti vya wanafunzi 247 waliohitimu darasa la saba mwaka 2011 amewataka wafike shuleni kuchukua vyeti vyao.
Tuhuma hizo ziliibuliwa na baadhi ya wazazi wa wanafunzi hao, wakisema wamechoshwa na ahadi za mwalimu huyo kwa zaidi ya miaka miwili sasa tangu vyeti hivyo kupotea, ziliandikwa na gazeti hili hivi karibuni.
Wazazi hao walidai mkuu huyo alihusika kwa sababu hakuwa wazi kueleza mazingira halisi ya jinsi vyeti hivyo vilivyopotea na kwamba hakupenda suala hilo lifike ngazi za juu.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, mwalimu huyo, alisema tofauti zilizojitokeza awali hadi kusababisha vyeti hivyo kuchelewa kukabidhiwa kwa wahitimu zimepatiwa ufumbuzi na vyeti hivyo vipo tayari.
Alisema baada ya mchakato wa kuviandaa vyeti hivyo kukamilika tangu juzi, klichobaki ni kuwakabidhi wahitimu hao.
“Mbona nimeanza kuwakabidhi wachache waliopata taarifa… nimeweka matangazo katika eneo linalozunguka shule kwa ajili ya kuwajulisha kuwa vyeti vyao vipo tayari ni wao wenyewe sasa.
“Niwaombe wazazi kupitia gazeti lenu wa waambie watoto wao waende shuleni hapo wakachukue vyeti vyao,” alisema Jasembe.
Hivi karibuni wazazi wa watoto hao, walifikisha tuhuma hizo kwa Mbunge wa Kigamboni, Faustine Ndugulile, Ofisa Elimu na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke.