Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumanne, 3 Septemba 2013

KUWAFUKUZA WANAFUNZI WA KIKE WANAOPATA MIMBA NI KUKATISHA NDOTO ZAO


 
Hukumu ya hivi karibuni ya mahakama ya kikatiba imethibitisha kwamba shule haziwezi kuwafukuza wanafunzi kwa kupata uja uzito.Lakini Afrika Kusini bado inang'ang'ana kukabliana na suala hilo linalowaathiri wasichana 180,000 kila mwaka.


Daktari Jay-Anne Devjee ambaye ni mkuu wa afya ya akina mama katika hospitali ya King Dinuzulu anasema kwa mara nyingi hulazimika kuwazalisha wasichana kwa njia ya upasuaji, jambo linaloongeza hatari ya kuvuja damu na kuhatarisha maisha ya wazazi hao.
Msichana mwenye umri mdogo zaidi hapa ana umri wa miaka 14 na anaonekana kuzidiwa na uchungu wa uzazi kiasi cha hata kushindwa kuongea.
Phumla Tshabalala, mwenye umri wa miaka 16, anamshikilia mwanawe mchanga aliye na umri wa siku moja.Hii ni mara yake ya kwanza kujifungua na anasema ana wasiwasi kuhusu uwezekano wa kumlea mwanawe peke yake.
Anaeleza hajamuona mpenzi wake kwa muda mrefu na licha ya kumuarifu kwamba amejifungua, hakuna mtu kutoka familia ya mpenzi wake aliyekuja kumjulia hali.
Anatoka katika familia maskini, Babake ndiye anayeilisha familia. Yeye ni binti wa mwisho kati ya mabinti watatu na wa kwanza aliyejifungua mtoto, jambo ambalo familia yake bado haijalipokea vyema.
Inakisiwa kuwa kila mwaka wasichana zaidi ya laki moja na themanini nchini Afrika Kusini hushika ujauzito. 180 kati ya wengine 1000, hupata kuwa wajawazito. 36% ya wasichana wenye mimba hufariki kila mwaka kulingana na takwimu za nchi hiyo wakati wanapojifungua.
Mifuko yao ya uzazi huwa bado haijakuwa vyema kiasi cha kubeba mimba na wengi huwa na wakati mgumu sana wanapojifungua , kulingana na daktari Jay-Anne Devjee.
Phumla anapanga kurudi shuleni kwa wakati muafaka ili aweze kufanya mtihani wa mwisho wa mwaka , lakini ana wasiwasi kuhusu vipi atakavyoweza kutimiza majukumu yote mawili ya kuwa mwanafunzi na mzazi pia.

Anasema laitani angesubiri hadi angekuwa mkubwa.

Lakini anajiona kuwa mwenye bahati kwa kuwa yeye na mwanawe ni wazima na wenye afya.
Madakatari wanasema kuna hatari ya kuzaa ukiwa una umri mdogo. Kwa mujibu wa baraza la utafiti wa sayansi ya binaadamu, viwango vya akina mama wanaofariki ni kubwa kwa wasichana kwa asilimia 36 ya vifo katika uzazi kila mwaka licha ya kwamba ni asilimia 8 pekee ya vifo hivyo ndivyo vinavyoripotiwa.
Utafiti unaashiria kwamba wasichana wengi hulazimika kuacha masomo ili kuwalea watoto wao na wengi wao hukosa kurudi kusoma baadaye.
Maafisa wa elimu wanasema katika shule ya upili wa Intshisekelo nje ya mji wa Durban, zaidi ya wasichana 20 walipachikwa mimba katika nusu ya kwanza ya mwaka.
Maafisa nchini humo wana wasiwasi kwamba huenda kushiriki kwa vijana katika ngono bila ya kinga kukaathiri vita dhidi ya HIV/Ukimwi. Mwalimu mmoja anasema mimba ni miongoni mwa sababu kuu pamoja na umaskini zinazochangia nusu tu ya wanafunzi wa kike kumaliza shule.
Kwa mujibu wa sheria, shule hazipaswi kufichua ni wanafunzi gani waja wazito na inasema baadhi ya wasichana huwa na kibarua kigumu cha kificha matumbo yao yanayozidi kukuwa ikwemo kuvaa nguo kubwa na pia kubeba mabegi yao ya shule mbele.
Sheria hiyo ya mwaka 1996 inasema wanafunzi hawapswi kufukuzwa kwa kuwa ni waja wazito lakini shule zinasema wanalazimika kuwafukuza kwa sababu hazijapewa mafunzo ya namna ya kuwasaidia wasichana hao waja wazito.