Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Alhamisi, 5 Septemba 2013

WATANZANIA WATOA MAONI YAO TOVUTI YA WIZARA YA ELIMU



Ukifungua tovuti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, pembeni kushoto kuna sehemu ya kupiga kura ya maoni kuhusu hali ya elimu nchini. Kwa maoni yaliyopo mpaka sasa, asilimia 42 ya waliotoa maoni yao-wana mtazamo kuwa hali ni mbaya; wakifuatiwa na asilimia 35 wenye mtazamo kwamba 'kuna kitu hakiko sawa'. Maoni hayo yasiyo ya kuridhisha-yanayofikia asilimia 77 yametumwa na wananchi na wadau mbalimbali wa elimu kwenye tovuti ya wizara ya elimu. Je, wizara inayatumiaje maoni haya ya wadau? Big Result ndiyo jawabu?