Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumamosi, 2 Novemba 2013

kufutwa kwa division ziro je ni mpango wa kutekeleza Big results now

hivi karibini serikali imetangaza mabadiliko ya alama za ufaulu kama inavyoonekana hapo chini

A ni 75 hadi 100; huu ni ufaulu uliojipambanua
B+ ni 60 hadi 74; huu ni ufaulu bora sana
B ni 50 hadi 59; huu ni ufaulu mzuri sana
C ni 40 hadi 49; huu ni ufaulu mzuri
D ni 30 hadi 39; huu ni ufaulu hafifu
E ni 20 hadi 29; huu ni ufaulu hafifu sana
F ni 0 hadi 19; huu ni ufaulu usioridhisha

Kimsingi alama yoyote kuanzia sifuri hadi mia moja ni ufaulu wa aina flani;

Madaraja yatakuwa kama ifuatavyo;

Division One = pointi 7 hadi 17
Division Two= pointi 18 hadi 24
Division Three = pointi 25 hadi 31
Division Four= pointi 32 hadi 47
Division Five = pointi 48 hadi 49

Yaani mtu akipata E mbili na F tano, ana division four; au akipata D moja na F sita atakuwa na division four.

swali la msingi tunalopaswa kujiuliza ni je huu ndio utekelezaje halisi wa MATOKEO MAKUBWA SASA na kama ndio utekelezaje serikali haijaweka wazi na kuwaelimisha wadau juu kusudio hasa lililopelekea kupangwa kwa alama za ufaulu marafiki wa elimu tunaamini kwamba kupangwa kwa alama za ufaulu si suruhisho la matatizo ya elimu yanayokabili nchi ila tunaamini kuwa serikali ikitekeleza malengo yaliyobainisha kwenye vipaumbele vya mpango wa big results now elimu itafanikiwa kwa kiwango kikubwa sana.