Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumanne, 29 Julai 2014

ZAIDI YA WANAFUNZI 860 WA SEKONDARI WILAYANI KILINDI WAMEACHA SHULE.


Wanafunzi zaidi ya 860 wa shule mbali mbali za sekondari wilayani Kilindi wameacha shule kwa sababu mbali mbali ikiwa ni pamoja na baadhi ya wazazi wao kuwaozesha huku wengine wakiwekwa kinyumba na baadhi ya makundi ya vijana.
Mkuu wa wilaya ya Kilindi bwana Selemani Liwowa amesema hayo katika kikao cha baraza la madiwani ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Dr . Jakaya Kikwete kuwataka viongozi wa mkoa wa Tanga kuhakikisha kuwa watuhumiwa waliosababisha tatizo hilo wanakamatwa na kufunguliwa kesi katika vyombo vya sharia.
Akielezea mikakati waliyojiwekea na hatua zitakazochukuliwa mkuu huyo wa wilaya amesema kwanza wanataka wawarejeshe watoto hao kwa wazazi kisha watawakamata wazazi na watuhumiwa waliowakatisha masomo kwa ajili ya kuwachukulia hatua kali za kisheria zoezi ambalo linaanza utekelezaji wake baada ya sikukuu ya eid kumalizika.


chanzo ITV

Wanafunzi 140 wakwepa masomo tunduma na kujihusisha na biashsra ndogondogo.

Zaidi ya wanafunzi 140 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu katika halmashauri ya mamlaka ya mji mdogo wa Tunduma wilayani momba mkoani Mbeya bado hawajaripoti shuleni kuanza masomo na badala yake wanadaiwa kujihusisha na biashara ndogondogo kama vile kuuza karanga na kubeba mizigo mpakani mwa Tanzania na Zambia mjini Tunduma.
Akizungumza kwenye baraza la halmashauri ya mamlaka ya mji mdogo wa Tunduma, mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya momba ambaye pia ni katibu tawala wa wilaya hiyo, Mathias Mizengo amesema kuwa halmashauri ya mamlaka ya mji mdogo wa Tunduma inakabiliwa na changamoto ya baadhi ya vijana ambao wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu kutoripoti shuleni na hivyo akawataka viongozi wa mamlaka hiyo kuhakikisha vinaja hao wanatafutwa kila mahali walipo na kuwapeleka shuleni.
 
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Juma Kitabuje amesema kuwa hadi kufikia mwezi juni mwaka huu wanafunzi 144 kati ya wanafunzi 956 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika mji wa Tunduma ndio ambao walikuwa hawajaripoti shuleni kati yao wanafunzi 70 wakiwa ni wavulana na wanafunzi 74 wasichana huku akielezea sababu kubwa ya watoto hao kutohudhuria masomo kuwa ni kutelekezwa na wazazi na kujihusisha na biashara za kuuza karanga na kubeba mizigo mpakani.
 
Kuhusu hatua ambazo zinachukuliwa na mamlaka hiyo kuhakikisha kuwa wanafunzi hao wanaendelea na masomo, mkurugenzi huyo amesema kuwa wazazi wa watoto hao wamefikishwa kwenye baraza la kata na kupewa muda hadi kufikia Agosti 25 mwaka huu kuwasaka watoto wao popote walipo na kuwapeleka shuleni.

Kwa wasiomfahamu mwalimu.

Mwalimu JK Nyerere

1. Ndiye rais aliyewahi kulipwa mshahara kidogo duniani
 
2.ndiye mtu aliyeitetea china isitengwe na UN, baada ya mataifa yote kuogopa vtisho vya marekani, wachina wanamtambua na kumheshimu sana

 
3. Ndiye rais pekee aliyetishia kuvunja balozi za uingereza, ujeruman na ufaransa na hata kukataa msaada wao kwa kitendo chao cha kuunga mkono serikali ya kibaguz afrika kusini

 
4. Ndiye rais aliyewezesha watoto wa masikin wasome bila ada na matibabu bure. Nenda nchi za kenya, afrika kusini . Kama baba yako hakushirik harakati za ukomboz ili utoke labda uwe jambaz maana huwez hata kujilipia ada


Ndiye rais pekee aliyechukia ufisadi toka moyoni.