Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatano, 26 Februari 2014

kusoma na kuhesabu bado changamoto shule za msingi nchini

Tangu mwaka 2010, taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Twaweza kupitia mradi wake wa Uwezo, imekuwa ikifanya tafiti katika nchi za Afrika Mashariki zinazolenga kubaini uwezo wa watoto wa shule za msingi katika stadi za kusoma na kuhesabu.
Majaribio haya, yamekuwa yakihusisha masomo ya Hesabu na lugha za Kiswahili na Kiingereza kwa ngazi ya darasa la pili. Sampuli hujumuisha wanafunzi wa darasa la tatu na darasa la saba.
Sampuli ya washiriki
Takwimu zinaonyesha kuwa, mwaka 2010 watoto walioshirikishwa kwenye utafii huo walikuwa 37,683 mwaka 2011 wanafunzi 114,761 na mwaka 2012 wanafunzi walioshiriki ni 104,568.
Kwa upande wa kaya, mwaka 2010 zilishiriki kaya 18,952 mwaka 2011 zilikuwa kaya 59,992 na mwaka 2012 kaya. 55,191. Kwa wilaya, mwaka 2010 zilishiriki Wilaya 38, mwaka 2011 zilikuwa wilaya 119 na mwaka 2012 wilaya 126.
Shule zilizoshiriki kwenye utafiti uliofanyika mwaka 2010 zilikuwa ni 1,010 mwaka 2011 zilikuwa 3,709 na mwaka jana zikawa 3,624.
Mratibu wa Uwezo upande wa Tanzania, Zaida Mgalla anasema aghlabu majaribio hayo hutayarishwa kwa pamoja na wataalamu wa masomo kutoka vyuo vikuu, Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na walimu wa masomo husika wa darasa la pili.
Matokeo 2010
Utafiti huu ulipofanywa mwaka 2010 ulionyesha kuwa, japo Kiswahili ni lugha inayozungumzwa kwa upana zaidi nchini, idadi kubwa ya watoto hawawezi kusoma kupitia lugha hiyo.
“Kwenye sampuli zetu, chini ya nusu (42.2 asilimia) ya watoto waliofanyiwa uchunguzi waliweza kusoma kwa hatua ya hadithi. Wakati watoto wote katika darasa la tatu wanapaswa kuweza kusoma hadithi ya ngazi ya darasa la pili, watoto chini ya mmoja kati ya watatu (32.7 asilimia) ndio wanaweza.
‘’Hata hivyo, hadi wanamaliza shule ya msingi, mtoto mmoja kati ya 5 hawezi kusoma hadithi ya ngazi ya darasa la pili, licha ya kumaliza miaka saba ya elimu ya msingi,”inasema sehemu ya utafiti huo.
Kwa upande wa Kiingereza, ripoti hiyo ya mwaka 2010 inaonyesha kuwa chini ya mwanafunzi mmoja kati ya 10 (7.7 asilimia) ndio anayeweza kusoma hadhithi ya Kiingereza ya ngazi ya darasa la pili
Tangu mwaka 2010, taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Twaweza kupitia mradi wake wa Uwezo, imekuwa ikifanya tafiti katika nchi za Afrika Mashariki zinazolenga kubaini uwezo wa watoto wa shule za msingi katika stadi za kusoma na kuhesabu.
Majaribio haya, yamekuwa yakihusisha masomo ya Hesabu na lugha za Kiswahili na Kiingereza kwa ngazi ya darasa la pili. Sampuli hujumuisha wanafunzi wa darasa la tatu na darasa la saba.
Sampuli ya washiriki
Takwimu zinaonyesha kuwa, mwaka 2010 watoto walioshirikishwa kwenye utafii huo walikuwa 37,683 mwaka 2011 wanafunzi 114,761 na mwaka 2012 wanafunzi walioshiriki ni 104,568.
Kwa upande wa kaya, mwaka 2010 zilishiriki kaya 18,952 mwaka 2011 zilikuwa kaya 59,992 na mwaka 2012 kaya. 55,191. Kwa wilaya, mwaka 2010 zilishiriki Wilaya 38, mwaka 2011 zilikuwa wilaya 119 na mwaka 2012 wilaya 126.
Shule zilizoshiriki kwenye utafiti uliofanyika mwaka 2010 zilikuwa ni 1,010 mwaka 2011 zilikuwa 3,709 na mwaka jana zikawa 3,624.
Mratibu wa Uwezo upande wa Tanzania, Zaida Mgalla anasema aghlabu majaribio hayo hutayarishwa kwa pamoja na wataalamu wa masomo kutoka vyuo vikuu, Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na walimu wa masomo husika wa darasa la pili.
Matokeo 2010
Utafiti huu ulipofanywa mwaka 2010 ulionyesha kuwa, japo Kiswahili ni lugha inayozungumzwa kwa upana zaidi nchini, idadi kubwa ya watoto hawawezi kusoma kupitia lugha hiyo.
“Kwenye sampuli zetu, chini ya nusu (42.2 asilimia) ya watoto waliofanyiwa uchunguzi waliweza kusoma kwa hatua ya hadithi. Wakati watoto wote katika darasa la tatu wanapaswa kuweza kusoma hadithi ya ngazi ya darasa la pili, watoto chini ya mmoja kati ya watatu (32.7 asilimia) ndio wanaweza.
‘’Hata hivyo, hadi wanamaliza shule ya msingi, mtoto mmoja kati ya 5 hawezi kusoma hadithi ya ngazi ya darasa la pili, licha ya kumaliza miaka saba ya elimu ya msingi,”inasema sehemu ya utafiti huo.
Kwa upande wa Kiingereza, ripoti hiyo ya mwaka 2010 inaonyesha kuwa chini ya mwanafunzi mmoja kati ya 10 (7.7 asilimia) ndio anayeweza kusoma hadhithi ya Kiingereza ya ngazi ya darasa la pili

MATOKEO KIDATO CHA NNE 2013:Elimu yazikwa rasmi

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imetupiwa lawama kwa kuruhusu upangaji wa madaraja ya mitihani ya kidato cha nne unaozua utata na kuwa na dalili za kuzika elimu nchini.

Akizungumza na NIPASHE jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa Shirikisho la Wamiliki na Mameneja wa Shule Binafsi  na Vyuo Visivyo vya Kiserikali (Tamongso), Benjamin Nkonya, ameiambia NIPASHE kuwa upangaji wa madaraja uliofanywa na Necta utaligharimu taifa kwa kiasi kikubwa kwani unaangamiza elimu badala ya kuiinua.

Nkonya alisema kuwa madaraja hayo mapya yaliyotumika katika kutangaza matokeo ya mtihani uliopita ya kidato cha nne yanaonekana kuwa na nia ya kuuonyesha umma kuwa watahiniwa wameanza kufanya vizuri zaidi na kujenga dhana kuwa kiwango cha elimu kinapanda kwavile imepanua wigo wa ufaulu bila kuzingatia haja ya kuboresha maeneo muhimu kama ya uandaaji wa mitaala sahihi na kuboresha mazingira ya utoaji wa elimu yenyewe.

Alisema kuwa wao (Tamongso), walishapinga mara kadhaa utaratibu huo uliotumika sasa lakini wanashangaa kuona kuwa bado serikali kupitia Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) ikitumia madaraja yaleyale waliyokuwa wakiyapinga kila mara.

"Kwa mfano, sisi tulipendekeza alama za ufaulu zianzie angalau alama 35 hadi 50 kwa daraja la nne... wanaopata chini ya hapo watafutiwe utaratibu mwingine ikiwa ni pamoja na kuwapeleka kwenye vyuo vya ufundi. Lakini hilo halijazingatiwa na kilichopo sasa, ni siasa tupu katika elimu ambayo mwishowe itaua elimu," alisema Nkonya.

Mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia, amesema matokeo ya kidato cha nne yaliyotangazwa hivi karibuni ni danganya toto na kama siyo serikali kupandisha madaraja, yangekuwa mabaya kuliko ya mwaka jana kwani wengi waliofaulu, wakifuatilia kiundani ni sawa na wamefeli.

Alisema matokeo hayo ni kucheza na akili za Watanzania hususan walala hoi kwa kuwa katika shule za serikali ambazo kwa sasa zimegeuziwa kisogo, hakuna mtoto wa kiongozi au mtumishi wa umma mwenye kipato cha kati anayesoma huko.

Mbunge wa Ubungo, John Mnyika ameitaka serikali kuboresha mazingira ya kutolea elimu ili kuinua kiwango na siyo kwa njia hii ya kubadili madaraja kwa namna inayotia shaka kwani huko ni kuangamiza elimu nchini.

"Serikali kwa barakoa (veil) ya kutekeleza Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) imeamua kulificha taifa juu ya Matokeo Mabaya ya Sasa (Bad Results of Now).
Hivyo, wachambuzi wa masuala ya elimu wanapaswa kutoa takwimu za matokeo yangekuwa namna gani iwapo viwango vya awali vya ufaulu vingetumika ili nchi ijue hali halisi kwa manufaa ya wananchi," alisema Mnyika.

UTATA
Uchunguzi uliofanywa na NIPASHE kupitia matokeo yaliyotangazwa mwishoni mwa wiki umebaini kuwa mbali na wizara hiyo kushusha sana alama za ufaulu na hivyo kupunguza pia idadi ya watahiniwa waliofeli kutoka asilimia 56.92 ambayo ni sawa na wanafunzi 210,846 mwaka 2012 hadi kufikia asilimia 42.91 (wanafunzi 151,187), bado kumekuwa na matokeo yenye utata, hasa katika vigezo vya kuwapanga waliopata daraja sifuri na wale waliofaulu kwa kiwango cha walau daraja la nne.

Katika baadhi ya shule, NIPASHE imebaini kuwa matokeo hayo yamewachanganya watahiniwa kwa kiasi kikubwa, yakionyesha kuwa baadhi yao wamefeli kwa daraja sifuri licha ya kupata alama za jumla walizoamini kuwa zingewaweka katika kundi la waliofaulu kwa kiwango cha daraja la nne.

Aidha, wengine wamejikuta wakichanganywa pia na matokeo ya wenzao wanaoonekana kupata alama za jumla za chini zaidi lakini bado wakipewa daraja la nne.

Miongoni mwa matokeo hayo ya utata yanaonekana katika Shule ya Sekondari Wigamba iliyopo Mbeya mjini na pia katika Shule ya Sekondari Dr. Nchimbi, hasa tofauti ya alama kati ya madaraja ya nne na sifuri. Baadhi ya wanafunzi katika shule hizo wanaonekana kufeli vibaya kwa kupata daraja la sifuri, licha ya jumla ya alama walizopata kuonyesha kuwa ni 42.

Kwa mujibu wa upangaji mpya wa madaraja wa NECTA, daraja la sifuri huanzia alama 47 hadi 49 huku daraja la nne likiwa ni kwa ajili ya watahiniwa waliopata jumla ya alama zinazoanzia 32 hadi 46.

Katika shule ya Wigamba, mtahiniwa mvulana mwenye namba S3133/0054 anaonekana akiwa amepata daraja la sifuri licha ya kupata alama 43. Huyu amepata D ya English na E za masomo ya Civics, Kiswahili na Biology huku akiwa amefeli kwa kupata F katika masomo mawili ya Historia na Hisabati.

Hata hivyo, mtahiniwa mwingine katika shule hiyo hiyo ya Wigamba, mwenye namba S.3133/0010 amefaulu kwa kupata daraja la nne licha ya kwamba jumla ya alama zake kuwa 44, moja zaidi ya mtahiniwa S.3133/0054 aliyepata sifuri. Mwingine aliyepata sifuri licha ya kupata alama 42 ni mtahiniwa mwenye namba S.3133/0092 wakati mwenzake mwenye namba S.3133/0100 akifaulu kwa kiwango cha daraja la nne licha ya alama zake kuwa sawa na yeye ambazo ni 42.

Mifano mingine inayoashiria utata au kutoeleweka wazi kwa mfumo mpya wa madaraja ni pamoja na matokeo ya mtahiniwa mwenye namba S.1877/0007 wa Shule ya Sekondari ya Dr. Nchimbi. Huyu anaonekana kufaulu kwa kupata daraja la nne licha ya kuwa na pointi 46, akipata C ya Kiswahili na F za masomo sita ya Civics, History, Geography, English, Chemistry, Biology na Basic Maths.

Mtahiniwa mwenye namba S1877/0006 wa Shule ya Sekondari Dr. Nchimbi pia anaonekana kupata daraja la nne licha ya kuwa na alama 46 wakati mwanafunzi mwingine wa shule hiyo hiyo, mwenye namba S1877/0170 akifeli kwa kupata daraja sifuri licha ya kuwa na alama 46 kama mwenzake mwenye namba S1877/0006. 

Kwa mujibu wa NECTA, madaraja mapya yaliyotumika sasa yanaonyesha kuwa sawa na yale yaliyowahi kutangazwa na Profesa Sifuni Mchome na kupingwa na baadhi ya wabunge ambayo ni daraja la kwanza lililiobaki vilevile kuanzia alama za jumla 7 hadi 17, daraja la pili likibadilika kutoka 18-21 hadi 18-24, daraja la tatu kuwa 25-31 badala ya 22-25 ; daraja la nne kubadilika kutoka 26-32 na kuwa 32-46 huku daraja sifuri likiwa 47 hadi 49.

Aidha, katika utaratibu wa sasa, A huanzia 75-100; B+ ni 60-74; B ni 50-59 wakati C ni alama kuanzia 40 hadi 49. Mgawanyo mwingine unaonyesha kuwa D huhusisha alama kati ya 30 hadi 39, E ni 20 hadi 29 na F huhusisha ufaulu wa alama 0-19.

Hata hivyo, ilitarajiwa kuwa kutokana na mabadiliko hayo, wale waliopata alama za jumla kuanzia 32 hadi 46 wangekuwamo katika orodha ya waliofaulu kwa kiwango cha daraja la nne na siyo sifuri.  

NECTA YAFAFANUA
Akizungumzia kuhusu utata wa madaraja, Afisa Uhusiano wa Necta, John Nchimbi, aliiambia NIPASHE jana kuwa ufaulu wa daraja la nne hautegemei alama za jumla peke yake bali ni pamoja na sharti lake kuu ambalo ni lazima kila mtahiniwa awe amepata angalau D mbili na C moja.

Aliongeza kuwa kifungu cha 20 (6) cha Kanuni za Mitihani ndicho kinachoeleza wazi kuhusu vigezo vya ufaulu wa daraja la nne ambavyo ni pamoja na ulazima wa kufaulu kwa kiwango cha C au D mbili na siyo wingi wa alama.

Alieleza dhana nyingine za madaraja hayo mapya kuwa ni pamoja na kuangalia viwango vya ufaulu, kuanzia A hadi F ya makundi ya alama ambazo watahiniwa wamezipata; hilo likiambatana na mabadiliko yaliyopanua wigo kutoka makundi matano yaliyozoeleka awali (A, B, C, D NA F) hadi kufikia makundi saba ya A, B+, B, C, D, E na F.

Akitoa mfano, Nchimbi alisema kuwa mtahiniwa mwenye alama 42 anaweza kuwamo katika kundi la waliofeli kwa kupata daraja sifuri ikiwa atakosa sifa ya kuwa na walau C moja au D mbili.

Aidha, alieleza mazingira yanayoweza kumfanya mtahiniwa apate daraja la nne licha ya kuwa na jumla ya alama 46 kuwa ni pamoja na kupata C na kisha masomo sita kati ya saba yanayohesabiwa akawa amefeli yote kwa kupata F. 

Hata hivyo, haikufahamika mara moja kama wanafunzi wote waliofanya mtihani huo walishajulishwa juu ya upangaji huo mpya wa madaraja na kufanya mazoezi kupitia mitihani yao ya majaribio maarufu kama 'mock' na pia mitihani ya kawaida ambayo kidato cha nne huifanya wakati wote wanapojipima kwa maandalizi ya mtihani wa taifa.

BUNGE
Licha ya Necta kutoa ufafanuzi huo kuhusu madaraja, NIPASHE inatambua kuwa uamuzi wa baraza hilo umekiuka mapendekezo kadhaa ya wabunge wakati wakijadili kadhia ya matokeo mabaya ya mitihani ya kidato cha nne mwanzoni mwa mwaka 2012.

Katika majadiliano yao, wabunge wengi walipinga mapendekezo kadhaa ya kuwapo kwa madaraja mapya likiwamo la daraja la tano lililotangazwa awali mbele ya waandishi wa habari na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Mchome kabla serikali kumkana bungeni kupitia kauli iliyotolewa na aliyekuwa Naibu Waziri, Philip Mulugo, akisema kuwa hakuna daraja la tano na kwamba, daraja sifuri lililotangazwa kufutwa na Mchome linabaki palepale.

Matokeo yaliyotangazwa mwishoni mwa wiki na Kaimu Katibu wa Necta, Dk. Charles Msonde yalionyesha kuwa kwa ujumla, ufaulu umeongezeka kwa asilimia 15.17 kulinganisha na mwaka 2012, matokeo ambayo baadhi ya wadau wameyakosoa vikali.
 
chanzo ippmedia.com

Jumatatu, 24 Februari 2014

UTATA WA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2013 WAIBUKA.

 Baada ya matokeo ya kidato cha IV mwaka 2013 kutangazwa mwishoni mwa wiki iliyopita , Kumeibuka maswali yanayohitaji majibu ya kina kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi . Wananchi wangependa kufahamu utaratibu uliotumika kupanga madaraja kwani kumeibuka mkanganyiko mkubwa usio na majibu mfano kuna wanafunzi wenye alama 42 wamepewa Division Zero huku wenzao wenye alama 46 wakipewa Division Four. Pia vyombo vya habari vimenukuu Shule ya Mtakatifu Francis kuwa kinara katika mitihani huo ikiwa na Division 1 = 81; Division 2 = 8 , Division 3 =1 , Divison 4= HAKUNA na Division 0= HAKUNA ingawa Shule ya Wavulana ya Marian ina Division 1= 100, Division 2= 10, Division 3= HAKUNA, Division 4= HAKUNA na Division 0= HAKUNA . Pengine kuna mambo mengine ambayo yanaleta mkanganyiko baada ya kupokea matokeo hayo, tutafakari na kuhoji ili kupata ufafanuzi.

chanzo .haki elimu

Alhamisi, 13 Februari 2014

madiwani watafuta mbinu za kutokomeza ziro


MADIWANI wa Halmashauri ya Ushetu, wilayani Kahama, wamehoji  watoto wanaosoma na kumaliza katika shule za sekondari za kata huku wengi wao wakiambulia kupata alama sifuri na kusababisha kubaki vijijini bila mwelekeo wa maisha.
Hoja hiyo ilikuja katika kikao cha baraza lao la madiwani wa halmashauri hiyo baada ya Diwani wa Chona, Mohamed Mwarabu (CHADEMA) kuhoji mpango wa kuwanusuru vijana hao ambao wengi wamejiingiza katika usanii wa nyimbo zisizokuwa na tija.
Mwarabu alisema sifuri kwa wanafunzi hao ni ukosefu wa walimu kwenye shule hizo  na hata wale wenye masomo ya Kilimo, Kiswahili na Kiingereza hawapo, hali inayofanya wanafunzi hao wamalize elimu ya sekondari sawa na wale waliomaliza darasa la saba.
Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, Isabela Chilumba, alidai wanafunzi waliomaliza kidato cha nne na kupata alama sifuri hawako sawa na waliomaliza darasa la saba.
Chilumba alisema faida ya mwanafunzi aliyesoma sekondari ni nyingi, ambazo si kufaulu peke yake na kuwa hata kuanza maisha atakuwa na umri mkubwa kuliko yule wa darasa la saba ambaye huanza kupambana na maisha akiwa na umri mdogo.
Makamu Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Tabu Katoto, aliwataka madiwani hao suala la ukosefu wa walimu lisiwakatishe tamaa ya kusimamia ujenzi wa sekondari nyingine, kwani suala hilo litamalizika, kwa kuwa kila mwaka serikali inaajiri walimu.
Katoto alisema halmashauri yake inatarajia kufungua sekondari tatu katika mwaka huu wa fedha, mwaka 2014/2015 katika kata za Igunda, Nyankende na Sabasabini.

Alhamisi, 6 Februari 2014

serikali inachangia kuua elimu nchini

SERIKALI imekuwa kama haioni maovu yanayofanywa kienyeji na watendaji wake  ndani ya sekta ya elimu.
Na kama inaona basi inaamua kufumbia macho.
Novemba 7, 2012, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Elimu, Majaliwa Kassim, alisema bungeni kuwa ni kosa walimu wakuu kutoza fedha kwa watoto wanaoanza darasa la kwanza, lakini tozo limekithiri.
Majaliwa alionya mwalimu atakayefanya hivyo atachukuliwa hatua kali za kisheria, agizo ambalo serikali yenyewe kupitia watendaji  linaonekana kupigwa mweleka, huku wazazi wakishangaa kuwapo michango isiyoeleweka na mingine ilikubalika kupitia kamati za shule.
Imefika mahali sasa inaonekana wazazi wanafahamu sana umuhimu wa watoto wao kusoma ili baadaye walikwamue taifa  na familia zao, lakini watendaji wa elimu husika wamekuwa mzigo na kikwazo cha watoto hao kupata elimu.
Hivi karibuni mkoani Morogoro, wazazi walifikia kupigana wakigombea watoto waandikishwe ili wasome, lakini mbali ya ugomvi huo, lalamiko na kikwazo kilichotajwa, ni tatizo la tozo na michango kwa wanaoandikisha kufikia sh 50,000 kwa mtoto.
Mbunge wa Morogoro Mjini, Abdulaziz Abood, katika uandikishaji huo, aliingia katika suluba kutoa ufafanuzi ili kuondoa utata baina ya wazazi na waandikishaji, ambapo malipo  ya sh 50,000 kwa mtoto anayeandikishwa, kunaashiria wakuu wa shule kuwa na mradi wa kutumbua fedha kupitia uandikishaji.
Kwa kuwa Kassim alishatolea ufafanuzi, Mwalimu Mkuu au yeyote anayekiuka agizo la michango kuwa atachukuliwa hatua kali, basi kwa hali ilipofikia hadi wazazi wanapigana na wengi wao kukosa kuandikisha watoto wakitumia tozo feki, waadhibiwe.
Ninasema hivyo kwa sababu walimu wakuu wakisaidiana na watendaji wa vijiji na kata, wanaamua kufanya lolote kuhusu elimu bila kupata hata ushauri.
Siku hizi imekuwa si ajabu, walimu wakuu na waratibu wa elimu wakikosa mapato, basi wakilala na kuamka utakuta wanapanga mipango ya kuhakikisha wanapata fedha, mojawapo ikiwa ni kutumia uandikishaji wa wanafunzi kama mradi wa kujipatia fedha.
Bila kufahamu uwezo na kipato cha wananchi wa hali ya chini, wamekuwa wakiwakandamiza na kuwanyanyasa wananchi, na wakati mwingine wanafikia kuwaweka ndani eti kwa sababu ya kushindwa kulipa michango hiyo.
Hapa ndipo ninaposema, aibu ya elimu Tanzania tujifiche wapi? Maana udhaifu wa sekta hii na mipango yake mibovu, haionyeshi mpango mkakati wowote unaowekwa ili kuwe na uwazi wa kuandikisha wanafunzi.
Ni mara nyingi tumeona walimu wakuu na waratibu wa elimu, wamekuwa tatizo kwenye elimu ndani ya vitongoji, vijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa na taifa, ambapo watendaji wamekuwa wakiamua mambo wanavyotaka bila kuwa na vigezo huku wazazi wakiteseka.
Tatizo jingine linalosababisha malumbano sekta ya elimu, ni Kamati za shule ambazo zimekuwa mizigo zikishirikiana na wakuu wa shule, kiasi kwamba wanakaa kupanga mambo wakiangalia uwezo na mishahara waliyonayo bila kutazama kipato cha wananchi.
Ifike mahali hawa nao wasifumbiwe macho maana badala ya kuwa kioo ndani ya elimu, wamekuwa giza kwenye elimu hiyo.
Hawana mbinu na mikakati ya kuwasaidia wazazi wamudu kusomesha watoto, ila mikakati ya tozo lao

chanzo tanzania daima

matatizo yanayomkumba mtoto wa kike kupata elimu bora

Kama kuna mikakati iliyobuniwa kuwasaidia watoto wa kike kupata elimu nchini, ni pamoja na ujenzi wa shule za sekondari za kata.
Pamoja na udhaifu wa shule hizo kama unavyojulikana kwa watu wengi, angalau sasa watoto wengi wa kike wanapata fursa ya kukaa shuleni kwa miaka minne badala ya kuozwa na kuwa mama katika umri mdogo na kuwa mwisho wa elimu yao.
Hata hivyo, mkakati huu pekee haujawa mwarobaini wa changamoto zinazowakabili watoto wa kike katika safari yao ya kuelekea kupata elimu. Bado kuna tatizo kubwa la umasikini uliokithiri na unaokuzwa zaidi na janga la Ukimwi katika jamii ya Kitanzania kiasi kwamba baadhi ya wasichana wanaoingia shule za sekondari hawaendelei muda mrefu.
Hawa wanalazimika kuacha shule ama mwanzoni au katikati kwa kukosa ada ama mahitaji mengine ya shule. Watoto wengi ni yatima na katika maeneo yaliyoathirika kwa kiwango kikubwa na tatizo la Ukimwi hata ndugu na jamaa wamelemewa na mzigo.
Tatizo hili nimeliona Mkoa wa Iringa na sehemu nyingine nchini. Kama utafiti ungefanyika kujua ukubwa wa tatizo hili ingekuwa ni jambo jema. Kwa hiyo, Serikali haina budi kubuni mikakati ya kuwapa fursa wasichana wa kutoka familia maskini na mayatima kumaliza elimu ya sekondari na vyuo vikuu.
Huko nyuma kumekuwepo mifuko ya misaada kama ule wa Shirika la Kimataifa la Misaada la Sweden (SIDA) na mingine, lakini kuna baadhi ya viongozi serikalini walipenyeza watoto wao na waliostahili wakakosa fursa hiyo. Hii ni tofauti na enzi za Mwalimu Julius Nyerere sisi tuliotoka familia maskini tuliweza kusoma hadi chuo kikuu bila matatizo. Cha msingi ni kuwa na sera nzuri inayoelekeza namna ya kuwapa fursa wasichana.
Umbali mrefu
Shule nyingi vijijini ziko mbali na makazi ya watu, hivyo wasichana wanalazimika kutembea masafa marefu kwenda na kurudi shuleni. Umbali huu una athari na hatari zake kwa watoto wa kike. Kwa mfano, wengi huchoka na mwishowe inawaathiri kimasomo.
Vilevile, katika safari hizo ndefu wasichana wengine huchokozwa na wahuni au hata kubakwa. Baadhi ya wazazi na walezi wamepangishia vyumba watoto wao karibu na shule. Suluhu hii imesababisha wasichana kuwekwa kinyumba na wanaume wakware na wasichana wengi wamepata ujauzito.
Tatizo hili la umbali pia huathiri hata walimu wa kike wanaopangwa kufundisha shule zilizo mbali vijijini ambako huduma za jamii kwa mfano usafiri, maji, umeme, nyumba na nyinginezo muhimu ni shida. Vilevile, walimu wa kike wanafanyiwa vitendo vya kihuni ama na walimu wenzao au hata wanajamii wengine vikiwamo vitendo vya kishirikina.
Mila za jamii ya wafugaji
Ingawa wilaya nyingi wasichana wako shuleni (msingi na sekondari) na hasa ukiangalia takwimu kitaifa, lakini wasichana kutoka jamii za wafugaji wengi wako majumbani kutokana na mila na desturi zao. Katika maeneo haya kuna shule chache na watoto hutembea masafa marefu kwenda shule na kurudi nyumbani.
Makabila haya ingawa yana utajiri wa mifugo, lakini ni wagumu kuiuza ili wasomeshe watoto wao hususan wa kike. Kwa sababu hii serikali inahitaji kubuni mkakati maalumu kutatua tatizo la usawa ili watoto wote wa kike kutoka makabila yote wapate elimu.
Katika nchi nyingi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini, ipo sera maarufu Kiingereza kwa jina la ‘Re-entry’.
Sera hii huruhusu wasichana wanaopata mimba wakiwa shuleni kuruhusiwa kuendelea na masomo hadi wanapojifungua na vilevile kuwaruhusu kurudi na kuendelea na masomo baada ya kujifungua.
Sera hii imejadiliwa na kupeleka pendekezo Wizara ya Elimu kwa muda mrefu, lakini haijulikani ni lini itapitishwa na kuwa sera au sehemu ya sheria ya elimu. Wasichana wengi kutoka familia maskini hupata ujauzito na kuacha elimu rasmi baada ya ujauzito.
Wale wanaotoka katika familia tajiri baada ya kujifungua hupelekwa shule binafsi na kuendelea na masomo. Hata hivyo, suala la ujauzito kwa wasichana ni kwa sababu tu ya maumbile yao.
Kama wavulana nao wangeumbwa kuweza kubeba mimba sielewi nani angebaki huko shuleni!
Viongozi wengi ngazi za kufanya uamuzi ni wanaume, hivyo hawaoni kwamba suala hili linahitaji lifanyiwe uamuzi upesi ili kuwanusuru wasichana wengi wanaoathirika badala ya kuwaona au kuwaita ni malaya.
Nipendekeze kwamba, kama suala hili la kuwa na mifuko ya elimu kwa ajili ya wasichana katika ngazi mbalimbali za masomo hususan shule za msingi na sekondari linakuwa zito kitaifa, litolewe mwongozo au sera ili litengewe fedha katika ngazi ya Halmashauri.
Ellen Binagi ni mdau na mwanaharakati wa masuala ya elimu.
Amewahi kufanya kazi katika mashirika na asasi mbalimbli zinazohusiana na elimu.

makala kusoma kuhesabu tatizo kubwa kwa wanafunzi nchini

Tangu mwaka 2010, taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Twaweza kupitia mradi wake wa Uwezo, imekuwa ikifanya tafiti katika nchi za Afrika Mashariki zinazolenga kubaini uwezo wa watoto wa shule za msingi katika stadi za kusoma na kuhesabu.
Majaribio haya, yamekuwa yakihusisha masomo ya Hesabu na lugha za Kiswahili na Kiingereza kwa ngazi ya darasa la pili. Sampuli hujumuisha wanafunzi wa darasa la tatu na darasa la saba.
Sampuli ya washiriki
Takwimu zinaonyesha kuwa, mwaka 2010 watoto walioshirikishwa kwenye utafii huo walikuwa 37,683 mwaka 2011 wanafunzi 114,761 na mwaka 2012 wanafunzi walioshiriki ni 104,568.
Kwa upande wa kaya, mwaka 2010 zilishiriki kaya 18,952 mwaka 2011 zilikuwa kaya 59,992 na mwaka 2012 kaya. 55,191. Kwa wilaya, mwaka 2010 zilishiriki Wilaya 38, mwaka 2011 zilikuwa wilaya 119 na mwaka 2012 wilaya 126.
Shule zilizoshiriki kwenye utafiti uliofanyika mwaka 2010 zilikuwa ni 1,010 mwaka 2011 zilikuwa 3,709 na mwaka jana zikawa 3,624.
Mratibu wa Uwezo upande wa Tanzania, Zaida Mgalla anasema aghlabu majaribio hayo hutayarishwa kwa pamoja na wataalamu wa masomo kutoka vyuo vikuu, Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na walimu wa masomo husika wa darasa la pili.
Matokeo 2010
Utafiti huu ulipofanywa mwaka 2010 ulionyesha kuwa, japo Kiswahili ni lugha inayozungumzwa kwa upana zaidi nchini, idadi kubwa ya watoto hawawezi kusoma kupitia lugha hiyo.
“Kwenye sampuli zetu, chini ya nusu (42.2 asilimia) ya watoto waliofanyiwa uchunguzi waliweza kusoma kwa hatua ya hadithi. Wakati watoto wote katika darasa la tatu wanapaswa kuweza kusoma hadithi ya ngazi ya darasa la pili, watoto chini ya mmoja kati ya watatu (32.7 asilimia) ndio wanaweza.
‘’Hata hivyo, hadi wanamaliza shule ya msingi, mtoto mmoja kati ya 5 hawezi kusoma hadithi ya ngazi ya darasa la pili, licha ya kumaliza miaka saba ya elimu ya msingi,”inasema sehemu ya utafiti huo.
Kwa upande wa Kiingereza, ripoti hiyo ya mwaka 2010 inaonyesha kuwa chini ya mwanafunzi mmoja kati ya 10 (7.7 asilimia) ndio anayeweza kusoma hadhithi ya Kiingereza ya ngazi ya darasa la pili

Wizara sita kufanyiwa tathmini `Matokeo Makubwa Sasa`

Mfumo  wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) unatarajia kufanya tathmini katika wizara sita ili kuona ni kwa kiasi gani umefanya kazi na ripoti itakabidhiwa kwa Rais Jakaya Kikwete na kuwekwa kwenye mitandao.

Mtendaji Mkuu wa mfumo huo chini ya Ofisi ya Rais, Omari Issa, alisema tathmini ya mwaka mmoja itafanyika na taarifa kuwekwa wazi ili kila wizara ijipime na kuona kama imefikia malengo husika.

Alisema pia Februari 24, mwaka huu kutakuwa na mkutano na wafanyabiashara lengo likiwa ni kuwapa uwanja wa kueleza vikwazo vya kufanya biashara vilivyopo nchini kwa sasa ambavyo vinalalamikiwa.

Alisema chini ya mfumo huo ambao unmelenga kutatua matatizo yanayokwamisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ambayo wengi wamesingizia kukosekana kwa fedha jambo ambalo alisema siyo kweli.

“Katika tathmini hiyo watabainisha matatizo ya wizara hadi wizara, mradi hadi mradi, uchambuzi wa kina utaonyesha nani apewe kiasi gani kwa ajili ya kutekeleza lipi…awali wizara ilikuwa inapewa kulingana na bajeti hata kama hawazitumii kwa wakati huo, lakini kwa sasa watapewa kulingana na utekelezaji,” alisema Issa.

Alisema mfumo huo umeweka utaratibu thabiti wa kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa miradi katika maeneo ya kilimo, elimu, maji, nishati, uchukuzi na ufuatiliaji wa rasilimali, lengo likiwa ni kuwa na uwajibikaji wa kila mshiriki au taasisi katika utekelezaji wa miradi ya serikali ili kupata mafanikio haraka.

Kadhalika, Issa alisema mfumo umeanzisha kitengo cha kusimamia utekelezaji na ipo katika mchakato wa kuanzisha vitengo vya kusimamia utekelezaji katika ngazi za mikoa na mamlaka za serikali za mitaa ili kuongeza ufanisi wa kutekeleza miradi katika ngazi zote.

“Ili kufanikisha BRN, tunahitaji ushirikiano wa sekta binafsi ambayo italeta teknolojia, utaalamu wa menejimenti na mtaji, ili kuhamasisha ushirikiano huo tumeanzisha mchakato wa kurazinisha mfumo na taratibu za ubia baina ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) ili tuhakikishe inatoa mchango wake stahili katika utekelezaji wa BRN,” alisema.

Alisema maeneo ya kimkakati ya kitaifa ni usambazaji wa maji salama vijijini ambako kwa kipindi cha miezi sita zaidi ya watu 300,000 wamepata maji, ulinzi wa chakula, elimu ya msingi na sekondari, kuimarisha usafirishaji wa bandari, reli na barabara katika kanda ya kati, upatikanaji na uzalishaji na utafutaji wa rasilimali fedha.