Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatatu, 27 Januari 2014

walimu wastaafu wa sayansi kupewa ajira tena

naibu waziri wa elimu philipo mulugo
Serikali imetangaza neema kwa walimu wastaafu wa somo la sayansi kujitokeza na kupeleka majina yao Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ili waweze kupatiwa nafasi za kufundisha, kuziba pengo la ukosefu wa walimu hao nchini.

Hatua hiyo imechukuliwa ili kupunguza tatizo la upungufu wa walimu 26,000 uliopo hivi sasa hali inayoathiri zaidi wanafunzi wanaochukuwa masomo ya sayansi.

Hayo yalisemwa jijini Arusha na aliyekuwa Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo siku moja kabla ya kuvuliwa wadhifa huo, wakati akizungumza katika mahafali ya tano ya chuo cha ufundi Arusha (ATC) ambapo jumla ya wanafunzo 256 walitunukiwa vyeti vya astashahada, stashahada na shahada ya kozi mbalimbali.

Alisema endapo walimu hao wastaafu hawatajitokeza, serikali itaingia hasara kubwa kutokana na kuajiri walimu wa fani hiyo kutoka nje ya nchi. Mulugo alisema serikali itawaombea kibali wizarani walimu wastaafu wa masomo ya sayansi watakaojitokeza  ili waweze kufundisha katika shule mbalimbali kwa kipindi cha miaka miwili na watakaopenda kuendelea hata kwa miaka 10 watakubaliwa.

“Tumekuwa tukitangaza sana kujitokeza kwa walimu wastaafu wa masomo ya sayansi nchi nzima kuleta majina yao wizarani ili waweze kupata ajira kwani tuna upungufu mkubwa sana, na tangu tutoe matangazo hayo wamejitokeza walimu wastaafu 96 tu, na hao hawatoshi bado tunawakaribisha sana popote pale walipo,” alisisitiza Mulugo.
 
Chanzo ippmedia.com