Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatano, 22 Januari 2014

mabadiliko baraza la mawaziri kila mmoja na mtizamo wake

Hatimaye Baraza jipya la Mawaziri limetangazwa , tumeshuhudia mabadiliko katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambapo Naibu Waziri wa Elimu wa sasa ni Mh. Jenista Mhagama amechukua nafasi ya Mh. Philipo Mulugo. Wako watanzania wanayaona mabadiliko haya kutokuwa na tija huku wengine wakiamini mabadiliko yanaweza kutokea, wote wana sababu za msingi kabisa kuamini kile wanachoamini. Je mdau wa elimu ni mambo yapi Uongozi wa sasa unatakiwa kuyazingatia/kuyafanya ili kuhakikisha kiwango cha elimu nchini kinapanda na wanafunzi kote nchini wanapata elimu bora? Tafakari na tushikirikishane
 
chanzo haki elimu facebook page

Habari TATU KALI zinazohusu masuala ya Elimu nchini Tanzania zinazopamba katika vyombo vya habari tarehe 22 January 2014



1. Wanafunzi 11,000 katika mkoa wa DSM wamekosa nafasi za kujiunga na kidato cha kwanza licha ya kufaulu mtihani wa darasa la saba mwaka jana. (Chanzo: Habari Leo)

2. Mkuu wa Wilaya ya Nzega ameagiza wanafunzi wote wa shule za msingi na sekondari wilayani humo waliokatishwa masomo yao kwa sababu mbalimbali ikiwemo mimba, utoro n.k (Chanzo:Tanzania Daima)

3. VETA yaanzisha maabara za LUGHA katika vyuo vyake ili kuwezesha ufundishaji wa lugha za kigeni kwa ubora zaidi na kuondoa tatizo la watanzania kushindwa kujieleza kwa lugha za kigeni. ( Chanzo: The Guardian)
 
chanzo haki elimu page