Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumanne, 16 Aprili 2013

Boresha chekechea ni jukumu la kila mmoja wetu

wanafunzi wakiwa wamekaa chini

Suala la elimu ya awali ni suala nyeti linalotakiwa kutazamwa kwa macho mawili na jamii nzima Serikali na kila mdau wa elimu elimu. Elimu ya awali (chekechea) umsababisha mwanafunzi kuanza darasa la kwanza akiwa anazijua stadi za awali.
Mwanafunzi hawezi kuwa mzigo tena kwa mwalimu wa darasa la kwanza ikiwa atapitia elimu ya awali ( chekechea)
ni jukumu letu sote kuhakikisha elimu ya chekechea inakuwa bora  kwa watoto wote kwa kuwapatia mahitaji muhimu kama uji, madawati, walimu bora pamoja na miundo mbinu rafiki ya kuwafanya wapende mazingira ya shule.

Kwa pamoja tuinue sauti za wanyonge