Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatano, 13 Agosti 2014

Iringa shule yenye wanafunzi 600 ina mwalimu mmoja

Photo: TAFAKARI YA WIKI HII : Gazeti la RaiaTanzania limeripoti habari inayohusu shule ya msingi katika mkoa wa Iringa yenye wanafunzi 600  ikiwa na mwalimu mmoja tu (1), wakati huo huo Radio Uhuru imeripoti Shule moja mkoani Shinyanga yenye wanafunzi takribani 500 wana matundu mawili (2) pekee ya vyoo .Gazeti la Mtanzania pia limeripoti shule yenye wanafunzi 480 katika wilaya ya Serengeti ina madawati matano  tu (5).Muasisi wa Taifa letu , Mwalimu Nyerere alituasa ili nchi iendelee tunahitaji mambo manne SIASA SAFI, ARDHI, UONGOZI BORA NA WATU . Hakuna ubishi kwamba bado hatuna uongozi bora kwani imepita miaka 50 tangu Uhuru kukiwa na awamu nne za uongozi lakini changamoto kama hizi si ngeni miongoni mwa watanzania, Siasa yetu nayo bado ina madhaifu hilo halina ubishi. Leo tuachane na UONGOZI MBOVU NA SIASA MBOVU kabisa, tujiangalie SISI (WATANZANIA) kama wananchi  tujiulize tumefanya nini kuhakikisha tunaondokana na changamoto hizi? Je ni kwa kiwango kipi tumefanikiwa katika yale tuliyofanya katika kuleta mabadiliko ? Nini wajibu wetu watanzania katika kutatua changamoto hizi?. Hii ni aibu kwetu sote, kwangu mimi, yule na wewe. Tafakari na tujadili hatua zipi zichukuliwe kuhakikisha changamoto hizi zinatatuliwa.TAFAKARI YA WIKI HII : Gazeti la RaiaTanzania limeripoti habari inayohusu shule ya msingi katika mkoa wa Iringa yenye wanafunzi 600 ikiwa na mwalimu mmoja tu (1), wakati huo huo Radio Uhuru imeripoti Shule moja mkoani Shinyanga yenye wanafunzi takribani 500 wana matundu mawili (2) pekee ya vyoo .Gazeti la Mtanzania pia limeripoti shule yenye wanafunzi 480 katika wilaya ya Serengeti ina madawati matano tu (5).Muasisi wa Taifa letu , Mwalimu Nyerere alituasa ili nchi iendelee tunahitaji mambo manne SIASA SAFI, ARDHI, UONGOZI BORA NA WATU . Hakuna ubishi kwamba bado hatuna uongozi bora kwani imepita miaka 50 tangu Uhuru kukiwa na awamu nne za uongozi lakini changamoto kama hizi si ngeni miongoni mwa watanzania, Siasa yetu nayo bado ina madhaifu hilo halina ubishi. Leo tuachane na UONGOZI MBOVU NA SIASA MBOVU kabisa, tujiangalie SISI (WATANZANIA) kama wananchi tujiulize tumefanya nini kuhakikisha tunaondokana na changamoto hizi? Je ni kwa kiwango kipi tumefanikiwa katika yale tuliyofanya katika kuleta mabadiliko ? Nini wajibu wetu watanzania katika kutatua changamoto hizi?. Hii ni aibu kwetu sote, kwangu mimi, yule na wewe. Tafakari na tujadili hatua zipi zichukuliwe kuhakikisha changamoto hizi zinatatuliwa.
 
 souce Haki Elimu