Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumapili, 6 Julai 2014

umuhimu wa Kiswahili kama Lugha ya kufundishia elimu ya sekondari


Lugha ya kufundishia Sekondari ni Kiingereza. Wadau wengi wanasema hii ni sababu moja ya vijana kutoelewa/kufeli. Tufundishe kwa Kiswahili? Sote tunatambua kwamba Elimu ndio nguzo muhimu kwa maendeleo na katika kurekebisha Elimu yetu suala la lugha ni muhimu. Tutafakari pia msingi wa elimu ni nini hasa? Msingi wa elimu ni kupata maarifa na kuyatumia kujiendeleza na kujenga jamii. Sababu ya elimu ni kupata maendeleo. Elimu sio kwa ajili ya ajira tu. Shabaha ya elimu pia ni kujenga udadisi na ubunifu katika kutafuta majawabu ya changamoto ndani ya jamii. Je maarifa hayawezi kupenyezwa kwa Kiswahili? Tukisema Kiswahili hakijitoshelezi maana yake tunakatia tamaa uwezekano wa kukipanua? Katika nchi ndogo lakini zilizoendelea - Sweden, Norway, Denmark, Finland - lugha zilizotumika kuvumbua mambo ni zao. Hii haiwezekani hapa kwetu? Je ni kweli watu hufikiria kwa lugha yake ya asili? Ukimlazimisha mtu afikirie, abaini na avumbue kwa lugha isiyo yake ataweza au ataiga tu? Lugha sio kwa ajili ya mawasiliano tu na walimwengu wengine. Lugha pia ni kwa ajili ya kujenga fikra na kujitambua. Elimu haina majibu ya shida zote za jamii. Na elimu ya kukaririsha majibu haifai. Elimu inapaswa kujenga uwezo na maarifa ya kutafuta MAJAWABU.

na january makamba