Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Ijumaa, 12 Septemba 2014

diwani kata ya kigera ahukumiwa kifungo miaka 3 kwa kosa la kubomoa madarasa

madarasa yaliyobomolewa na kuwaacha wanafunzi bila kuwa na pahala pa kusomea
diwani wa kata ya kigera mheshimiwa Gabriel Ocharo Aenda  amehukumiwa kifungo cha cha nje miaka mitatu na kulipa fidia ya milioni tano kwa kosa la kubomoa madarasa matatu yenye vyumba 6 vya madarasa katika shule ya msingi Kigera

Diwani huyo amekubwa na dhoruba hiyo baada ya kugundulika kubomoa madarasa hayo pasipo kufuata utaratibu. hivi karibuni ililipotiwa na kituo cha habari cha BBC katika kipindi cha haba na haba kuwa wanafunzi wa madarasa ya awali wa shule hiyo wamekuwa wakisomea katika moja ya jengo la ofisi kutokana na upungufu wa madarasa.
lakini suala hilo limechukua sura ya kisiasa zaidi baada ya MNEC Vedastus Manyinyi Mathayo kutoa ahadi hewa katika moja ya mikutano yake ya kisiasa kuwa atatoa mabati 100 kwa ajili ya ukarabati wa jengo hilo ambapo mpaka leo hajapeleka hata bati moja
hivi karibuni Mbunge wa Musoma Mjini  Vincent Nyerere na Meya Alex Kisurula katika mikutano yao ya kuelezea mafanikio na changamoto wameahidi wananchi wa kata ya Kigera kuwa madarasa hayo yatakarabatiwa kabla ya mwezi disemba mwaka huu.

wito wetu marafiki wa elimu musoma kwa viongozi :  ELIMU NI TAALUMA ISIYOHITAJI SIASA VIONGOZI WASILETE MCHEZO NA ELIMU YA WATOTO WA MASKINI.