Kutoka kijiji cha Bisumwa wilaya mpya ya Butiama wazazi wamegomea uongozi wa shule yao pamoja na kamati juu ya suala la kuchangia chakula kwa wanafunzi shuleni kama agizo la serikali linavyosema wanafunzi wanapaswa kula shuleni ili kuongeza ari ya kujifunza na kupunguza utoro.
shule iliwaomba wazazi hao kichangia kiasi cha debe moja la mahindi na maharage kilo4 kila mwezi kwa ajili ya chakula cha wanafunzi awali katikabkikao hicho cha kamati ya shule na wazazi kamati iliwaambia wazazi kuwa kila mzazi atatakiwa kuchangia mchango huo kwa kila mtoto iwapo mzazi una watoto 4 basi utatakiwa kuchangia mahindi debe 4 na maharage kilo 16
baada ya wananchi kusikiliza maelezo hayo toka kwa uongozi wa shule walitoa kauli ya pamoja kwamba hawako tayari kuchangia kiasi hicho kutokana na hali ya maisha ya sasa na pia hawako tayari kuchangia hata debe moja kwa watoto 4 hivyo shule iendelee na utaratibu wa kutawanyisha watoto mapema ili waende majumbani mwao kula kisha warudi shule kama ilivyokuwa ikifanyika awali
suala la wazazi kuchangia chakula kwa ajili ya wanafunzi limeonekana kuwa tatizo sana hasa katika mikoa ya kanda ya ziwa na huenda likashindikana kabisa serikali inapaswa kuangalia njia mbadala ya kutekeleza mpango huu
harakati za marafiki wa elimu musoma wasiliana nasi kwa namba +255755 650 075 au +255786 650 075 ni jukumu letu kuboresha elimu
HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania
Jumamosi, 28 Machi 2015
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)