Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumamosi, 13 Desemba 2014

serikali za mitaa muongozo sahihi wa serikali kuu fanya maamuzi sahihi

huu ni wakati sahihi wa kufanya maamuzi sahihi kwa miaka mitano ijayo ili iwe sahihi kwa jamii yako kura yako haki yako maendeleo yako marafiki wa elimu musoma tunawatakia watanzania wote uchaguzi mwema wa serikali za mitaa

Alhamisi, 13 Novemba 2014

habari picha marafiki wa elimu wakihamasisha jamii juu ya ujenzi wa maktaba

bi.perus akigawa machapisho kwa wanafunzi

bi pesus akigawa machapisho



wananchi wakimsikiliza rafiki wa elimu bi. perus

wananchi wakimsikiliza bi. perus akihamasisha ujenzi wa maktaba


mmoja wa wananchi ambae ni mwalimu akitoa maoni


wananchi wakimsikiliza Juma richard aonekani pichani
picha mbalimbali zikiwaonyesha marafiki wa elimu wakihamasisha jamii katika uchangiaji wa maktaba ya jamii anae onekana pichani ni rafiki wa elimu Bi. perus masokomya akihamasisha jamii juu ya ujenzi wa maktaba ya jamii wananchi pia wameonyesha nia ya kuchangia na wako tayari kwa ajili ya ujenzi huo

picha matukio na Juma richard

Alhamisi, 18 Septemba 2014

mwanafunzi ajinyonga na kuacha ujumbe unaowalaumu madaktari

Mwanafunzi, Ezra Gerald Wabamba, aliyekuwa anasoma kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Ihungo, mkoani Kagera, amekatisha maisha yake kwa kujinyonga akiwa hospitalini na kuacha ujumbe mzito juu ya chanzo cha kifo chake.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Gilles Muroto, mwanafunzi huyo alifikishwa hosptalini hapo Septemba 11, mwaka huu na kulazwa ili kupatiwa matibabu.

Alisema Ezra alijinyonga saa 1:30 asubuhi katika mti ulikuwa umbali wa hatua 73 kutoka kwenye wodi ya wagonjwa namba tatu aliyokuwa amelazwa, kwa kutumia shuka yake binafsi.

Alisema baada ya maiti yake kugundulika na kufanyiwa upekuzi kwenye mifuko yake ya nguo kulikutwa Sh. 3,900, funguo mbili za Solex na kipande cha karatasi chenye ujumbe.

Alisema ujumbe huo ulisomeka: “Haiwezekani binadamu kuhudumiwa kama mbwa, yaani nafika hospitali naeleza hali yangu halafu daktari ananiandikia kulazwa bila ya kupimwa, sasa sijui watatibu  nini?, kwa kweli siwezi kuvumilia yaani wenzangu wanasoma halafu mimi nimekalishwa tu hapa hospitalini bila ya kujua wananitibu nini, inaniuma sana  mpaka kufika hatua hii ya kujiondoa duniani, ni kwasababu ninaona wanachezea ndoto zangu, mimi siwezi kuona ndoto yangu inazimwa wakati ninatakiwa niwepo shuleni nikamilishe ndoto zangu, mjitahidi tukutane mbinguni.”

Mwanafunzi huyo alimalizia ujumbe huo kwa maeneo ya kiingereza yaliyosomeka: “ Respect my family and brother Henry.”

Kamanda Muroto alisema katika tukio hilo hakuna aliyekamatwa ila uchunguzi juu ya kifo cha mwanafunzi huyo aliyekuwa akisoma masomo ya mchepuo wa kemia, bailojia na jiografia (CBG) unaendelea, ili utaratibu wa kuukabidhi mwili wa marehemu kwa familia yake yenye makazi yake mkoani Tabora ufanyike.

Juhudi za kumpata Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa Kagera, Dk. Thomas Rutachunzibwa, ili kupata ufafanuzi wa kifo hicho chenye mazingira tata hazikufanikiwa kutokana na kuwa nje kiofisi, ingawa Katibu wa hostali hiyo, Justus Benges, alithibitisha tukio hilo kutokea hospitalini hapo.

Alisema mwanafunzi huyo alikuwa akiendelea na huduma ya matibabu kutokana na kugundulika na ugonjwa wa malaria kali.

Mazingira ya kifo cha mwanafunzi huyo yameleta sintofahamu katika jamii ya wakazi wa mji wa Bukoba, huku baadhi  wakihusisha kuwapo huduma mbovu inayotolewa na hositali hiyo pamoja na lugha zisizorafiki kwa wagonjwa.

Imebainika kuwa marehemu tangu alazwe hospitalini hapo, alikuwa akihudumiwa kwa kupelekewa chakula na wanafunzi marafiki zake ambao walikuwa wakitoka shuleni.

chanzo Ippmedia.com

Ijumaa, 12 Septemba 2014

diwani kata ya kigera ahukumiwa kifungo miaka 3 kwa kosa la kubomoa madarasa

madarasa yaliyobomolewa na kuwaacha wanafunzi bila kuwa na pahala pa kusomea
diwani wa kata ya kigera mheshimiwa Gabriel Ocharo Aenda  amehukumiwa kifungo cha cha nje miaka mitatu na kulipa fidia ya milioni tano kwa kosa la kubomoa madarasa matatu yenye vyumba 6 vya madarasa katika shule ya msingi Kigera

Diwani huyo amekubwa na dhoruba hiyo baada ya kugundulika kubomoa madarasa hayo pasipo kufuata utaratibu. hivi karibuni ililipotiwa na kituo cha habari cha BBC katika kipindi cha haba na haba kuwa wanafunzi wa madarasa ya awali wa shule hiyo wamekuwa wakisomea katika moja ya jengo la ofisi kutokana na upungufu wa madarasa.
lakini suala hilo limechukua sura ya kisiasa zaidi baada ya MNEC Vedastus Manyinyi Mathayo kutoa ahadi hewa katika moja ya mikutano yake ya kisiasa kuwa atatoa mabati 100 kwa ajili ya ukarabati wa jengo hilo ambapo mpaka leo hajapeleka hata bati moja
hivi karibuni Mbunge wa Musoma Mjini  Vincent Nyerere na Meya Alex Kisurula katika mikutano yao ya kuelezea mafanikio na changamoto wameahidi wananchi wa kata ya Kigera kuwa madarasa hayo yatakarabatiwa kabla ya mwezi disemba mwaka huu.

wito wetu marafiki wa elimu musoma kwa viongozi :  ELIMU NI TAALUMA ISIYOHITAJI SIASA VIONGOZI WASILETE MCHEZO NA ELIMU YA WATOTO WA MASKINI.

Jumatano, 10 Septemba 2014

kila la heri wanafunzi wa darasa la 7 kwa mitihani yenu ya kumaliza elimu ya msingi

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Jenista Mhagama
Jumla ya watahiniwa 808,111 wanatarajia kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi leo, huku kati ya hao wavulana ni 378,470 sawa na asilimia 46.84 na wasichana ni 429,641  (asilimia 53.16).

Aidha, katika mtihani huo, watahiniwa 783,223 watafanya mtihani kwa lugha ya Kiswahili, watahiniwa 24,888 watafanya mtihami kwa lugha ya Kiingereza.

Kwa upande wa wasioona walioandikishwa kufanya mtihani ni 86 , wavulana 54 na wasichana 32, na watahiniwa wenye uoni hafifu wanaotarajiwa kufanya mtihani huo ni 714, kati yao  wavulana ni 371 na wasichana 343.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Jenista Mhagama, alisema maandalizi yote kwa ajili ya mtihani yameshakamilika ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa karatasi za mitihani, fomu maalum za OMR za kujibia mitihani pamoja na nyaraka zote muhimu zinazohusu mtihani huo.

Mhagama alisema mtihani mtihani huo ni muhimu kwa taifa, wazazi na jamii kwa ujumla na kwamba masomo yatakayotahiniwa ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na Maarifa ya Jamii  mtihani ambao utafanyika kwa siku mbili mfululizo.

Alitoa wito kwa kamati za mitihani za mikoa na wilaya kuhakikisha taratibu zote za mitihani zinazingatiwa ipasavyo na kuwataka wasimamizi, walimu, wananchi na wanafunzi  kutoshiriki katika vitendo vya udanganyifu na kwamba atakayebainika atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Alhamisi, 4 Septemba 2014

Shule nyingi za msingi nchini zakabiliwa upungufu madawati

baadhi ya wanafunzi shule ya msingi mwisenge wakiwa wamekaa sakafuni
Shule nyingi za msingi zinakabiliwa na upungufu mkubwa wa madawati, hali inayotishia maendeleo ya elimu nchini.

Wakizungumza kwa njia ya simu kwa nyakati tofauti na kipindi cha Kumepambazuka kinachorushwa na Radio One Stereo, wakuu wa mikoa ya Iringa, Dodoma, Morogoro na Tanga, walithibitisha kuwapo kwa tatizo hilo katika mikoa yao.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma, alisema kwa njia ya simu kuwa licha ya mkoa wake kuwa unazalisha miti mingi ya mbao na uwapo wa shamba la miti la Taifa (Sao Hill), upungufu wa madawati upo, ingawa si mkubwa ukilinganisha na mikoa mingine.

Alisema tayari serikali ya mkoa wake imeshaanza kujipanga mapema kulikabili tatizo hilo hata kabla ya tamko la Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, huku mkoa huo ukijiwekea mikakati ya kuhakikisha unatekeleza agizo hilo mapema mwishoni mwa Desemba, mwaka huu.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Rehema Nchimbi, alisema mkoa wake una upungufu wa madawati kwa asilimia zaidi ya 40 kutokana na kutokuwa na vyanzo vizuri vya miti ya mbao suala, ambalo limekuwa ni changamoto kubwa.

Alisema ili kufikia malengo, wameanza na kuimarisha mfuko wa elimu na kwamba, wameweka utaratibu wa wilaya kuchangia Sh. 10,000 na nyingine kuchangia Sh. 5,000, kupitia mifugo ya kuku wanaopatikana kwa wingi katika mkoa huo.

Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, alikiri mkoa wake kukabiliwa na uhaba mkubwa wa madawati, hasa katika shule za msingi na kwamba, kwa tathmini waliyoifanya ni upungufu wa kiasi cha madawati 91,000 kwa wilaya zote mkoani humo.

Tatizo la uhaba wa madawati limekuwa ni changamoto kubwa nchini kiasi cha kumfanya Pinda kutoa tamko la kuwataka wakuu wote wa mikoa kuhakikisha kila mmoja anamaliza tatizo hilo ifikapo Juni 30, 2015.

chanzo ippmedia,
picha. marafiki wa elimu musoma

Jumapili, 31 Agosti 2014

Timu ya Haki Elimu uso kwa uso na afisa elimu (shule ya mwisenge)

afisa elimu bi. Beatrice Mkina akiteta kidogo na wafanyakazi wa Haki Elimu walipokutana shule ya msingi Mwisenge
maktaba ya kisasa iliyojengwa na Haki Elimu shule ya msingi Mwisenge

wanafunzi wasioona shule ya Mwisenge kujengewa kiwanja cha michezo


Afisa elimu Msingi manispaa ya Musoma Mjini Bi
. Beatrice Mkina alibainisha mpango wake wa kuwezesha shule ya msingi Mwisenge kujengewa kiwanja cha michezo kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavua wa macho.
siku ya ijumaa 29/8/2014 afisa elimu huyo aliitembelea shule ya msingi Mwisenge kwa minajili ya walimu wa shule hiyo kumpendekezea eneo zuri la ujenzi wa kiwanja hicho cha michezo
afisa elimu akiangalia eneo lililopendekezwa kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja cha michezo
afisa elimu katikati na baadhi ya walimu na wajumbe wa kamati ya shule
hii ni juhudi nzuri kwa serikali kuwakumbuka wanafunzi wasioona wa shule ya msingi mwisenge.
Afisa elimu kushoto na mjumbe wa kamati ya shule mwisenge

Alhamisi, 28 Agosti 2014

umoja wa marafiki wa elimu musoma (sauti zetu club) tumetimiza miaka 6

Marafiki wa elimu musoma
umoja wa marafiki wa elimu musoma tunaounda kikundi cha SAUTI ZETU CLUB leo tumetimiza miaka sita tangu kuanzisha umoja wetu mwaka 2008 tunamshukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania na kuzidi kutuaminisha kwa jamii na viongozi pamoja na wadau wa elimu Musoma Mijini

Kwa pamoja tunaweza kuinua sauti za wanyonge

Jumatatu, 25 Agosti 2014

Hatimae shule ya kigera mbunge nyerere asema itajengwa kabla ya disemba mwaka huu

majengo ya shule ya kigera yaliyobomolewa na diwani bila kufuata utaratibu
hatimae Mbunge wa musoma mjini Mheshimiwa Vincent Nyerere katoa ahadi jana kwenye mkutano wa kuelezea mafanikio aliyofikia kwa miaka minne kuwa,
shule ya msingi Kigera iliyobomolewa na diwani wa kata hiyo ndugu Gabriel Ocharo Aenda kwa kile kilichogundulika kuwa ni kutokufuata utaratibu na kupelekea wanafunzi kukosa pahala pa kusomea ,

mbunge wa musoma mjini jana kamsimamisha Meya wa manispaa ndugu Alex Kisurura kujibu sakata la shule hiyo na kueleza kwamba ifikapo mwezi disemba shule hiyo iliyobomolewa vyumba sita vya madarasa na kupelekea wanafunzi kurundikana madarasani vitakuwa vimekarabatiwa tena kwa kiwango cha juu na kuahidi kuwa licha ya ukarabati pia watapeleka madawati mapya katika madarasa hayo.

sakata la kubomolewa madarasa hayo sita  mpaka sasa bado linaendelea mahakamani baada ya diwani huyo kufunguliwa kesi kwa kosa hilo la kobomoa madarasa hayo.

akizidi kuelezea waliyoyafanya kwa miaka minne ya uongozi wake mhe Nyerere kasema wamegawa computer 5 na projector kwa shule 3 wametengeneza madawati 1902  pamoja na mipango mingine mingi sana ikiwa ni pamoja na kujenga maabara ya kisasa shule ya sekondary bweri makatani na kujenga madarasa karibu kila shule ya sekondary

Alhamisi, 21 Agosti 2014

Wanafunzi 28,000 elimu ya juu kukosa mikopo

Wanafunzi 28,037 watakosa mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HELSB), hivyo kulazimika kusaka njia mbadala kama wanataka kuendelea na masomo ya elimu ya juu.

Idadi hiyo ni sehemu ya wanafunzi 58,037 ambao hadi kufikia Julai 31, mwaka huu walikuwa wamewasilisha maombi ya mikopo kwa ajili ya mwaka wa masomo 2014/15, huku bodi hiyo ikiwa na uwezo wa kutoa mikopo kwa wanafunzi 30,000 pekee wa mwaka wa kwanza.

Idadi hiyo inafanya asilimia 49 ya waombaji wote kusaka vyanzo mbadala kama wanataka kuendelea na elimu ya juu nchini kwa mwaka ujao. HELSB imesema kuwa ina uwezo wa kutoa mikopo kwa asilimia 51.5 pekee.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salama jana, Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa HESLB, Cosmas Mwaisoba, alisema maombi yaliyopokelewa mwaka huu yameongezeka kutoka 53,239 mwaka jana hadi 58,037 sawa na ongezeko la asilimia tisa.

Alisema miongoni mwa waombaji wa mikopo, kundi la diploma ya ualimu wa sayansi ni 480 wakati wale wa shahada ya uzamili/uzamivu kwa vyuo vya ndani ya nchi wakiwa ni 276.

Kwa mujibu wa Mwaisoba, waombaji wa shahada kwanza kwa vyuo vya ndani ya nchi ni 56,922, wale wa shahada ya uzamili/uzamivu nje ya nchi wakiwa ni 126 na wale wa shahada ya kwanza nje ya nchi ni 233.

Alisema baada ya kufungwa rasmi kwa kipindi cha kupokea maombi ya mikopo, hatua inayoendelea kwa sasa ni uhakiki wa taarifa za waombaji kwa kuzipitia nyaraka mbalimbali zilizoambatanishwa na waombaji mikopo.

Nyaraka hizo ni cheti cha kuzaliwa, vyeti vya taaluma, vielelezo vya mdhamini, saini ya mwombaji na mdhamini wake na ushuhuda wa mwanasheria au hakimu kwamba vivuli vya nyaraka zilizowasilishwa kwenye bodi ni halisi.

Alisema mchakato wa uchambuzi na upangaji wa mikopo utakamilika baada ya majina ya wanafunzi waliodahiliwa na Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) kujiunga na vyuo mbalimbali yanapowasilishwa rasmi kwenye bodi.

Kwa mujibu wa Mwaisoba, udahili wa wanafunzi unafanywa na TCU kwa mfumo wa pamoja wa udahili (CAS) unaotumiwa na vyuo takriban vyote vya elimu ya juu nchini. Alisema kwa vyuo ambavyo havimo katika mfumo wa pamoja wa CAS hutuma TCU majina ya wanafunzi, ambao vimewadahili ili wathibitishwe kabla ya kupatiwa mikopo.

“Taarifa za udahili ni muhimu katika zoezi la upangaji wa mikopo kwa kuwa zinatoa mwongozo wa gharama halisi za program za mafunzo,” alisema Mwaisoba.

Alisema wanafunzi wanaostahili na waliotimiza masharti na vigezo vya ukopeshaji ndiyo hupangiwa mikopo kulingana na bajeti iliyotengwa na serikali.

Mwaisoba alisema majina ya wanafunzi waliopata mikopo kulingana na udahili, yatatangazwa kwenye tovuti ya bodi na katika vyombo vya habari ili kuwataarifu wadau wote ikiwa ni pamoja na wanafunzi, vyuo vya elimu ya juu, wazazi na umma kwa jumla.

Alisema nakala za majina ya wanafunzi waliopangiwa mikopo zitatumwa kwenye vyuo husika.

Mwaisoba, alisema kwa kutambua umuhimu wa masomo ya sayansi na kukabiliana na upungufu wa walimu wa masomo hayo katika ngazi ya shule za msingi na sekondari, mwaka huu serikali imetoa fursa ya mikopo kwa wanafunzi watakaojiunga na masomo ya stashahada maalumu ya ualimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati.

Alisema wanafunzi 5,000 wanatarajiwa kujiunga na stashahada hiyo maalumu katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) na kwamba, wote watanufaika na mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

“Kwa taarifa hii, bodi inapenda kuwataarifu wadau wote kuwa mchakato wa utoaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2014/2015 unaendelea,” alisema Mwaisoba.

Aliwataka waombaji wa mikopo, wazazi/walezi na umma kwa jumla kutambua kuwa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu ni sehemu ya utekelezaji wa sera ya uchangiaji wa elimu ya juu na hivyo iwapo kuna waombaji wanaoweza kujigharimia, wasiombe mikopo ili kutoa nafasi kwa wahitaji wengi zaidi.

Alisema miongoni mwa changamoto zinazoikabili HESLB ni pamoja na ucheleweshaji wa urejeshaji wa mikopo, ushirikiano hafifu kutoka kwa wadau katika urejeshaji wa mikopo na mazingira ya kijiografia kuweza kuwafuatilia waliokopa.

Hata hivyo, alisema HESLB ina uwezo wa kukusanya marejesho ya mikopo Sh. bilioni tatu kwa mwezi.

KUMALIZANA NA TAHLISO WIKI IJAYO
Kuhusu madai ya wanafunzi wa vyuo vitano ya kutaka wapewe Sh. bilioni 6.6 kwa ajili ya mafunzo ya vitendo, Mwaisoba alisema malipo hayo yanaandaliwa na kwamba, hundi za malipo hayo zinatarajiwa kupelekwa katika vyuo wiki ijayo.

Alisema wanafunzi wa vyuo hivyo walichelewa kulipwa kutokana na fedha kuchelewa kupatikana.Hali hiyo ilisababisha Jumuiya ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu nchini (Tahliso) kuitisha maandamano ya amani wiki iliyopita kwenda ofisi za Waziri Mkuu kushinikiza serikali kuwalipa fedha hizo.

Hata hivyo, maandamano hayo yalisambaratishwa na Jeshi la Polisi, lakini siku mbili baadaye, Tahliso ilitangaza tena kuitisha maandamano keshokutwa.

Kiwango hicho cha fedha kinachodaiwa na wanafunzi hao, kimo kwenye takwimu zilitolewa na Mkurugenzi wa HESLB wakati wakifanya mazungumzo juu ya hatma ya vyuo hivyo.

Vyuo hivyo, ambavyo havijapata  fedha hizo ni Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino (Saut) Mwanza na Tabora, Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji-Mbeya, Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira, Chuo Kikuu Kishiriki cha Kumbukumbu ya Stefano Moshi (SMUCCO) na Chuo Kikuu cha Jordan Morogoro.    

CHANZO IPPMEDIA.COM

Jumatano, 13 Agosti 2014

Iringa shule yenye wanafunzi 600 ina mwalimu mmoja

Photo: TAFAKARI YA WIKI HII : Gazeti la RaiaTanzania limeripoti habari inayohusu shule ya msingi katika mkoa wa Iringa yenye wanafunzi 600  ikiwa na mwalimu mmoja tu (1), wakati huo huo Radio Uhuru imeripoti Shule moja mkoani Shinyanga yenye wanafunzi takribani 500 wana matundu mawili (2) pekee ya vyoo .Gazeti la Mtanzania pia limeripoti shule yenye wanafunzi 480 katika wilaya ya Serengeti ina madawati matano  tu (5).Muasisi wa Taifa letu , Mwalimu Nyerere alituasa ili nchi iendelee tunahitaji mambo manne SIASA SAFI, ARDHI, UONGOZI BORA NA WATU . Hakuna ubishi kwamba bado hatuna uongozi bora kwani imepita miaka 50 tangu Uhuru kukiwa na awamu nne za uongozi lakini changamoto kama hizi si ngeni miongoni mwa watanzania, Siasa yetu nayo bado ina madhaifu hilo halina ubishi. Leo tuachane na UONGOZI MBOVU NA SIASA MBOVU kabisa, tujiangalie SISI (WATANZANIA) kama wananchi  tujiulize tumefanya nini kuhakikisha tunaondokana na changamoto hizi? Je ni kwa kiwango kipi tumefanikiwa katika yale tuliyofanya katika kuleta mabadiliko ? Nini wajibu wetu watanzania katika kutatua changamoto hizi?. Hii ni aibu kwetu sote, kwangu mimi, yule na wewe. Tafakari na tujadili hatua zipi zichukuliwe kuhakikisha changamoto hizi zinatatuliwa.TAFAKARI YA WIKI HII : Gazeti la RaiaTanzania limeripoti habari inayohusu shule ya msingi katika mkoa wa Iringa yenye wanafunzi 600 ikiwa na mwalimu mmoja tu (1), wakati huo huo Radio Uhuru imeripoti Shule moja mkoani Shinyanga yenye wanafunzi takribani 500 wana matundu mawili (2) pekee ya vyoo .Gazeti la Mtanzania pia limeripoti shule yenye wanafunzi 480 katika wilaya ya Serengeti ina madawati matano tu (5).Muasisi wa Taifa letu , Mwalimu Nyerere alituasa ili nchi iendelee tunahitaji mambo manne SIASA SAFI, ARDHI, UONGOZI BORA NA WATU . Hakuna ubishi kwamba bado hatuna uongozi bora kwani imepita miaka 50 tangu Uhuru kukiwa na awamu nne za uongozi lakini changamoto kama hizi si ngeni miongoni mwa watanzania, Siasa yetu nayo bado ina madhaifu hilo halina ubishi. Leo tuachane na UONGOZI MBOVU NA SIASA MBOVU kabisa, tujiangalie SISI (WATANZANIA) kama wananchi tujiulize tumefanya nini kuhakikisha tunaondokana na changamoto hizi? Je ni kwa kiwango kipi tumefanikiwa katika yale tuliyofanya katika kuleta mabadiliko ? Nini wajibu wetu watanzania katika kutatua changamoto hizi?. Hii ni aibu kwetu sote, kwangu mimi, yule na wewe. Tafakari na tujadili hatua zipi zichukuliwe kuhakikisha changamoto hizi zinatatuliwa.
 
 souce Haki Elimu
 

Jumanne, 12 Agosti 2014

wanaobeza juhudi za Mbunge Vincent Nyerere hawaitakii mema sekta ya elimu Musoma

Mbunge wa Musoma Mjini Vincent Nyerere na walimu wa shule ya Sec Kiara
siku ya leo napenda kuchukua fursa hii kuzungumzia japo kwa uchache juhudi za Mbunge wa jimbo la Musoma Mjini Vincent Nyerere. kwa kile alichokifanya hivi karibuni kwa kugawa Computer pamoja na Projector kwa baadhi ya shule za Sekondari za hapa Musoma Mjini na kuahidi kugawa zingine hivi karibu
Sababu kubwa ya kuzungumzia suala hili ni baadhi ya wanasiasa wasioitakia mema sekta ya elimu kuendelea kudai kuwa hakukuwa na haja ya kugawa Computer kwa wanafunzi kwa wakati huu na badala yake angefanya kitu kingine na si kugawa computer.
harakati za marafiki wa elimu musoma tunapatikana hasa Kata ya kigera na katika Shule ya sekondari Kiara ambayo iko kata ya Kigera wamebahatika kugawiwa Computer 5 pamoja na Projector 1 na mbunge kuaidi kuwapatia tena Computer zingine 5

tatizo letu na wanaobeza juhudi za Mbunge huyu ni kwanini wao hawasemi ambacho mbunge angefanya kwa sasa kizuri zaidi ya kugawa hizo computer,
na Je hao wanaobeza watoto wao  wanasoma shule zetu za kata au wanasoma zile za St fulani  zenye kila kitu shuleni ikiwa ni pamoja na computer

kwa nini wanabeza maendeleo kwa watoto wa maskini , je si haki watoto wa maskini kuwa na computer mashuleni?

Je watoto wa maskini wa shule za kata wakifahamu kutumia computer ni jambo baya

sie marafiki wa elimu tunaamini kwamba hao watoto wa maskini wa shule za kata wana haki ya kumiliki computer mashuleni mwao kwani hata wakifeli kidato cha nne watakuwa na nguzo kidogo huenda wakawa masekretari kwani watakuwa walau na uzoefu wa kutumia computer
marafiki wa elimu tunapongeza juhudi za Mbunge huyu
na daima tukumbuke kuwa Elimu Ni taaluma isiyohitaji wanasiasa kuiharibu kwa siasa zao za kubeza mema yanayofanywa na mtu kisa tu si chama kile au itikadi ile

Tafakari chukua! hatua kiongozi bora ni yule anaethamini wapiga kura wake wa maendeleo ya elimu kwenye jimbo lake.

imeendikwa na Rafiki wa elimu
      Juma Richard Okumu

Jumatatu, 4 Agosti 2014

Miaka 30 kisiwa hakina shule, watoto 300 hawana pa kusoma


Mmoja wa kina mama wenye watoto kisiwani Kome Mchangani akiwa katika mizunguko yake ya kila siku kisiwani humo hivi karibuni.
Wakati taifa likiendelea na mikakati mbalimbali ya kuboresha elimu nchini ikiwa ni pamoja na kuwapo kwa Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN), hali ni tofauti kwa watoto zaidi ya 300 wanaoishi katika Kisiwa cha Kome Mchangani kilichopo kwenye Ziwa Victoria, Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza baada ya kutojengwa shule kwa zaidi ya miaka 30.

Uchunguzi uliofanywa na NIPASHE kwa zaidi ya wiki mbili kwenye kisiwa hicho umebaini kuwa tatizo hilo halitokani na kuwapo kwa hamasa ndogo ya elimu kwa wazazi wa watoto hao; bali ni matokeo ya utekelezwaji wa Sheria ya Uhifadhi Misitu ya Mwaka 2002, katika kifungu cha 26 kinachokataza mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na kujengwa kwa majengo ya kudumu.

Kisiwa cha Kome Mchangani ni miongoni mwa visiwa vya Ziwa Victoria vilivyotangazwa na serikali kuwa hifadhi ya misitu.

Kiongozi wa wakazi na wafanyabiashara wa mazao ya samaki katika kisiwa hicho, Tibenda Luhuya, aliiambia NIPASHE kuwa wamejitahidi kupigania uwapo wa shule na huduma nyingine za jamii kisiwani humo kwa muda mrefu lakini hakuna wanachoambulia zaidi ya kuambiwa kuwa sheria za nchi haziruhusu.

"Tunaelezwa kuwa eneo lote la kisiwa (cha Kome) halitakiwi kuwa na majengo ya kudumu na hivyo, serikali haiwezi kutujengea shule wala zahanati kwa sababu kufanya hivyo ni kuvunja hizo sheria," alisema Luhuya.

Hata hivyo, wakati shule na majengo mengine ya kudumu yakizuiwa, serikali imeruhusu kuwapo kwa jengo la kudumu la vyumba vitatu ambalo linatumiwa na Kikosi cha Usimamizi wa Fukwe (BMU).

"Bado tunaendelea kuisihi serikali kuwa itujengee shule kwa ajili ya watoto wetu ambao wanaishia kuvua samaki tu na kukosa elimu ambayo ni haki yao ya msingi," aliongeza.

Anasema kisiwa hicho kina wakazi zaidi ya 5,000 na kinahesabika kipo katika Kijiji cha Buhama, Kata ya Nyakasasa, Tarafa ya Buchosa. Umbali wa kutoka kisiwa hicho mpaka Kijiji cha Buhama ambako kuna Shule ya Msingi ni zaidi ya kilomita tano.

Akieleza zaidi, Luhuya anasema kwa zaidi ya miaka 30 tangu wavuvi na wafanyabiashara wa mazao yatokanayo na samaki walipoanza kuishi hapo hawajawahi kuwa na shule na hivyo, baadhi ya wazazi hulazimika kuwapeleka watoto wao kwa ndugu, jamaa na marafiki wanaoishi nje ya kisiwa hicho ili wakasome.

Hata hivyo, anasema zoezi hilo limekuwa gumu kwa kuwa baadhi ya wazazi wakishawapeleka huko (kwa ndugu zao), huwa wanawatelekeza na matokeo yake watoto hao wanarudi wenyewe kwa kuomba nauli na wengine kuingia ndani ya boti inazokwenda kisiwani humo bila ya kuwa na nauli.

WATOTO, WAZAZI WANENA
"Inaniuma sana kujikuta naishi bila kujua kusoma na kuandika. Wazazi wangu ni wavuvi na wote hawakusoma. Lakini na mimi nitaishia kuwa mvuvi nisiyejua kusoma na kuandika kama wao kwa sababu hapa kwetu (Kome) hakuna shule," ndivyo anavyoanza kueleza mtoto mmojawapo kisiwani Kome Mchangani, John (11).

Ibrahimu anasema kuwa kwa muda mrefu amekuwa akisikia kwamba kuna harakati zinafanywa za kuiomba serikali iwajengee shule. Lakini hadi sasa hakuna kilichofanyika na anaamini kuwa yeye na watoto wenzake wote kisiwani humo hawatapata fursa ya kujua kusoma na kuandika.

"Mimi inaniuma sana kwa kutojua kusoma... huwa ninawaona baadhi ya watu wanasoma magazeti na vitabu, hasa wanaotoka Mwanza kuja kununua samaki huku kwetu. Lakini mimi sijui kusoma wala kuandika.Ninachokijua zaidi ni kuvua na kufanya kazi ya kusomba dagaa kutoka ziwani kuwaleta nchi kavu," anasema Ibrahim.

Mtoto aitwaye Yona, mwenye umri wa miaka 10, anasema kutokana na kisiwa hicho kukosa shule, wazazi wake walimpeleka Mwanza mjini kwa rafiki yao ili akasome huko, lakini hilo halikuwezekana kwa sababu huko alikopelekwa, wenyeji hawakuipa shule nafasi na hata watoto wao (wa wenyeji) hawakuwa wakienda shule.

''Sasa nimerudi kwa wazazi wangu hapa kisiwani. Nimekaa wala sijui kama nitasoma... naendelea na kazi ya kibarua cha kusomba samaki kutoka katika mitumbwi ya wavuvi nyakati za jioni,'' alisema.

Tatu Kipile ni mmoja wa wakazi wa kisiwa cha Kome Mchangani. Anasema kuwa yeye ameshindwa kumpeleka shule mtoto wake anayeishi naye huko kutokana na kukosa fedha za kumsafirisha kutoka kisiwani humo na kumhudumia wakati anapokwenda kwenye eneo lenye shule.

"Nilihamia hapa (Kome) wakati mwanangu akiwa na miaka mitatu. Sasa ni zaidi ya mwaka wa tano niko hapa. Ninapenda sana mwanangu asome, lakini sina namna ya kufanya kwa sababu kisiwa hiki hakina shule na sina fedha za kumpeleka kwenye maeneo ya mbali yaliyo na shule za msingi," alisema mama huyo.

Hellen Cosmas alisema analazimika kumpangia chumba jijini Mwanza mtoto wake mwenye umri wa miaka 10 ili apate fursa ya kusoma, ingawa anasema bado kuna changamoto nyingi ya kutekeleza azima yake hiyo kwa sababu hana mwangalizi maalum.

"Hivi sasa nimemrudisha hapa kisiwani (Kome) kwa sababu mazingira ya kuishi Mwanza ni magumu. Hana mwangalizi na hivyo sasa niko naye hapa... haendi tena shule," alisema Hellen.

Sara Machera bado hajabahatika kupata mtoto. Hata hivyo, alisema kuwa hali iliyopo sasa ni ngumu kwa wazazi wa kisiwa hicho kutekeleza jukumu la kusomesha watoto wao kwavile hakuna shule. Aliongeza kuwa watoto wanaopelekwa kwa ndugu zao ili wasome ni kama huwa wanatelekezwa kwani uangalizi huwa mdogo.

Neema Abel ambaye pia bado hajapata mtoto anasema watoto kisiwani humo hukosa elimu kwavile hakuna shule na hivyo anaiomba serikali ifikirie kuwajengea shule ili kuokoa mamia ya watoto walio katika hatari ya kuwa wajinga, wasiojua kusoma wala kuandika.

VISIWA VINGINE
Tatizo la shule linalowakabilia wakazi wa kisiwa cha Kome Mchangani lipo pia katika visiwa vingine kadhaa vilivyomo kwenye Ziwa Victoria.
Mwanamama Agnes Joseph, mkazi wa kisiwa cha Ikulu alisema kuwa yeye ana watoto watano, na wote amewapeleka kwa mama yake ambako ni katika eneo lisilokuwa la kisiwa wilayani Sengerema ili wasome.

"Huwa ninawatembelea kila baada ya miezi miwili na kuwaachia fedha za matumizi... sitaki wanangu wakose fursa ya elimu," anasema Agnes.
Kiongiozi wa Kisiwa cha Ikulu Baharini, Juma, alisema watoto kukosa elimu na kuishia kuwa wavuvi kwa sababu ya kukosekana kwa shule ni janga kubwa kwao na taifa.

Alisema kwavile serikali inafahamu kwamba kwenye visiwa kuna mamia ya watu ambao ni Watanzania halisi, inapaswa kuchukua hatua sahihi ya kuwajengea shule.

Kiongozi wa Kisiwa cha Ito, Neema Elias, alisema eneo hilo lina wakazi (wavuvi) zaidi ya 500, lakini hakuna shule kwa ajili ya watoto wao.
Aliongeza kuwa tatizo la watoto kukosa elimu kwa sababu ya serikali kutokubali kujenga shule lipo pia katika visiwa vingine vingi miongoni mwa visiwa 35 vilivyopo katika Ziwa Victoria, hasa kwenye eneo la Wilaya ya Sengerema.

Alisema licha ya kukosekana shule katika eneo hilo, lakini pia wamepata maagizo ya serikali kwamba kamwe hawaruhusiwa kuishi kisiwani humo wakiwa na watoto wao.

"Hii siyo sawa.  Wazazi wanapozaa watoto wanalazimishwa kuwaondoa watoto kwa madai kwamba hakuna shule na tunatakiwa kuwapeleka kwa ndugu, jamaa na marafiki walio katika maeneo yenye shule, nje kabisa ya visiwa. Lakini hili limeshindikana... bado tunaishi na watoto wetu na matokeo yake wanakosa elimu," anasema.

OFISA ELIMU, MBUNGE
Akizungumzia tatizo la kukosekana kwa shule, Ofisa mtendaji wa Kata ya Nyakasasa, Mathayo Kanisiro alisema, eneo la visiwa hivyo ni msitu wa hifadhi na kwamba serikali imeagiza pasijengwe nyumba wala jengo lolote la kudumu.

Kanisiro alikiri kwamba hakuna namna ya kufanya, lakini amekuwa akistushwa na ukubwa wa tatizo kwani watoto wanaoishi na wazazi wao katika visiwa hivyo bila kupata haki yao ya msingi ya elimu imezidi kuongezeka.

Diwani wa Kata ya Nyakasasa, Avoid Geogratias, anasema eneo hilo la visiwa wanalokalia wavuvi na familia zao, lilitengwa kwa ajili ya hifadhi ya mistu miaka mingi iliyopita na kwamba, awali, wavuvi waliruhusiwa kuishi huko ili kulinda misitu huo dhidi ya watu waliokuwa wanapasua mbao.

Naye, kama ilivyo kwa Kanisiro, alisema hana namna yoyote ya kuwasaidia watoto hao ili wapate nafasi ya kusoma na kwamba, anajua kwamba watoto wamezidi kuwa wengi kama wanavyoongezeka wazazi wao (wavuvi).

Ofisa Elimu wa Wilaya ya Sengerema, Juma Mwajombe, alisema kuwa siku za nyuma kulikuwa na utaratibu wa wa wazazi kuchangishana fedha kisha kuwapeleka watoto wao kusoma nje ya visiwa. Lakini mpango huo ulifikia mwisho mwaka 2010 baada ya kutokea ajali ya kuzama kwa mtumbwi na wanafunzi 18 walipoteza maisha.

"Baada ya kutokea kwa ajali hiyo, zoezi hilo lilisimamishwa na hadi sasa watoto wengi wameendelea kuishi visiwani bila kupata elimu," alisema Mwajombe, aliyeelezea wasiwasi mwingine kuwa huenda misitu itakuwa hatarini kwa sababu baadhi ya wakazi wa visiwani wataona hakuna haja ya kulinda misitu wakati watoto wao wakikosa elimu kwa kutojengewa shule kwa sababu ya zuio litokanalo na sheria ya kulinda misitu.

Ofisa Ustawi wa Jamii wa Wilaya ya Sengerema, Consolata Magaka, alisema serikali inafahamu shida wanayopata wazazi na watoto walio kweney visiwa kama Kome Mchangani, lakini hakuna namna ya kufanya.

Alisema serikali haiwezi kupeleka huduma za shule kwa kuwa wananchi hao wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi wako aktika eneo la hifadhi ya misitu.
Mbunge wa jimbo la Buchosa Wilaya ya Sengerema, Charles Tizeba, aliiambia NIPASHE kuwa, kama kuna mwananchi anayetaka kuendelea kukaa kisiwani (kama Kome) ambako ni hifadhi ya misitu, lazima amuondoe mtoto wake huko na kumrudidisha alikozaliwa ili ampatie fursa ya kusoma.

Alisema hawezi kuwatetea wananchi wake hao kujengewa shule visiwani, kwani kufanya hivyo ni kuvunja sheria ya misitu ambayo inakataza kuwapo kwa majengo ya kudumu.

Akizungumza na NIPASHE, Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Focus Majimbi, alisema ni vigumu kujenga shule kwenye kisiwa cha Kome na visiwa vingine vya hifadhi ya misitu kwani sheria inazuia maeneo hayo (ya hifadhi ya misitu) kujengwa majengo ya kudumu. Aliitaja sheria hiyo kuwa ni namba 14, ya mwaka 2002, kifungu cha 26.

Majimbi alikiri kwamba suala la ukosefu wa elimu kwa watoto ni baya na lina athari kubwa. Alisisitiza kuwa, kwa kuzingatia sheria hiyo ya hifadhi ya misitu, maeneo ya visiwa hivyo hayatakiwi kujengwa shule wala jengo lolote la kudumu na kwamba serikali imeagiza kuhamisha watoto wote walioko huko ili wakasome katika maeneo mengine.

Hata hivyo, amri hiyo ya serikali ya kutaka watoto wanaozaliwa huko waondoshwe inakiuka sheria nyingine ya nchi; namba 21 ya mwaka 2009 ambayo inalinda haki za watoto wenye umri chini ya miaka 18.

Wilaya ya Sengerema ina ukubwa wa kilomita za mraba, 8,817 na kati ya hizo, kilomita za mraba 3,335 ni nchi kavu sawa na asilimia 38 na kilomita 5, 832 ni nchi kavu, sawa na asilimia 62.

Kwa mujibu sensa ya watu na makazi ya mwaka 2010, wilaya hiyo ina watu 662,166 na kati ya hao, wanaume ni 335,756 na wanawake ni 326,410.
CHANZO: NIPASHE

Ijumaa, 1 Agosti 2014

Waziri mkuu aagiza kumalizwa kwa tatizo la madawati

Waziri mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda ameagiza wakuu wa mikoa kote nchini kuhakikisha wanamaliza tatizo la uhaba wa madawati katika shule za msingi ifikapo juni 31 mwakani ikiwa ni kabla ya kumalizika kwa mwaka huu wa fedha ili serikali inapoanza mwaka mpya wa fedha shule zote nchini ziwe na madawati ya kutosha.
Waziri mkuu Mizengo Pinda ambaye amewasili jijini Mbeya kwa ajili ya kuhudhuria kongamano ya uwekezaji katika mikoa ya nyanda za juu kusini ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa ya mkoa wa Mbeya ambayo imeonyesha kuwa kuna tatizo kubwa la uhaba wa maawati katika shule za msingi.
 
Aidha waziri mkuu ameonyesha kutoridhishwa na ufaulu wa wanafunzi wa shule za msingi katika mkoa wa Mbeya, ambao mwaka jana wanafunzi wake wamefaulu kwa asilimia 48.5 ikiwa ni chini ya lengo la taifa la ufaulu wa asilimia 60, hivyo akatoa agizo kwa mkoa huo kuhakikisha unaweka mikakati itakayowezesha mwakani wanafunzi kufikia kiwango cha ufaulu ambacho kimewekwa kitaifa.

Waziri mkuu aagiza kumalizwa kwa tatizo la uhaba wa madawati

Waziri mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda ameagiza wakuu wa mikoa kote nchini kuhakikisha wanamaliza tatizo la uhaba wa madawati katika shule za msingi ifikapo juni 31 mwakani ikiwa ni kabla ya kumalizika kwa mwaka huu wa fedha ili serikali inapoanza mwaka mpya wa fedha shule zote nchini ziwe na madawati ya kutosha.
Waziri mkuu Mizengo Pinda ambaye amewasili jijini Mbeya kwa ajili ya kuhudhuria kongamano ya uwekezaji katika mikoa ya nyanda za juu kusini ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa ya mkoa wa Mbeya ambayo imeonyesha kuwa kuna tatizo kubwa la uhaba wa maawati katika shule za msingi.
 
Aidha waziri mkuu ameonyesha kutoridhishwa na ufaulu wa wanafunzi wa shule za msingi katika mkoa wa Mbeya, ambao mwaka jana wanafunzi wake wamefaulu kwa asilimia 48.5 ikiwa ni chini ya lengo la taifa la ufaulu wa asilimia 60, hivyo akatoa agizo kwa mkoa huo kuhakikisha unaweka mikakati itakayowezesha mwakani wanafunzi kufikia kiwango cha ufaulu ambacho kimewekwa kitaifa.

Jumanne, 29 Julai 2014

ZAIDI YA WANAFUNZI 860 WA SEKONDARI WILAYANI KILINDI WAMEACHA SHULE.


Wanafunzi zaidi ya 860 wa shule mbali mbali za sekondari wilayani Kilindi wameacha shule kwa sababu mbali mbali ikiwa ni pamoja na baadhi ya wazazi wao kuwaozesha huku wengine wakiwekwa kinyumba na baadhi ya makundi ya vijana.
Mkuu wa wilaya ya Kilindi bwana Selemani Liwowa amesema hayo katika kikao cha baraza la madiwani ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Dr . Jakaya Kikwete kuwataka viongozi wa mkoa wa Tanga kuhakikisha kuwa watuhumiwa waliosababisha tatizo hilo wanakamatwa na kufunguliwa kesi katika vyombo vya sharia.
Akielezea mikakati waliyojiwekea na hatua zitakazochukuliwa mkuu huyo wa wilaya amesema kwanza wanataka wawarejeshe watoto hao kwa wazazi kisha watawakamata wazazi na watuhumiwa waliowakatisha masomo kwa ajili ya kuwachukulia hatua kali za kisheria zoezi ambalo linaanza utekelezaji wake baada ya sikukuu ya eid kumalizika.


chanzo ITV

Wanafunzi 140 wakwepa masomo tunduma na kujihusisha na biashsra ndogondogo.

Zaidi ya wanafunzi 140 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu katika halmashauri ya mamlaka ya mji mdogo wa Tunduma wilayani momba mkoani Mbeya bado hawajaripoti shuleni kuanza masomo na badala yake wanadaiwa kujihusisha na biashara ndogondogo kama vile kuuza karanga na kubeba mizigo mpakani mwa Tanzania na Zambia mjini Tunduma.
Akizungumza kwenye baraza la halmashauri ya mamlaka ya mji mdogo wa Tunduma, mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya momba ambaye pia ni katibu tawala wa wilaya hiyo, Mathias Mizengo amesema kuwa halmashauri ya mamlaka ya mji mdogo wa Tunduma inakabiliwa na changamoto ya baadhi ya vijana ambao wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu kutoripoti shuleni na hivyo akawataka viongozi wa mamlaka hiyo kuhakikisha vinaja hao wanatafutwa kila mahali walipo na kuwapeleka shuleni.
 
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Juma Kitabuje amesema kuwa hadi kufikia mwezi juni mwaka huu wanafunzi 144 kati ya wanafunzi 956 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika mji wa Tunduma ndio ambao walikuwa hawajaripoti shuleni kati yao wanafunzi 70 wakiwa ni wavulana na wanafunzi 74 wasichana huku akielezea sababu kubwa ya watoto hao kutohudhuria masomo kuwa ni kutelekezwa na wazazi na kujihusisha na biashara za kuuza karanga na kubeba mizigo mpakani.
 
Kuhusu hatua ambazo zinachukuliwa na mamlaka hiyo kuhakikisha kuwa wanafunzi hao wanaendelea na masomo, mkurugenzi huyo amesema kuwa wazazi wa watoto hao wamefikishwa kwenye baraza la kata na kupewa muda hadi kufikia Agosti 25 mwaka huu kuwasaka watoto wao popote walipo na kuwapeleka shuleni.

Kwa wasiomfahamu mwalimu.

Mwalimu JK Nyerere

1. Ndiye rais aliyewahi kulipwa mshahara kidogo duniani
 
2.ndiye mtu aliyeitetea china isitengwe na UN, baada ya mataifa yote kuogopa vtisho vya marekani, wachina wanamtambua na kumheshimu sana

 
3. Ndiye rais pekee aliyetishia kuvunja balozi za uingereza, ujeruman na ufaransa na hata kukataa msaada wao kwa kitendo chao cha kuunga mkono serikali ya kibaguz afrika kusini

 
4. Ndiye rais aliyewezesha watoto wa masikin wasome bila ada na matibabu bure. Nenda nchi za kenya, afrika kusini . Kama baba yako hakushirik harakati za ukomboz ili utoke labda uwe jambaz maana huwez hata kujilipia ada


Ndiye rais pekee aliyechukia ufisadi toka moyoni.

Jumanne, 22 Julai 2014

binti aliyekeketwa alilia shule

 Akiwa darasa la nne alikamatwa kwa nguvu..
Mama mzazi wa binti muathirika wa ukeketaji akifafanua 
Mama mzazi wa binti muathirika wa ukeketaji akifafanua jambo huku akisikilizwa na binti yake.
Kuna mambo mengi anakumbukia msichana mwenye umri wa miaka 12  yamemtokea maishani. Lakini tukio la siku hiyo, kuitwa na mama yake mdogo, kisha kukamatwa kwa nguvu na kukeketwa  linabaki kuwa kovu lisilopona katika maisha yake. Ni ukatili uliopitiliza uliobadili kabisa ndoto za maisha yake za kupata elimu.
 
Binti wa miaka 12 (jina linahifadhiwa)  ni mtoto wa mwisho wa kike kati ya watoto nane wa mzee Isaya na Mama Gyar Baa kutoka familia moja ya kabila la Kimbulu.
 
Kabla  hajakumbwa na mkasa uliobadilisha kabisa welekeo wa maisha yake, alikuwa mwanafunzi wa darasa la nne mwenye  ndoto za kusoma hadi kufikia ukomo wa maisha yake.
Hata hivyo, ndoto hizo zilizimwa baada ya  kujikuta akilazimishwa kukeketwa ikiwa ni ishara ya maandalizi ya kutafutiwa mume ili aolewe.Tukio hilo la kikatili liliathiri maisha yake.
 
Makazi ya familia ya binti huyo ni katika kijiji cha Konje wilaya ya Handeni mkoani Tanga, kilichopo umbali wa kilometa 16 kutoka Handeni mjini.
 
Msichana huyo, anatoka katika familia ya wafugaji, yenye tabia ya kuhamahama ili kufuata malisho, hasa nyakati za ukame ili kuhakikisha kuwa mifugo yao haikosi chakula na maji.

Akisimulia kwa uchungu mkasa alioupata uliobadili kabisa uwelekeo wa maisha yake, msichana huyo anasema siku hiyo ya Jumanne (hakumbuki tarehe) aliitwa na mama yake mdogo (mama wa kambo). Aliitika na kutii amri kwa kwenda kusikiliza alichoitiwa akiwa hana fununu kabisa ya dhamira ya muitaji.
 
Anasema baada ya kufika nyumbani kwa mama yake huyo, alishangazwa kumkuta dada yake anayemfuata (jina linahifadhiwa) akiwa amefungwa mikono na miguu huku akilia kwa uchungu sana. Kilichomsikitisha zaidi ni kuona jinsi ambavyo dada yake alikuwa akivuja damu nyingi katika sehemu zake za siri.
 
Jambo hilo, lilimtisha sana Tansiana na kutokana na hamaki akapata wazo na maamuzi ya haraka ya kukimbia  kutoka nyumbani kwa mama yake mdogo  ili kujinusuru na hatari aliyoona kuwa inamkabili. Hata hivyo, hakufanikiwa kutimiza matakwa yake.
 
“Nilishtuka sana, kumuona dada akilia huku damu zinamtoka kwa wingi  sana katika sehemu zake za siri. Lakini nilivyotaka kukimbia mama mdogo  na bibi yule niliyemkuta pale nyumbani ambaye sikufahamu ametokea wapi wakanikamata na  kunifunga mikono na miguu kwa kamba,” anasimulia msichana huyo kwa masikitiko.
 
Baada ya kufungwa na kudhibitiwa kikamilifu ndipo bibi huyo asiyemfahamu akachukua kiwembe na kumkata kwenye sehemu yake ya siri kwa namna alivyojiridhisha na kusababisha atokwe damu nyingi kama ilivyokuwa kwa dada yake.
 
“Wakati  wananikata sikusikia maumivu sana kwa sababu nilikuwa na hasira sana kwa kile kitendo nilichokiona amefanyiwa dada yangu…ndipo  baada ya kupita muda kama kama saa moja hivi nikaanza kusikia maumivu makali sana kama roho inataka kutoka. Ndipo nikatambua namna gani watu wale walivyo wakali. Nilikuwa nimefanyiwa unyama wa hali ya juu bila ya ridhaa yangu. Nililia sana na kwa hakika nimemchukia sana huyo mama mdogo na sijui kama nitamsamehe,” anasema.
 
Akikumbukia zaidi anasema kuwa “wakati wananifanyia unyama huo, mama yangu mzazi alikuwa amesafiri kwenda Karatu na baba  hakuwapo nyumbani. Aliporudi alikuta tayari tumekeketwa.”
 
Anabainisha kwamba, ilimchukua takriban mwezi mmoja kuuguza kidonda hicho hadi kupona. Aina ya matibabu aliyokuwa akipewa anasema kuwa, ni kupakwa maziwa na mafuta ya taa mara mbili kwa siku.Yaani asubuhi na jioni kama dawa ya kuponyesha jeraha hilo. Alipata msongo mkali wa mawazo kuhusu tukio hilo baya kabisa na la ukatili wa kupindukia.
Baba yake, licha ya kutabua unyama waliofanyiwa, lakini hakuchukua hatua zozote dhidi ya wahalifu wale.
 
Anasema kuwa, miongoni mwa sababu walizoelezwa zilizolazimisha wachukuliwe hatua hiyo kukeketwa ni watoto wa kike kuwafanya waachane na vitendo vya uhuni kwa kile kinachodaiwa kuwa, wasipokeketwa wanakuwa na tamaa kali ya  kufanya mapenzi muda wote.
 
Hii ni kutokana na mila na desturi za kabila lao, kwamba iwapo binti hatakeketwa, basi ni dhahiri kwamba hatapata mume wa kumuoa na hatakuwa na heshima wala thamani anayostahili kupewa mwanamke kwenye jamii hiyo.
 
Kutokana na kitendo hicho, anasema kuwa ni dhahiri kwamba ameandaliwa kwa ajili ya kuolewa, hata kama jambo hilo litafanyika litakuwa ni kinyume cha ridhaa yake.
 
“Najua sasa hivi nasubiri tu kuolewa. Lakini ni kwamba watanilazimisha tu lakini mimi mwenyewe sipendi…napenda sana kusoma… natamani sana ajitokeze mtu wa kunisaidia katika hilo. Nipo tayari kabisa kwa hilo…na baada ya kusoma cha kwanza nitakachofanya ni kuhakikisha nazuia mila hii mbaya isiendelee kufanyika kwa wasichana wengine wa jamii hii. Kwa kweli inauma sana…tunateseka sana jamani,” anasema msichana huyo huku akibubujikwa machozi.
 
Msishana huyo, licha ya hatua ngumu ya maisha yake aliyopitia, lakini ana matumaini kuwa, siku moja atakuwa mwanaharakati wa kutetea haki za wanawake, na kupiga vita mila na desturi ambazo zimekuwa zikitumika kumgandamiza mwanamke.
 
Aina hiyo ya maisha, ndiyo imechangia kwa kiasi kikubwa kumfanya msichana huyo kuwa miongoni mwa wale waliokosa fursa ya kupata haki yake ya msingi hasa elimu. Alikuwa na ndoto za siku moja kupata elimu ili uwe mwanga wa uhakika kwa maisha yake na jamii yake inayomzunguka.
 
Pamoja na kukabiliwa na changamoto hiyo maishani, lakini binti huyo  katika familia yake ana msimamo wa kupenda elimu na kujituma kwa kazi za kifamilia na kwamba iwapo atatokea mfadhili yoyote atakayekuwa tayari kumchukua na kwenda kumsomesha  hata wazazi wake sasa wameutambua ukweli huo na kuwa tayari kumruhusu aende akapate elimu.
 
“Kamwe sitasahau unyama huu…nikipata elimu lazima niwe mwanaharakati wa kupinga unyama huu ,” anasema.
Mama mzazi wa binti huyo aitwaye Gyar Baa Isaya anasema kuwa wakati binti yake anakeketwa, alikuwa safarini na hakushirikishwa na mumewe kuhusu kufanyika kwa kitendo hicho.

Kimsingi anasema, alikuwa anafahamu kuwa siku moja binti yake atalazimika kufanyiwa mila hiyo kwa sababu ni utamaduni ambao hata yeye ameupitia na hakuwa na mamlaka ya kuupinga, kwani kwa kufanya hivyo, angeweza kumsababishia matatizo mtoto wake ikiwamo kutoolewa.

“Kusema kweli kwa mila za kwetu ili uonekane ni mwanamke ambaye umekamilika ni lazima ukeketwe…vinginevyo hupati mume na unaweza kupatwa na majanga makubwa  ikiwamo binti kuanza tabia mbaya kabla ya wakati wake…sasa watoto wangu wamelazimika kufanyiwa mila hiyo ingawa hawakuridhika nayo kabisa,” anasema mama huyo.

Naye  dada wa msichana huyo aliyeanza kufanyiwa ukatili huo, anasema kuwa sababu kubwa ya mdogo wake kushindwa kuendelea na masomo licha ya kuwa na ndoto za kufika mbali kimaisha ni ile hofu ya kuchekwa na wenzake hasa wakati wa kuoga wakimuona amekeketwa.

“Unajua mnapokuwa rika moja mnakuwa hamuoneani aibu kabisa, hata kama kuoga mtaenda wote, sasa wenzako wakikuona uko tofauti na wao kimaumbile wanakushangaa na wengine wanakucheka. Hali hii nilipokuwa nikimwelezea mdogo wangu ilichangia kumkatisha tamaa ya kusoma kwa hofu ya kuchekwa,” anasema dada huyo ambaye  ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule moja.

Hata hivyo anasema, kitendo walichofanyiwa kinadhihirisha udhalilishaji kwa mtoto wa kike na kwamba licha ya baba yao kuwa ni miongoni mwa wafugaji wenye tabia ya kuhamahama, lakini amedhamiria kuhakikisha kuwa anamaliza masomo yake.

“Baba yetu ni miongoni mwa wafugaji wenye tabia ya kuhamahama makazi, hali hii imetuathiri sana kielimu tena mimi ni nafuu kwa sababu naishi kwenye hosteli za shule. Mdogo wangu ndiyo amerudi nyuma kwani hadi sasa hasomi na  aliishia darasa la nne,” anasema dada huyo.
CHANZO: Ippmedia.com

Jumamosi, 19 Julai 2014

Waliohitimu la 7 Vijibweni waitwa kuchukua vyeti



BAADA ya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Vijibweni, Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, Mathew Jasembe kutuhumiwa kupoteza vyeti vya wanafunzi 247 waliohitimu darasa la saba mwaka 2011 amewataka wafike shuleni kuchukua vyeti vyao.
Tuhuma hizo ziliibuliwa na baadhi ya wazazi wa wanafunzi hao, wakisema wamechoshwa na ahadi za mwalimu huyo kwa zaidi ya miaka miwili sasa tangu vyeti hivyo kupotea, ziliandikwa na gazeti hili hivi karibuni.
Wazazi hao walidai mkuu huyo alihusika kwa sababu hakuwa wazi kueleza mazingira halisi ya jinsi vyeti hivyo vilivyopotea na kwamba hakupenda suala hilo lifike ngazi za juu.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, mwalimu huyo, alisema tofauti zilizojitokeza awali hadi kusababisha vyeti hivyo kuchelewa kukabidhiwa kwa wahitimu zimepatiwa ufumbuzi na vyeti hivyo vipo tayari.
Alisema baada ya mchakato wa kuviandaa vyeti hivyo kukamilika tangu juzi, klichobaki ni kuwakabidhi wahitimu hao.
“Mbona nimeanza kuwakabidhi wachache waliopata taarifa… nimeweka matangazo katika eneo linalozunguka shule kwa ajili ya kuwajulisha kuwa vyeti vyao vipo tayari ni wao wenyewe sasa.
“Niwaombe wazazi kupitia gazeti lenu wa waambie watoto wao waende shuleni hapo wakachukue vyeti vyao,” alisema Jasembe.
Hivi karibuni wazazi wa watoto hao, walifikisha tuhuma hizo kwa Mbunge wa Kigamboni, Faustine Ndugulile, Ofisa Elimu na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke.

Jumatano, 16 Julai 2014

SHULE YA ISANGO ILIYOKUWA IKIMILIKIWA NA JUMUIYA YA WAZAZI CCM YAUZWA KWA BEI CHEE

Photo: shule ya sekondari Isango iliyoko Kinesi Wilaya ya Rorya mkoa wa Mara imeuzwa kwa bei sawa na bure ya sh. milioni 125

wakizungumza kwa nyakati tofauti mwenyekiti wa ccm na mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wilaya ya Rorya kupitia kituo cha radio Victoria Vfm wamedai kuwa shule hiyo imeuzwa kijanja janja kwani tangu mwenyekiti huyo wa wazazi aingie madarakati hakuwahi kuambiwa juu ya uwepo wa deni lililopelekea kuuzwa shule hiyo.
mwenyekiti huyo wa jumuiya ya wazazi alienda mbali zaidi na kusema kitendo hicho kimefanywa makusudi kwa lengo la kumharibia uwajibikaji wake kwani kadai aliyeinunua shule hiyo ni mtoto wa aliyekuwa Mwenyekiti wa wazazi ccm mkoa wa Mara.
pia kasema kuwa dalali alionyesha wazi muenendo wa rushwa, kwa kugonga nyundo ya mwisho wakati bado wateja wengine wakiendelea kupandisha dau.

baada ya hapo ametoa wito kwa wananchi kumuunga mkono ili kuhakikisha shule hiyo inarejeshwa kwa wananchi baada ya kuwaambia wananchi hao kuwa tayari wamekwisha fungua kesi mahakama ya rufaa na hivi karibuni atakwenda kuonana na katibu mkuu wa chama cha mapinduzi ili kuhakikisha shule hiyo inarejeshwa mikononi mwa wananchi.shule ya sekondari Isango iliyoko Kinesi Wilaya ya Rorya mkoa wa Mara imeuzwa kwa bei sawa na bure ya sh. milioni 125

wakizungumza kwa nyakati tofauti mwenyekiti wa ccm na mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wilaya ya Rorya kupitia kituo cha radio Victoria Vfm wamedai kuwa shule hiyo imeuzwa kijanja janja kwani tangu mwenyekiti huyo wa wazazi aingie madarakati hakuwahi kuambiwa juu ya uwepo wa deni lililopelekea kuuzwa shule hiyo.
mwenyekiti huyo wa jumuiya ya wazazi alienda mbali zaidi na kusema kitendo hicho kimefanywa makusudi kwa lengo la kumharibia uwajibikaji wake kwani kadai aliyeinunua shule hiyo ni mtoto wa aliyekuwa Mwenyekiti wa wazazi ccm mkoa wa Mara.
pia kasema kuwa dalali alionyesha wazi muenendo wa rushwa, kwa kugonga nyundo ya mwisho wakati bado wateja wengine wakiendelea kupandisha dau.

baada ya hapo ametoa wito kwa wananchi kumuunga mkono ili kuhakikisha shule hiyo inarejeshwa kwa wananchi baada ya kuwaambia wananchi hao kuwa tayari wamekwisha fungua kesi mahakama ya rufaa na hivi karibuni atakwenda kuonana na katibu mkuu wa chama cha mapinduzi ili kuhakikisha shule hiyo inarejeshwa mikononi mwa wananchi.

Jumatano, 9 Julai 2014

Tunataka wapate maarifa au wajue Kiingereza? makala ya Gervas Zombwe.

Tafiti zote duniani zinasema wazi kuwa binadamu yeyote anajifunza na kuelewa kikamilifu anapofundishwa kwa lugha anayoijua zaidi. Na uwezo wa kujenga utambuzi na kukuza vipawa umo ndani ya mila na desturi asilia zinazofungamana moja kwa moja na lugha mama inayomiliki maarifa na michepuo ya akili.
Kufundishwa kwa lugha asiyoielewa vizuri kunamzuia binadamu kumiliki maarifa ya kukuza michepuo ya akili. Kweli atasoma, atapata cheti, digrii, lakini maarifa na ubunifu viitabaki nje ya utambuzi wake.
Ndiyo maana nchi zote zilizoendelea wanafundisha watu wao kwa lugha zao. Huwezi kubuni kwa kutumia lugha ya jirani, huwezi kufikiri kwa kutumia lugha ya kukopa, kuwezi kuvumbua kwa kutumia lugha ya kigeni. Ni ndoto!
Mwalimu wa lugha, mtafiti na mtetezi wa lugha Profesa Martha Qorro, siku zote kupitia tafiti nyingi alizofanya amekuwa akisisitiza manufaa ya kutumia lugha ya taifa kufundishia vijana wetu.
Ili mwanafunzi afike ngazi ya juu kabisa ya uelewa, ni lazima maarifa yapitie kwenye lugha anayoijua vizuri. Vinginevyo atakuwa anajifunza juu juu tu na kuishia kwenye uelewa wa hatua ya mwanzo tu. Hatua za uelewa ziko kama ifuatavyo:
Hatua ya kwanza, uwezo wa lugha ya ‘kuombea maji’. Akilazimika kujifunzia lugha katika ngazi hii mzungumzaji inabidi akariri karibu kila kitu kwa kuwa ana uelewa mdogo. Huchukua muda mrefu kuelewa mambo madogo kwa kuwa lugha ni kikwazo. Haoni uhusiano kati ya maisha yake na mambo yale anayofundishwa au anayoelezwa shuleni. Masomo humchosha na mawazo huhama darasani.
Hatua ya pili, uwezo wa kumpa mtu maelekezo ya namna ya kufika sehemu fulani. Uelewa wa juu juu wa mambo yanayozungumzwa au kufundishwa kwa lugha hiyo. Tabia ya kukariri bado inaendelea, ingawa imepungua kwa kiasi kikubwa. Uwezo wa kuandika sentensi fupi fupi sahihi na kuuliza maswali rahisi. Kuna uwezekano mkubwa wa kutoelewa au kuelewa vibaya maana iliyokusudiwa. Uhuru wa fikra haupo!
Hatua ya tatu, uwezo wa kufikiri, kutafakari, kujadili, kuchambua na kuchanganua masuala na dhana mbalimbali yanayozungumzwa au kufundishwa kwa lugha husika. Mzungumzaji anakuwa na uwezo mkubwa wa kutumia lugha kama nyenzo ya kuvumbua mambo mapya. Ana uhuru wa kutumia lugha husika na yote atakayoelezwa katika kujikomboa kimawazo.
Katika hatua hii, lugha siyo kikwazo katika kuelewa, kupambana na changamoto za maisha. Hahitaji kukariri; bali hutumia uelewa wake katika kujibu maswali au kutoa maelezo juu ya yale anayoyaelewa. Ni katika hatua hii ya uelewa ndiyo wanafunzi wanapoweza kujifahamu, kujitambua, kuwa mbunifu, kutumia fursa, kujiendeleza, kutafiti na kutatua changamoto zinazomzunguka. Wanafunzi wetu wengi shuleni na vyuoni hawafiki hatua hii. Ushahidi unaonyesha shule za sekondari hawajifunzi na kupata maarifa kutokana na lugha. Kwa mfano, tafiti nyingi (Mlama na Matteru 1978, Criper and Dodd 1984, Roy-Campbell and Qorro 1987, Rubagumya, Jones and Mwansoko 1998, Qorro 1999, Mwinsheikhe 2003, Puja 2003, Brock Utne 2004, Vuzo 2005) zimeonyesha kuwa wanafunzi wengi katika shule za sekondari na vyuo nchini Tanzania wana uwezo wa hatua ya kwanza au ya pili ya uelewa wa lugha inayotumika kufundishia.
Kwa kung’ang’ania kutumia lugha wasiyoelewa, tunawafundisha wanafunzi wetu kushindwa! Wengi wao wanajifunza kutodadisi, kutofikiri, kutokuuliza maswali, kunakili na kukariri, kuwa waoga, kutojiamini, kukubali kila hali na kukata tamaa kwa kauli ya “yote maisha”. Ni vyema tukajiuliza, kuandaa vijana wasioweza kuelewa, kujadili, kufikiri, kuchambua na kuchanganua masuala na dhana mbalimbali zinazofundishwa ni kwa masilahi ya nani? Ni wazi kwamba tunahitaji elimu ya kujikomboa na kwamba ili kufanikisha elimu ya kujikomboa shuleni na vyuoni, ni lazima wanafunzi watumie lugha ambayo wao na walimu wao wana uelewa wa hali ya juu.
Katika hali ambayo wanafunzi wana uelewa mdogo wa lugha, wanafunzi wengi, hasa wasichana, huwa wanyonge na kwa muda mwingi hunakili maandiko ya mwalimu (mengine yakiwa na makosa) kwa kadri watakavyoweza kuyasoma. Maandiko hayo kwa sehemu kubwa wengi hawayaelewi.
Badala ya kujifunza masuala ya msingi, wanafunzi wanaishia kukariri maneno kwa lugha wasiyoelewa na muda mwingi unapotea na ari ya kusoma inapungua. Elimu hii ya kunakili na kukariri haiwapi uwezo wa kujikomboa bali huenda kinyume na makusudio.Kama tunataka maendeleo ya kweli, Waafrika ni lazima wachukue mamlaka juu ya taratibu zinazotumika kuendesha elimu yao. Lazima wafundishe watoto wao kwa lugha wanazoelewa ili kuwaandaa kuwa wadadisi wa kutafuta majibu ya matatizo yanayoikabili jamii. Ikumbukwe kuwa lengo kuu la elimu ni maendeleo siyo umahiri wa lugha fulani. Ni falsafa mbadala!

Jumapili, 6 Julai 2014

umuhimu wa Kiswahili kama Lugha ya kufundishia elimu ya sekondari


Lugha ya kufundishia Sekondari ni Kiingereza. Wadau wengi wanasema hii ni sababu moja ya vijana kutoelewa/kufeli. Tufundishe kwa Kiswahili? Sote tunatambua kwamba Elimu ndio nguzo muhimu kwa maendeleo na katika kurekebisha Elimu yetu suala la lugha ni muhimu. Tutafakari pia msingi wa elimu ni nini hasa? Msingi wa elimu ni kupata maarifa na kuyatumia kujiendeleza na kujenga jamii. Sababu ya elimu ni kupata maendeleo. Elimu sio kwa ajili ya ajira tu. Shabaha ya elimu pia ni kujenga udadisi na ubunifu katika kutafuta majawabu ya changamoto ndani ya jamii. Je maarifa hayawezi kupenyezwa kwa Kiswahili? Tukisema Kiswahili hakijitoshelezi maana yake tunakatia tamaa uwezekano wa kukipanua? Katika nchi ndogo lakini zilizoendelea - Sweden, Norway, Denmark, Finland - lugha zilizotumika kuvumbua mambo ni zao. Hii haiwezekani hapa kwetu? Je ni kweli watu hufikiria kwa lugha yake ya asili? Ukimlazimisha mtu afikirie, abaini na avumbue kwa lugha isiyo yake ataweza au ataiga tu? Lugha sio kwa ajili ya mawasiliano tu na walimwengu wengine. Lugha pia ni kwa ajili ya kujenga fikra na kujitambua. Elimu haina majibu ya shida zote za jamii. Na elimu ya kukaririsha majibu haifai. Elimu inapaswa kujenga uwezo na maarifa ya kutafuta MAJAWABU.

na january makamba

Jumanne, 1 Julai 2014

nini kinaendelea kwenye shule zetu?

Mwananchi 1 tu kati ya 10 ndiye anayefikiri kuwa watoto wengi wanaomaliza darasa la 2 wana uwezo wa kusoma na kufanya hisabati wa darasa hilo hilo (ngazi ya darasa la 2). Mbaya zaidi, wananchi 3 tu kati ya 10 (31%) wanafikiri kuwa watoto hawa wanapaswa kuwa na uwezo wa kusoma na kuhesabu kwenye ngazi yao; ikimaanisha kuwa wananchi hawana matumaini kama kweli mfumo wa elimu utawafundisha watoto ujuzi na stadi wanazotakiwa kupata wakiwa shuleni.
Matokeo haya yalitolewa na Twaweza kwenye muhtasari wa utafiti wenye jina la Nini kinaendelea kwenye shule zetu? Wananchi watafakari juu ya hali ya elimu. Muhtasari huu umetokana na takwimu kutoka Sauti za Wananchi, utafiti wa kwanza Afrika kwa njia ya simu mkononi wenye uwakilishi wa kitaifa ambao unauwakilishi wa kaya zote Tanzania Bara.
Muhtasari huu unachunguza hali ya shule zetu, ufundishaji na ujifunzaji pamoja na ushiriki wa wazazi kwenye elimu ya watoto wao. Licha ya matarajio ya chini kwenye mfumo wa elimu, wazazi mara nyingi hutimiza wajibu wao kuhamasisha na kusimamia ujifunzaji. Wanafunzi 7 kati ya 10 waliripoti kuwa wazazi wao hupitia na kukagua madaftari yao mara kwa mara.
Walimu wana wajibu wa kuhakikisha watoto wanajifunza shuleni. Hata hivyo, hawawezi kufanya kazi hii kama walimu wenyewe hawaingii darasani. Wanafunzi 3 kati ya 10 walithibitisha kuwa mwalimu wao muhimu aliingia darasani vipindi vyote siku iliyopita. Wanafunzi 4 kati ya 10 (38%) waliripoti kuwa mwalimu wao hakuingia darasani siku nzima, na wanafunzi 3 kati ya 10 (28%) walisema kuwa, mwalimu aliingia baadhi ya vipindi tu vya siku hiyo.
Sauti za Wananchi iliuliza pia maswali kuhusu hali ya mazingira ya shule. Karibu wanafunzi wote (99%) wanafundishwa wakiwa madarasani, siyo nje, na wanafunzi 9 kati ya 10 (91%) hukaa kwenye fomu au dawati shuleni. Hata hivyo, ni nusu tu ya idadi ya wanafunzi (49%) waliosema hupewa chakula shuleni. Ingawa kukosekana kwa viti na madarasa kuna uwezekano wa kuathiri viwango vya kujifunza, watoto wanapokuwa na njaa wanakuwa na uwezo mdogo kupokea na kumiliki maarifa mapya.

chanzo twaweza tanzania

Tatizo la mimba kwa wanafunzi wa kike, serikali bado kigugumizi

kassim majaliwa
Nilikuwa nikisikiliza maelezo ya Mbunge Kasim Majaliwa, akiwa Bungeni, kuhusiana na suala la mimba za utotoni, na kama ni vizuri wanafunzi wanaopata mimba wasirudishwe au warudishwe shuleni kuendelea na masomo baada ya kujifungua. Na kuwa kama  kurudishwa shule hakutakuwa ni mfano mbaya kwa wengine, au kutakuwa ni faida.

Mimi nataka kusema kuwa hakuna hasara yoyote kwa kumrudisha msichana shuleni baada ya kujifungua, na sababu ziko nyingi!
‘Kosa’ la mwanafunzi wa kike ni moja tu, kuwa na tumbo linaloweza kukaa mtoto, na kuonekana hadharani kuwa alijihusisha katika mapenzi na hakuweza kujikinga na hatimaye alipata mimba.

Na kuwa wale waliohusika (nasema ni wengi waliohusika) na kupatikana kwa mimba ya huyu msichana hawana tumbo kama hilo, au wamejitenga na uwajibikaji kwa kosa husika.

Kabla sijafika huko kwenye kutaja walio na makosa yaliyosababisha mimba, nataka niulize? Hivi kweli Tanzania, serikali na watu wake wako tayari kuendelea na maisha ya karne ya ishirini na moja wakiwa na watu wasiojua kusoma na kuandika, watu ambao wana elimu nusunusu, watu ambao hawana uwezo wa kuajiriwa na kujiajiri?

Kisa ni kuwa msichana huyu amepata mimba akiwa mtoto- tena mimba ya utoto! Msichana huyu atakuwa ni mzigo kama asipoachwa aendelee na masomo, na hataweza kumudu maisha yake.

Katika nchi ambayo inataka kila mtu awe mjasiriamali, haiwezi kuruhusu kikundi cha watu wachache au wengi kuishi bila elimu, au elimu ya kutosha. Msichana huyu ataturudishwa nyuma kimaendeleo kama akiachwa asiendelee na shule kwa kosa dogo la mimba.

Waliohusika na kupatikana kwa mimba kwa huyu mtoto ni wazazi? Wazazi wajiulize kama walikaa na mtoto ambaye tayari amekua na kubalekhe, ili kumpa mwongozo bora wa maisha na umuhimu wa elimu kwake, na umuhimu wa urafiki na watu wa rika mbalimbali, lakini wakiwa waangalifu kuhusiana na suala la mapenzi? Au wazazi walitegea walimu, na walimu hawakuwajibika ipasavyo kwani walidhani kuwa wajibu wao ni kuwapatia elimu tu, ambayo ni masomo ya msingi bila kuhusisha stadi za mahusiano na maisha? Walimu wamekuwa wakiwalea watoto kwa muda wa kati ya saa 6 kwa siku hadi saa kumi na mbili, na wakati mwingine kwa miezi mitano hadi kumi kwa mwaka.

Hawa ni wazazi wa pili wa mwanafunzi huyu mdogo kwa umri, asiye na stadi kamilifu za mahusiano, na hawampatii mafunzo kuhusiana na hilo. Ukienda shule nyingi hakuna mfumo wa elimu ya unasihi ambapo mtoto anaweza kufika ofisini kwa mnasihi akihisi anasumbuliwa na mahusiano, au anataka kujiingiza kwenye mahusiano lakini hana uhakika na njia sahihi ya kuenda nayo.

Mtoto anajikuta akiishi kwa kubahatisha katika mahusiano ambao mengi yanaainisha ngono kama ndiyo msingi wa mahusiano. Na utaona hao hili lilimsababishia mtoto kupata mimba, ingawa eti lawama zinabaki kwa mtoto.

Watoto wanapotoka kwenye familia ya masikini, na kufika katika jamii ambako watoto wenzao wanakula vyakula vizuri, wana mali za kisasa, na wanaishi wakiwa na fedha zao wenyewe walizopewa na wazazi, siyo rahisi kujitoa katika mitego kama miongo ya kimalezi ya wazazi na ya shuleni ni hafifu au haipo.

Watoto hawa wanzongwa na mifumo ya habari na tamaduni pendwa ambavyo  vinawachagiza kujiingiza katika mahusiano au tabia ambazo zitawaingiza katika mahusiano bila kuwa na mwongozo sahihi.

Na watoto kama wageni katika dunia hii, wanapaswa kuwasaidia kuwaongoza watoto hao ili waelewe maana ya vitu wanavyokutana navyo. Watoto wanatakiwa kuongozwa, na wengi wa watoto waliopata mimba utotoni hawakuongozwa vizuri. Hawa walihusika kumpatia mtoto mimba, kwa sababu hawakutimiza wajibu wao!

Kinanishangaza zaidi pale ambapo aliyehusika na kudunga mimba anajulikana, au hata kama hajulikani, anaachwa aendelee na maisha yake, na mtoto wa kike ndiye anayebeba lawama. Kwa hili hatutofautiani na wale ambao mwanamke na mwanaume wakikamatwa wanazini, anayepigwa mawe na kuuawa ni mwanamke; mwanamke akibakwa, anayepigwa mawe na kufa ni mwanamke.

Wakati mwanaume, aliyehusika kumbaka, tena inajulikana kuwa ndiye aliyefanya hivyo, anaachwa aishi kwa raha na starehe akiendelea kuvizia wanawake  wengine wa kubaka.

Angalia jinsi vyombo vya habari vinavyohusika na kuwaambia watoto kuwa mapenzi kati yao inawezekana. Michezo ya kuigiza ya televisheni, redio, magazeti, na filamu, vyote hivi vinawaambia wanaume na wanawake kuwa mapenzi ya watoto kwa watoto, watoto na watu wazima, yanawezekana.

Kwa kifupi utaona kuwa waliohusika na kupewa mimba msichana ni wengi kutokana na tabia zao, ulegevu wao katika malezi na sera, lakini eti msichana ndiye pekee anabakizwa na kosa.

Huu ni uonevu. Ndiyo maana ninashangaa kusikia serikali inasita kumtambua mtoto wa kike kuwa ni kiumbe asiye na kosa!

Jumanne, 17 Juni 2014

Hali ya Elimu Tanzania

moja ya darasa shule ya msingi Bisumwa wilaya ya butiama


nchi haiwezi kuendelea na watu wachache wanaopata fursa za kipekee kwenye shule chache huku elimu ya jamii pana ikiwa mashakani. Hakuna haja ya kulumbana wala kuingiza siasa katika elimu, bali serikali itekeleze mipango na sera zilizopo na kuboresha mapungufu kwa kushirikisha wadau, na ukweli wa hali ya elimu nchini usisulubiwe wala kubezwa bali tuupokee na kuuwekea mikakati kwa pamoja tuweze kuboresha elimu yetu. pa kuanzia ni kila mmoja katika eneo lake,na kikubwa kufanya zaidi ya mazoea

Jumatano, 11 Juni 2014

changamoto ya elimu toka Geita


Walimu 97 katika shule ya msingi Nyankumbu na Mkombozi katika Wilaya ya Geita, wanatumia tundu moja la choo ambacho kipo kwenye nyumba ya mwalimu huku wanafunzi wa shule hizo 3,563 wakitumia matundu 14 ya choo na kuhofiwa kutokea magonjwa ya milipuko.

chanzo. jamii forums

Jumanne, 10 Juni 2014

kelele za Mbatia kuhusu ubora wa elimu je anasikilizwa?

james mbatia
Mbunge James Mbatia unajisumbua. Natambua uchungu ulio nao juu ya kudorora kwa sekta ya elimu, na natambua uhitaji wako wa mabadiliko katika sekta hii mapema inavyowezekana, lakini unajisumbua.

Sisemi kuwa ukate tamaa, na mimi sikati tamaa, ila naona unazungumza na watu ambao hawawezi kuelewa maana ya kile unachosema na kuhimiza. Nataka nieleza yafuatayo.

Mwaka jana ulipozungumza kuhusu mitaala, kuwa hakuna na kuwa sekta ya elimu inaendeshwa mzobemzobe kama Waluguru ambavyo wangesema, na kuwa vitabu vinavyotumika katika shule zetu havina uhakika wa ubora wake walikubeza, walikutukana, walikutenga, na kukuona mzushi.

Lakini wiki mbili baada ya kuahirishwa kwa Bunge, matokeo ya mitihani yakatoka, na kilichotokea, kuhusu kufeli kwa wanafunzi, Mungu tu anajua.
Mungu alikulipia na kuwaaibisha wale waliodhani kuwa ulikuwa mzushi, na ukarabati uliofanyika kuhusiana na matokeo hayo, na unaondelea kufanyika, sijui, ni suala la kuliombea taifa liondokane na pepo huyu ambaye hataki sisi tulioko serikalini tusikilize mawazo ya wananchi wenzetu.

Kuwa wananchi wenzetu wanapotushauri wanaonekana kuwa ni adui, na kuwa lengo lao sio kujenga ufanisi katika kutoa huduma bali kwa waliotupigia kura, bali kwa sababu wanataka kutujengea hoja tushidwe uchaguzi ujao.

Mbatia, unapokuwa na serikali ambayo wasiwasi wake ni kama itashindwa uchaguzi wa miaka mitano ijayo, na sio kama miaka mitano ijayo watakuwa na cha kuwaonyesha wananchi, katika orodha ndefu ya ahadi ndani na nje ya ilani ya uchaguzi waliyoinadi, sidhani kama unachokisema kitaeleweka.

Tumeona mwaka 2011, mara baada ya uchaguzi malumbano yakaanza ndani ya wanaserikali na walioko nje ya serikali, lakini wote wa chama kimoja, wakifanya maandalizi ya uchaguzi wa 2015.

Vikundi vya uchaguzi wa 2010 havikuvunjwa, kwa kweli vikaimarishwa na kampeni za uchaguzi kiaina zikaanza kwa makini kabisa, hadi walipoonyana wenyewe kwa wenyewe, lakini wale wenye masikio magumu wanaendelea bila kujali kitu.

Sasa hawa watu unapowaambia kuhusu kuimarisha sekta ya elimu unadhani inawezekana kweli, mawazo sio katika huduma bali katika kufanikisha chaguzi.

Mbunge Mbatia, maendeleo kwa wananchi kwa sasa, wewe unajua, sio kigezo cha kuchaguliwa. Hizo siasa zako ni za kizamani.

Sasa hivi unachaguliwa kwa sababu unaweza kutoa takrima, unaweza kuwanunulia watu ubwabwa wakashiba, ukawanunulia watu t-shirts, kofia na khanga, na kuwaimbisha nyimbo jioni wakala wakashiba.

Wananchi wa siku hizi hawaoni uhakiki wa utendaji wa walio madarakani kama ni kigezo, bali uwezo wake wa kutoa rushwa kwa wapiga kura. Sasa unapokuwa na uhakika wa kushinda kwa kutumia fedha na sio utendaji, unaanzaje kufikiria kuboresha elimu.

Elimu haikuwa kwenye ajenda wakati wa uchaguzi, ilitamkwa majukwaani kwa sababu mdomo haukosi cha kuzungumza ukikaa mbele ya kinasa sauti.

Kitu kingine ambacho unanishangaza James Mbatia ni kuwa huoni dunia inakwendaje?. Fasheni siku hizi ni kuhakikisha kuwa  watoto wanakwenda kusoma nje, na kama ni ndani basi katika shule za watu wakubwa, na wewe ukiwemo, nitashangaa kama haumo, kuwapeleka watoto kwenye English Medium, au sijui International Schools.

Unashangaa, mimi hapa ni waziri wa elimu, ofisa elimu, mkurugenzi wa elimu, mwalimu wa sekondari au mwalimu wa shule ya msingi, nimepewa dhamana ya kuhakikisha kuwa elimu inaboreshwa, na tulidhani kigezo kimojawapo ni kutuona sisi wenyewe tunawasomesha watoto wetu nje au ndani, lakini katika shule za serikali.

Lakini aka! Sasa kama tuliopewa dhamana ya kuboresha elimu tunakwepa shule zetu wenyewe, si ujue kuwa kuna jambo ambalo ni bovu tunaliona, na hatusemi ila tunawahamisha watoto wetu. Watoto wa masikini wajua wapi pa kuwapeleka wa kwao.

Kumeundwa kampeni kuwa wazazi wawagharimie watoto wao, badala ya kuimarisha shule za serikali, wanahimiza kuanzisha shule za binafsi.
Hivi kama kweli serikali ina nia ya kuboresha elimu, hao wazazi ambao wanalipa mabilioni ya fedha kwa ajili ya watoto wao, kama wangelipa robo tu ya hizo fedha kwenye shule za serikali kama ada, na serikali ikaweza kuboresha huduma na ubora wa, elimu, kungekuwa kweli na malalamiko dhidi ya sekta ya elimu?

Tungewaokoa wazazi wangapi ambao wanalipa ada kwenye shule ambazo hazina chochote ila utapeli. Lakini nadhani hatuwezi kufikiria kwa umakini.
Tunataka majibu rahisi kwa kitu kigumu, na hatutaki kufikiria kwa mkakati—strategically, bali kwa kuishi kama tulivyozoea.

Mbatia, tunahitaji kupungwa pepo huyu ambaye hataki kusikiliza vilio vya Watanzania kuhusu elimu.

Ijumaa, 6 Juni 2014

Kenya wanafunzi wanaenda na laptop shuleni Tanzania wanaenda na vidumu vya maji na fagio.

waziri mkuu Mizengo Pinda
Mbunge Maryam Salum Msabaha (Viti Maalum, Chadema), ameitaka serikali kutoa maelezo kuhusu chenji ya rada iliyotolewa ili kusaidia kupunguza tatizo la madawati katika shule za nchini kwa kuwa mpaka sasa wanafunzi wanaendelea kukaa sakafuni huku nchi jirani ya Kenya wanafunzi wake wakienda la Laptop.

Msabaha aliuliza katika kipindi cha maswali na majibu ya papo hapo ambayo hujibiwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kila Alhamisi.

Alisema nchi yoyote iliyoendelea duniani ilianza kuwekeza kwenye elimu na kutoa mfano wa nchi ya Malyasia, lakini hapa nchini watoto wanabeba madumu ya maji na fagio na kuketi sakafuni, wakati nchi jirani ya Kenya wanaenda na Laptop shuleni.

“Tuliambiwa chenji ya rada itapunguza tatizo mashuleni, lakini mpaka sasa watoto wanakaa chini na dawati moja wanakaa watoto mpaka watano,” alisema.

Akijibu, Waziri Mkuu  Pinda alisema jitihada ambazo serikali inafanya kuhusu elimu ni kuchukua maamuzi makubwa ambayo yamefanya suala la elimu kuzaa changamato kubwa kutokana na uandikishaji wa darasa la kwanza hadi la saba kuongezeka na kusababisha mahitaji  ya shule za sekondari, elimu ya juu ya vyuo vikuu kuongezeka.

Aliwataka Wabunge waendelee kusaidia serikali  ili bajeti ya Wizara ya Elimu iendelee kukua siku hadi siku kwani kukua kwa bajeti hiyo kutaongeza mambo mengi.

Katika swali  la nyongeza Msabaha alitaka kujua wakati huu wa utandawazi wa Sayansi na Teknolojia, serikali inachukua hatua gani kuona wanafunzi wa shule za msingi wanaanza kwenda shule na Laptop.

Hata hivyo, wakati akijibu, Waziri Mkuu Pinda alimhoji “unataka laptop kwa watoto wote wa shule inawezekana? Kwa sababu lazima uulize hilo swali.”

Alisema suala la wanafunzi wa darasa la kwanza mpaka la saba si kuwa na Laptop bali ni kuwa na mfumo wa digitali ambao utamwezesha vitabu vyake vyote kuwa ndani ya kompyuta kwa kutumia kifaa kinachoitwa tablets  badala ya kubeba mzigo mkubwa wa vitabu.

Jumanne, 3 Juni 2014

wanafunzi DIT wagoma kufanya mitihani

Wanafunzi wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) wamegoma kufanya mitihani ya muhula kutokana na wenzao 684 kutopatiwa namba za mitihani kwa madai ya kutokamilisha usajili.

Mgomo huo umesababisha mitihani iliyopangwa kufanyika jana asubuhi na mchana kutofanyika kutokana na wanafunzi hao kugomea kuingia vyumba vya mitihani.

Akizungumza na NIPASHE Rais wa serikali ya wanafunzi, Himida Elihuruma, alisema wamelazimika kugomea mitihani hiyo kwa sababu kuna wanafunzi walifanya usajili tangu Februari, lakini hawajapewa namba za mtihani kwa maelezo kuwa hawajakamilisha taratibu.

“Kuna wanafunzi wamesajiliwa baada ya kukamilisha taratibu zote tangu Februari, lakini  la kusikitisha hawajapatiwa namba kwa kuambiwa kwamba hawajafanya usajili,” alisema Elihuruma.

“Ofisi ya Uhasibu imegubikwa na rushwa, kuna ushahidi wa baadhi ya viongozi na wanafunzi waliombwa ili watafutiwe fomu ambazo zimepotea hali iliyopelekea hadi leo kutopata namba za mtihani,” alisema.

Aidha, alisema kumekuwapo na ubaguzi unaofanywa na utawala kwa kuwanyima namba za mitihani wanafunzi waliokamilisha usajili na kuwapa ambao hawajakamilisha. Aliongeza kuwa uongozi wa chuo umekuwa na utaratibu mbovu wa kupanga tarehe za usajili na kwa mara ya kwanza ilipangwa Machi 7  ikasogezwa Mei 16 hadi 23, mwaka huu bila kutoa taarifa kwa wanafunzi.

Wanafunzi waliohojiwa na gazeti hili walisema hawatafanya mitihani hiyo hadi pale wenzao watakapopewa namba.

Ofisa Uhusiano wa taasisi hiyo, Amani Kakana, alisema mgomo huo hautambuliki na mitihani iliyogomewa jana itapangwa tena na usajili hautaongezewa muda.

“Tulitoa muda wa kutosha wanafunzi kufanya usajili walioshindwa kufanya kwa wakati hawawezi kupatiwa namba, tunafuata utaratibu wa chuo uliopangwa unaoleweka na wanafunzi,” alisema Kakana.

“Mwanafunzi anayejielewa hawezi kugomea mtihani, ratiba haitaharibika itaendelea kama ilivyopangwa, tutamchukulia hatua kali mtu yeyote atakayejaribu kuchochea vitendo vya uvunjifu wa amani,” alisema.

souce ippmedia & nipashe