Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumapili, 31 Agosti 2014

Timu ya Haki Elimu uso kwa uso na afisa elimu (shule ya mwisenge)

afisa elimu bi. Beatrice Mkina akiteta kidogo na wafanyakazi wa Haki Elimu walipokutana shule ya msingi Mwisenge
maktaba ya kisasa iliyojengwa na Haki Elimu shule ya msingi Mwisenge

wanafunzi wasioona shule ya Mwisenge kujengewa kiwanja cha michezo


Afisa elimu Msingi manispaa ya Musoma Mjini Bi
. Beatrice Mkina alibainisha mpango wake wa kuwezesha shule ya msingi Mwisenge kujengewa kiwanja cha michezo kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavua wa macho.
siku ya ijumaa 29/8/2014 afisa elimu huyo aliitembelea shule ya msingi Mwisenge kwa minajili ya walimu wa shule hiyo kumpendekezea eneo zuri la ujenzi wa kiwanja hicho cha michezo
afisa elimu akiangalia eneo lililopendekezwa kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja cha michezo
afisa elimu katikati na baadhi ya walimu na wajumbe wa kamati ya shule
hii ni juhudi nzuri kwa serikali kuwakumbuka wanafunzi wasioona wa shule ya msingi mwisenge.
Afisa elimu kushoto na mjumbe wa kamati ya shule mwisenge