Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatatu, 28 Oktoba 2013

maafisa elimu watakiwa kuthamini michango ya walimu

mkuu wa wilaya ya Arusha
Mkuu wa Wilaya ya Arusha, John Mongella, amesema mabadiliko ya haraka katika elimu yanaweza kutokea iwapo walimu watawezeshwa kitaaluma na kuwahimiza maafisa elimu kutoa motisha na kutambua mchango wa anayefanya vizuri ili kuwajengea zaidi morali.

Mongella aliyasema hayo katika hafla maalum ya kutoa zawadi na vyeti kwa wanafunzi wa kidato cha tatu waliofanya vizuri mitihani ya majaribio kwa  mikoa ya Arusha na Kilimanjaro katika masomo ya Hisabati, Elimu viumbe, Kemia, Fizikia na Kiingereza iliyoandaliwa na asasi ya Asante Africa Foundation , Africaid na Chuo Kikuu cha Elimu cha Mwenge kilichopo mjini Moshi.

 “Kuendelea kwa nchi yoyote ile ni pale inapokuwa na wana sayansi wengi zaidi…mwanasiasa gani utaendesha nchi ambayo haina wanasayansi?” alihoji.
Alisema maofisa elimu wanaweza kuanzisha mradi kama huo wa kufanya majaribio ya mitihani kwa wanafunzi wa sekondari zilizopo kwenye mikoa yao au kwa kushirikiana na mikoa mingine.

“Hii ni changamoto kwa maofisa elimu, wanaweza kutenga hata Sh. milioni 10 kwa ajili ya walimu wa masomo hayo na kama wanafunzi watakuwa wamefanya vizuri wanaweza kuzawadiwa,” alisema.

Mongella alisema  hata katika programu  ya ‘Matokeo makubwa sasa’ inahitaji walimu waongezewe uwezo ili wanafunzi waweze kufanya vizuri zaidi na inawezekana kuwa hivyo kwa kuwashindanisha.

Kwa upande wake, meneja wa mradi huo wa uwezeshaji walimu wa shule za sekondari, Sokoro Munubi, alisema malengo yao yanaendana na mpango wa serikali unaosisitiza 'matokeo makubwa sasa' katika sekta ya elimu.

“Kwanza tunawajengea uwezo walimu kwa kuwapatia mafunzo ya mara kwa mara pamoja na kufanya ufuatiliaji wa mafunzo yanayotokana na walimu wao wenyewe katika maeneo ya shuleni.

Akizungumzia mafanikio ya mradi huo tangu kuanzishwa kwake, alisema umekwisha kufundisha walimu 80 wa sekondari 40 zilipo wilaya tisa za mikoa ya Kilimanjaro na Arusha.

Alisema walimu 560 kutoka shule hizo nao wamekwisha kufundishwa na walimu wenzao katika maeneo ya shule zao na pia mradi umefadhili mitihani ya majaribio kwa wanafunzi wa kidato cha tatu na kwamba wanafunzi 4,500 walishiriki kufanya mtihani huo.
Alisema kuanzia mwakani mradi huo unatarajia kuongeza mikoa miwili lengo likiwa kufikia mikoa sita kwa baadaye.
chanzo. ippmedia.com & nipashe

madudu yagunduliwa tume ya pinda

Ripoti ya Tume ya Kuchunguza Matokeo ya Kidato cha Nne iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda mapema mwaka huu, iliibua madudu mengi ambayo hayajawekwa hadharani.
Wajumbe waliounda kamati hiyo kwa nyakati tofauti waliliambia gazeti hili hivi karibuni kuwa waligundua mambo mengi yanayodhihirisha udhaifu mkubwa katika uendeshaji wa sekta ya elimu nchini. Sehemu kubwa ya matokeo ya uchunguzi huo inasemekana yamejikita zaidi katika kuzitupia lawama taasisi za Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET).
Udhaifu wa kiutendaji kati ya taasisi hizo mbili unadaiwa umechangia kwa wanafunzi wengi kufanya vibaya kwenye mitihani ya Kidato cha Nne mwaka jana kiasi cha kuilazimisha Serikali kuunda tume kuchunguza tatizo kutokana na kilio kikubwa cha wadau wa elimu na wananchi.
Viongozi watatu waandamizi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi hawakupatikana kuzungumzia uchunguzi huo jana. Simu ya Waziri wa wizara hiyo, Dk Shukuru Kawambwa haikupatikana kabisa pale ilipopigwa.
Naye Naibu wake, Philipo Mulugo alijitetea kwamba alikuwa na shughuli nyingi na hivyo hakuwa na muda wa kuzungumzia suala hilo wakati Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Sifuni Mchome hakupokea kabisa simu yake.
Matokeo hayo ya mtihani wa Kidato cha Nne uliofanyika mwaka jana yanaonyesha kuwa watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 walipata sifuri, huku wanafunzi 23,520 tu ambao ni sawa na asilimia 5.16 ndiyo waliofaulu na wengine 103,327 sawa na asilimia 26.02 wakiwa wamepata daraja la nne. Katika mtihani huo, watahiniwa 397,136 walikuwa wa shule na 68,806 wa kujitegemea.
Kutokana na hali hiyo, Waziri Mkuu Pinda aliamua kuunda tume iliyoanza kufanya kazi kuanzia Machi hadi Juni mwaka huu. Tume hiyo iliyokuwa inaongozwa na Profesa Mchome ilimkabidhi Waziri Mkuu ripoti Juni 15, mwaka huu.Hata hivyo, ripoti hiyo haijawahi kutolewa hadharani baada ya tume kumaliza kazi yake.
Badala yake imeshuhudiwa Profesa Mchome, ambaye alikuwa Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Vyuo Vikuu Tanzania akipandishwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Huku kwa upande mwingine, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (Necta), Dk Joyce Ndalichako akichukua likizo ya muda mrefu ya mapumziko.
Madudu yaliyogunduliwa na tume
Wajumbe wa tume hiyo walisema kuwa matokeo ya uchunguzi wao yalibaini kuwa, maswali na mitihani iliyotungwa ilikuwa ni ile yenye kuzingatia maudhui badala ya kuzingatia kujenga maarifa na ujuzi.
“Tulitegemea kwa vile tangu mwaka 2006, mihutasari ya elimu ya Tanzania ilibadilika kutoka ile inayozingatia maudhui, kwenda kwenye ile inayozingatia kujenga maarifa na ujuzi basi na mtihani ungekuwa na mwelekeo huo,” alisema mmoja wa wajumbe wa tume ile.
Pia uchambuzi wa kamati ile uligundua kuwa hakukuwapo mawasiliano kati ya Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na Baraza la Mitihani la Taifa (Necta).TET, ambao ndio wasimamizi wa mitalaa ya elimu walitakiwa kuhakiki mitihani ile baada ya kutungwa na Necta, lakini hilo halikufanyika.
Chanzo kingine kililiambia gazeti hili kuwa tume hiyo ilibaini katika uchunguzi wake kuwa Necta ilitumia wataalamu wasio na juzi wa kutosha kutunga na kuhakiki mitihani. Uchunguzi huo ulibaini baadhi ya mitihani kama ya masomo ya Hisabati, Kemia na Fizikia ilikuwa na maswali yaliyohitaji muda mwingi wa kuyajibu kuliko uliopangwa.
“Hii ilifanya wanafunzi kushindwa kukamilisha kujibu maswali yote yaliyotakiwa kujibiwa kwenye mitihani hiyo. Pia tulibaini kwamba baadhi ya maswali katika mitihani ya masomo ya Fizikia na Kemia yalikuwa nje ya mihutasari iliyotumika kuwaandaa wanafunzi,” aliongeza mjumbe mwingine.Mjumbe mmoja aliongeza pia kuwa mitihani ilikuwa na misamiati migumu na hata kuwasumbua walimu walioisahihisha.
Hali hii inaweza kuwa imechangia, kwa kiasi kikubwa, kuongeza ugumu wa mitihani hiyo na hili linaweza kuchangia wanafunzi kushindwa kuelewa vizuri maswali wanayoulizwa kwenye mitihani.
Wajumbe wa tume hiyo walieleza hali hiyo imefanya imani kujengeka kuwa mitihani ya Tanzania ni migumu kuliko ya nchi nyingine.Huku kwa upande mwingine, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (Necta), Dk Joyce Ndalichako akichukua likizo ya muda mrefu ya mapumziko.
Madudu yaliyogunduliwa na tume
Wajumbe wa tume hiyo walisema kuwa matokeo ya uchunguzi wao yalibaini kuwa, maswali na mitihani iliyotungwa ilikuwa ni ile yenye kuzingatia maudhui badala ya kuzingatia kujenga maarifa na ujuzi.
“Tulitegemea kwa vile tangu mwaka 2006, mihutasari ya elimu ya Tanzania ilibadilika kutoka ile inayozingatia maudhui, kwenda kwenye ile inayozingatia kujenga maarifa na ujuzi basi na mtihani ungekuwa na mwelekeo huo,” alisema mmoja wa wajumbe wa tume ile.
Pia uchambuzi wa kamati ile uligundua kuwa hakukuwapo mawasiliano kati ya Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na Baraza la Mitihani la Taifa (Necta).TET, ambao ndio wasimamizi wa mitalaa ya elimu walitakiwa kuhakiki mitihani ile baada ya kutungwa na Necta, lakini hilo halikufanyika.
Chanzo kingine kililiambia gazeti hili kuwa tume hiyo ilibaini katika uchunguzi wake kuwa Necta ilitumia wataalamu wasio na juzi wa kutosha kutunga na kuhakiki mitihani.Uchunguzi huo ulibaini baadhi ya mitihani kama ya masomo ya Hisabati, Kemia na Fizikia ilikuwa na maswali yaliyohitaji muda mwingi wa kuyajibu kuliko uliopangwa.
“Hii ilifanya wanafunzi kushindwa kukamilisha kujibu maswali yote yaliyotakiwa kujibiwa kwenye mitihani hiyo. Pia tulibaini kwamba baadhi ya maswali katika mitihani ya masomo ya Fizikia na Kemia yalikuwa nje ya mihutasari iliyotumika kuwaandaa wanafunzi,” aliongeza mjumbe mwingine. Mjumbe mmoja aliongeza pia kuwa mitihani ilikuwa na misamiati migumu na hata kuwasumbua walimu walioisahihisha.
Hali hii inaweza kuwa imechangia, kwa kiasi kikubwa, kuongeza ugumu wa mitihani hiyo na hili linaweza kuchangia wanafunzi kushindwa kuelewa vizuri maswali wanayoulizwa kwenye mitihani. Wajumbe wa tume hiyo walieleza hali hiyo imefanya imani kujengeka kuwa mitihani ya Tanzania ni migumu kuliko ya nchi nyingine.
mwananchi.co.tz

mwanafunzi achalazwa viboko zaidi ya 100

Mwanafunzi wa shule ya sekondari Idodi wilayani Iringa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa kwa madai ya kupigwa viboko zaidi ya 100 na mtu anayedaiwa kuwa ni mwalimu wa shule hiyo na kufungiwa katika bweni kwa siku 3 ili kuificha siri hiyo.
Tukio hilo linakuja wakati harakati mbalimbali za kijamii na asasi za kiraia zikipiga kelele kupinga vitendo vya ukatili wakati jeshi la Polisi likianzisha dawati la jinsia kwa ajili ya kutokomeza masuala hayo.
Ni mwanafunzi Lusinde Nyaulingo, wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Idodi, ambaye anaugulia maumivu makali katika Hospitali hii ya rufaa ya mkoa wa Iringa, word namba tano ya majeruhi, kutokana na ukatili uliosababisha majeraha sehemu mbalimbali za mwili wake, hasa maeneo ya mapaja, makalio na mgongo, baada ya kupigwa kwa tuhuma za kuchukua simu ya mwanafunzo mwenzie, jambo linalomfanya mwanafunzi huyu apoteze muda mwingi wa masomo wakati akipatiwa matibabu ili kurudisha afya yake.
Lusinde anasema baada ya kuangushiwa kipigo hicho kikali, kilichodumu kwa zaidi ya masaa tatatu, alipoteza fahamu na kisha kufungiwa katika bweni kwa siku tatu, huku wanafunzi wenzie wakipigwa marufuku kufikisha taarifa ya ugonjwa kwa wazazi wa Lusinde.
Hata hivyo jeshi la polisi kupitia kamanda wake mkoa wa Iringa ACP Athmani Mungi limesema kuwa wanafuatilia tukio hilo ili kuhakikisha haki inatendeka, kwa kumchukulia hatua za kisheria mtuhumiwa ikiwa ni pamoja na kumfikisha Mahakamani. 
http://bongoleotz.blogspot.com