Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumanne, 12 Agosti 2014

wanaobeza juhudi za Mbunge Vincent Nyerere hawaitakii mema sekta ya elimu Musoma

Mbunge wa Musoma Mjini Vincent Nyerere na walimu wa shule ya Sec Kiara
siku ya leo napenda kuchukua fursa hii kuzungumzia japo kwa uchache juhudi za Mbunge wa jimbo la Musoma Mjini Vincent Nyerere. kwa kile alichokifanya hivi karibuni kwa kugawa Computer pamoja na Projector kwa baadhi ya shule za Sekondari za hapa Musoma Mjini na kuahidi kugawa zingine hivi karibu
Sababu kubwa ya kuzungumzia suala hili ni baadhi ya wanasiasa wasioitakia mema sekta ya elimu kuendelea kudai kuwa hakukuwa na haja ya kugawa Computer kwa wanafunzi kwa wakati huu na badala yake angefanya kitu kingine na si kugawa computer.
harakati za marafiki wa elimu musoma tunapatikana hasa Kata ya kigera na katika Shule ya sekondari Kiara ambayo iko kata ya Kigera wamebahatika kugawiwa Computer 5 pamoja na Projector 1 na mbunge kuaidi kuwapatia tena Computer zingine 5

tatizo letu na wanaobeza juhudi za Mbunge huyu ni kwanini wao hawasemi ambacho mbunge angefanya kwa sasa kizuri zaidi ya kugawa hizo computer,
na Je hao wanaobeza watoto wao  wanasoma shule zetu za kata au wanasoma zile za St fulani  zenye kila kitu shuleni ikiwa ni pamoja na computer

kwa nini wanabeza maendeleo kwa watoto wa maskini , je si haki watoto wa maskini kuwa na computer mashuleni?

Je watoto wa maskini wa shule za kata wakifahamu kutumia computer ni jambo baya

sie marafiki wa elimu tunaamini kwamba hao watoto wa maskini wa shule za kata wana haki ya kumiliki computer mashuleni mwao kwani hata wakifeli kidato cha nne watakuwa na nguzo kidogo huenda wakawa masekretari kwani watakuwa walau na uzoefu wa kutumia computer
marafiki wa elimu tunapongeza juhudi za Mbunge huyu
na daima tukumbuke kuwa Elimu Ni taaluma isiyohitaji wanasiasa kuiharibu kwa siasa zao za kubeza mema yanayofanywa na mtu kisa tu si chama kile au itikadi ile

Tafakari chukua! hatua kiongozi bora ni yule anaethamini wapiga kura wake wa maendeleo ya elimu kwenye jimbo lake.

imeendikwa na Rafiki wa elimu
      Juma Richard Okumu