Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumanne, 24 Februari 2015

mbunge Nyerere agawa computer na projector kwa awamu ya pili kwa shule za sec musoma mjiji

kwa awamu ya pili sasa mbunge wa musoma mjini mh. Vincent Nyerere anakusudia kugawa computer kumi na tano  baada ya awamu ya kwanza kugawa computer kumi na tano

akizungumza na wakazi wa musoma mjini katika viwanja vya shule ya msingi mkendo mbunge huyo alielezea mafanikio mbalimbali aliyoyafikia katika sekta ya elimu. mpaka sasa ni

kujenga maabara ya kisasa katika shule ya sekondari bweri maarufu kwa jina la bweri makatani lengo likiwa ni kuwaanda wanafunzi kupenda sayansi
na kuwaahidi wananchi wa musoma mjini kuwa azma yake ya kuibadili shule ya msingi mkendo kuwa high school iko pale pale japo ni mchakato unaochukua muda mrefu kidogo.

mbunge nyerere aliefika uwanjani hapo na baadhi ya computer hizo pamoja na projector amesema kitu kikubwa anachoweza kuwalipa watoto wa
maskini wapiga kura wake ni elimu bora pekee hivyo atajitahidi kuhakikisha anakuza kiwango na ubora wa elimu musoma mjini

mbunge nyerere aliahidi kuzifikishia shule zote umeme ili iwe rahisi watoto kujifunza ambapo mpaka sasa kuna miradi kadhaa ya kupeleka umeme mashuleni imefikia  hatua za mwisho mwandishi wa blog hii alifanikiwa kuitembelea shule ya sekondari nyasho iliyokuwa mbali sana na miundombinu ya umeme na kukuta nguzo zikiwa tayari zimesimamishwa na nyaya zikigoja kuwashwa umeme tu.


mauaji ya albino

makamu meya wa manspaa ya musoma pia alizungumzia  juu ya mafanikio waliyoyafikia mpaka saa juu ya  kuzuia na kulinda watoto albino ni pamoja na kuhakikisha shule ya msingi mwisenge mpaka sasa imepata uzio kwa ajili ya kulinda watoto hao.
na pia licha ya shule ya mwisenge kupata uzio maabara ya kisasa imejengwa na inasubiri kuzinduliwa tu.

mbunge nyerere ni moja ya wabunge wanaoonyesha nia na uchungu wa kujuza kiwango cha elimu nchini.
Ongeza kich




Jumatatu, 2 Februari 2015

kamati ya shule ya nyang'omboli yajipanga kunusuru wanafunzi kukaa sakafuni

kamati mpya ya shule ya msingi nyang'omboli musoma mjini kwa kushirikiana  na wazazi wameazimia kwa pamoja kutengeneza madawati mapya kwa ajiri ya kuwasaidia wanafunzi kuindokana na adha ya kuketi sakafuni kama wanavyoonekana pichani