Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumapili, 13 Oktoba 2013

je kuna athari za kumrusha mtoto madarasa

Kuna wazazi (wakishirikiana na walimu) hurusha watoto wao madarasa (mfano anamaliza darasa la 3 anarushwa kuendelea na la 5)

- Je, unadhani ni kuna athari yoyote (kielimu, mahusiano yake na wanafunzi wenzake au kisaikolojia)?
- Unadhani kuna faida kufanya hivi?




Jana nilipeleka kijana kufanya mtihani wa kuanza kidato cha kwanza, wakati niko pale kukawa na akina mama wengine. Katika maongezi mama mmoja akasema kaleta binti yake wa darasa la sita kufanya mtihani huo, akifaulu anaruka la saba na kuanza kidato cha kwanza.

Na kuwa wakati, kuna mama mmoja tunafanya naye kazi alimrusha binti yake toka darasa la tatu na kuingia la tano, maana yake hakusoma darasa la nne kabisa.

Sasa mie nataka kujua kutoka kwa wadau.

  1. Unapomrusha mtoto darasa hakuna hasara yeyote? iwe kielimu, mahusiano yake na wanafunzi wenzie na saikolijia nzima ya mtoto(Ukizingatia mchana na usiku anakula ugali-kuna sred niliona mtu kasema ugali unasababisha mtu awe kilaza)
  2. Kuna faida yeyote kurusha mtoto darasa?
souce. jamii forums
Kuna wazazi (wakishirikiana na walimu) hurusha watoto wao madarasa (mfano anamaliza darasa la 3 anarushwa kuendelea na la 5)

- Je, unadhani ni kuna athari yoyote (kielimu, mahusiano yake na wanafunzi wenzake au kisaikolojia)?
- Unadhani kuna faida kufanya hivi?

Fuatilia mjadala huu => http://bit.ly/1gz2VIm