Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumanne, 12 Mei 2015

Geita walimu hawana meza wala viti

Geita. Walimu wa Shule ya Msingi Mwatulole mkoani Geita, hawana meza wala viti hali inayowalazimu kukalia madaftari ya wanafunzi kwa kuyatandika kwenye magogo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi baada ya kukutwa wamekalia madaftari, walimu hao walisema ukosefu wa samani shuleni hapo unawaathiri katika ufundishaji.
“Wakati mwingine tunasahihisha madaftari, huku tumesimama,” alisema Mwalimu Mathias Matiginya na kuongeza:
“Unakuta mwalimu ana vipindi vinne kwa siku, lakini anaishia kufundisha viwili kutokana na kusimama muda mrefu, anachoka haraka.”
Pia, alisema shule hiyo ina walimu wengi na haina ofisi, viti wala meza, hivyo walimu wanatumia darasa kama ofisi.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Catherine Mgisu alisema suala hilo limefikishwa kwa uongozi wa halmashauri na kamati ya shule.
Alisema kamati hiyo inafanya jitihada za kuhamasisha wazazi kusaidia maendeleo ya shule ikiwamo upatikanaji wa viti na meza za walimu.
“Hii shule ina changamoto nyingi siyo ukosefu wa vitu hivyo tu, bali ina wanafunzi wengi, uhaba wa madarasa na madawati pamoja na utoro wa wanafunzi,” alisema Mwalimu Mgisu.
Katika hatua nyingine; Mwalimu wa Taaluma, Salma Rajab alisema anakerwa na wingi wa wanafunzi.
Alisema kutokana na hali hiyo  kipindi cha mitihani mbanano huwa mkubwa hali inayowanyima fursa ya kusimamia vizuri.
“Walimu tunapata shida hasa wanafunzi wanapofanya mitihani, tunashindwa kupata uhalisia wa matokeo yao. Huwa hatulitawali darasa kutokana na msongamano, hivyo tunakaa nje,” alisema Mwalimu Rajab. Mwalimu Debora Lucas alisema darasa moja linachukua zaidi ya wanafunzi 3,000.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita, Magarita Nakainga alisema alipokea taarifa ya changamoto hizo na kwamba suala hilo linashughulikiwa ili kuhakikisha shule inakuwa na hali nzuri.


“Ni aibu kwa shule za mjini kuwa hivyo, hivi sasa tunaweka mikakati ya kukarabati na kuboresha miundombinu tunakusanya mapato ili tuanze kazi hiyo,”

chanzo mwananchi

alisema.

matukio ya picha mkutano wa mtandao wa marafiki wa elimu Musoma