Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatatu, 1 Februari 2016

Haki elimu yakusanya maoni kuhusu lugha ya kufundishia

shirika la Haki elimu linakusanya maoni ya wananchi kupitia mtandao wake wa twitter juu ya mapendekezo ya lugha ya kufundishia kama iwe KISWAHILI au KIINGEREZA unaweza kushiriki kwa kuwafuata kwenye ukurasa wao wa twitter kwa anwani ya  @hakielimu 

shiriki kwa kupiga kura yako je lugha ipi ungependa itumike kufundishia?