Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumapili, 11 Agosti 2013

WALIMU NA WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI BISUMWA NA CHANGAMOTO ZA MAJENGO BORA

CHOO CHA WALIMU SHULE YA MSINGI BISUMWA

NYUMBA YA MWALIMU SHULE YA MSINGI BISUMWA

Harakati za marafiki wa elimu leo zinatufikisha katika kijiji cha bisumwa ni kijiji kilicho jirani na manspaa ya Musoma Mjini lakini kwa sasa kijiji hiki kiko ndani ya wilaya mpya ya Butiama
marafiki wa elimu tulifanikiwa kuitembelea shule mojawapo katika kijiji hiki na kujionea hali halisi ya madarasa na vyoo picha hapo juu ni choo tegemezi ya walimu wa shule ya msingi Bisumwa.
Choo hiki kina matundu mawili peke yake hakina milango na wala hakiko katika hadhi ya kujisaidia walimu.

maswali tuliyoondoka tukijiuliza vichwani mwetu ni je walimu wanajisaidiaje katika choo hiki ilhali milango yake imeangalia madarasani, lakini kitu cha ajabu katika shule hii ni uwezo mzuri wa wanafunzi wake kujieleza kwa ufasaha pale wanapoojiwa na marafiki wa elimu.
madarasa ya shule hii pia yamechakaa kweli kweli na si salama tena kwa wanafunzi.  lakini licha ya changamoto hizo walimu na wanafunzi wa shule hii ni wanasema wao wanaangalia mbele katu hawatarudi nyuma kuwapatia wanafunzi elimu bora licha ya changamoto hizo.
DARASA MOJAWAPO SHULE YA MSINGI BISUMWA