Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Alhamisi, 28 Agosti 2014

umoja wa marafiki wa elimu musoma (sauti zetu club) tumetimiza miaka 6

Marafiki wa elimu musoma
umoja wa marafiki wa elimu musoma tunaounda kikundi cha SAUTI ZETU CLUB leo tumetimiza miaka sita tangu kuanzisha umoja wetu mwaka 2008 tunamshukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania na kuzidi kutuaminisha kwa jamii na viongozi pamoja na wadau wa elimu Musoma Mijini

Kwa pamoja tunaweza kuinua sauti za wanyonge