Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatatu, 17 Agosti 2015

RAFIKI WA ELIMU OMARI MUSA MAKANYA AINGIA KWENYE ULINGO WA SIASA

rafiki wa elimu Omari Makanya mgombea udiwani kupitia ACT
Wakati taifa likiwa kwenye matatizo na changamoto kubwa katika sekta ya elimu, na tukiwa tuko kwenye wakati wa uchaguzi mkuu na kupokea ahadi nyingi kutoka kwa watangaza nia mbalimbali lakini asilimia kubwa ya watia nia awaonyeshi moja kwa moja kutatua changamoto za elimu nchini.

leo tunakutana na mtangaza nia nafasi ya udiwani Kata ya Mugango wilaya ya Musoma vijijini rafiki wa elimu bwana Omary Mussa Makanya. huyu ni mdau wa elimu anaechukizwa na changamoto zinazokabiri elimu nchini kutokana na kushiriki katika shughuli mbalimbali za kuboresha elimu ameamua kujitosa rasmi kwenye ulingo wa siasa kwa lengo la kuwasaidia wakazi wa eneo la mugango

mdau huyu wa elimu amekuwa msitari mbele kutatua changamoto za wanafunzi na walimu hasa kuhakikisha tunaondoa dhana ya viongozi kutowajibika kwa wananchi wao.
pia amekuwa mhamasishaji wa michango mbalimbali kwa kushirikiana na wazazi kutatua changamoto za shule ,

Marafiki wa elimu Musoma tunamuombea rafiki mwenzetu bw. Omari Mussa Makanya aweze kufanikiwa kutimiza ndoto yake ya kukomboa watoto wa kitanzania kupata elimu bora