Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatatu, 14 Oktoba 2013

mshahara wa Rais milioni 32 kwa mwezi

 

Igunga. Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe amesema sababu ya kutaja mishahara ya viongozi wakuu wa nchi ni kuzuia mianya ya watu wachache kuiibia nchi kutokana na usiri wa jambo hilo.
Zitto alitoa kauli hiyo jana mjini Igunga, wakati akitangaza mshahara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa mujibu wa Zitto, kwa mwaka kiongozi huyo wa nchi analipwa Sh384 milioni ambazo ni wastani wa Sh32 milioni kwa mwezi bila kukatwa kodi.
Hatua ya Zitto ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya kudumu ya Hesabu za Mashirika ya Umma (PAC), kutaja mshahara wa rais inakuja wiki moja baada ya kutaja mshahara wa Waziri mkuu kuwa ni Sh26 milioni kwa mwezi pasipo kukatwa kodi
Zitto alisema hoja ya msingi si kiasi wanancholipwa viongozi hao walioajiriwa na wananchi bali ni usiri unaofanywa juu ya kiwango hicho. Alisemaha ni jambo la kusikitisha kuona mwalimu anayelipwa mshahara wa Sh200,000 kwa mwezi ukikatwa kodi huku viongozi wa kuchaguliwa wakiwa wanapokea mishahara mikubwa pasipo kukatwa kodi.
Alisema katiba ya sasa Ibara ya 43(1), inaeleza kuwa rais atalipwa mshahara na malipo mengine huku ibara hiyo hiyo kifungu cha pili ikizuia mshahara na marupu rupu kupunguzwa, hali aliyoelezea kuwa ni muhimu katiba mpya ikabadilisha sheria hizo kwa manufaa ya nchi.
“Kwa hiyo hata kesho kama Dk Slaa akiwa Rais na akataka kupunguza mshahara wake kwa katiba hii hawezi na hili jambo si sahihi kwani viongozi wa ngazi hizi wanapata kila kitu bure kutoka Serikalini,” alisema Zitto.
Zitto alisema kuwa kitendo cha Serikali kuyafungia magazeti ya Mwananchi na Mtanzania, hakikuzingatiwa kulingana na uwazi uliowekwa kwa kuandika uwazi wa viwango vya mishahara.
Alisema kuwa waziri aliyehusika kufunguia magazeti hayo hakufikiria kwa makini kutokana na kuwa na uelewa mdogo na kuongeza kuwa hakuna kosa lolote linalopelekea kufungiwa magazeti hayo kutokana na ukweli ulioandikwa.

chanzo. mwananchi.com

Serikali yashauriwa kuruhusu walimu wa jumuiya ya Afrika Mashariki ili kukabiliana na upungufu wa walimu

Serikali  imeshauriwa kufungua milango kwa walimu wanaotoka katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kufanya kazi nchini kwa masharti nafuu.

Hali hiyo imeelezwa kuwa itachagiza kasi ya kukabiliana na upungufu wa walimu uliopo nchini na  hivyo kuboresha sekta ya elimu.

Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari ya Brilliant ya jijini Dar es Salaam, Jasson Rweikiza, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa mahafali ya tatu ya shule hiyo.

Rweikiza ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba Vijijini (CCM), alisema pamoja na jitihada za uboreshaji wa elimu nchini, bado uhaba wa walimu umekuwa tatizo sugu linalokwamisha azma hiyo.

 “Tunaweza kuboresha mazingira yote katika sekta ya elimu, lakini kama hatutakuwa na walimu wa kutosha, ni dhahiri kwamba ufundishaji utakwama na azma ya kupata matokeo bora ya wanafunzi haitafikiwa,” alisema.  Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Mbunge wa Sengerema (CCM), William Ngeleja.

Rweikiza alisema mazingira yaliyopo sasa yanakabiliwa na vikwazo katika kupata vibali kwa walimu hasa wanaotoka nchi za EAC kufanya kazi nchini.  Kwa mujibu wa Rweikiza, gharama za kibali kwa mwalimu mmoja kutoka nje, zinakadiriwa kufikia Shilingi milioni mbili.

Akizungumza katika halfa hiyo, Ngereja, pamoja na mambo mengine alisema wakati umefika kwa serikali kutilia mkazo namna bora za kukabiliana na changamoto zilizopo katika sekta ya elimu.

Alisema changamoto hizo ikiwamo wa ukosefu wa walimu, zinakwamisha ama kurudisha nyuma jitihada za maendeleo ya nchi na raia wake.

Alitoa mfano kuwa hata ufanisi katika kufikia Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) utapatikana ikiwa sekta ya elimu itaboreshwa na kuwezesha kupatikana kwa wataalam.

ippmedia.com