Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumamosi, 14 Septemba 2013

JE MBUNGE WAKO ANAITHAMINI ELIMU

Agosti 11, 2013 tulifungua shule mpya ya msingi katika eneo la Kwebamba jimboni Bumbuli ambayo tumekamilisha ujenzi wake kwa juhudi za pamoja na wananchi. Kabla ya ufunguzi wa shule hii watoto walikuwa hawaendi kabisa shule katika eneo hili. Changamoto ni kuufanya mradi huu kuwa bora zaidi hasa kuwa na uwiano sahihi wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 40 kwa darasa.

Agosti 11, 2013 tulifungua shule mpya ya msingi katika eneo la Kwebamba jimboni Bumbuli ambayo tumekamilisha ujenzi wake kwa juhudi za pamoja na wananchi. Kabla ya ufunguzi wa shule hii watoto walikuwa hawaendi kabisa shule katika eneo hili. Changamoto ni kuufanya mradi huu kuwa bora zaidi hasa kuwa na uwiano sahihi wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 40 kwa darasa.
Ongeza kichwa