harakati za marafiki wa elimu musoma wasiliana nasi kwa namba +255755 650 075 au +255786 650 075 ni jukumu letu kuboresha elimu
HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania
Jumatano, 9 Oktoba 2013
wanafunzi kidato cha pili wafanya mtihani
Alisema kati ya idadi hiyo, wasichana ni 270,734 sawa na asilimia 50.9 na wavulana ni 260,723 sawa na asilimia 49.1.Mchome alisema katika taarifa yake kwamba idadi ya shule na vituo vilivyosajiliwa kufanyia mtihani huo mwaka huu ni 4,437 ikiwa ni ongezeko la vituo 140 sawa na asilimia 3.3 ikilinganishwa na vituo 4,297 vilivyosajiliwa mwaka 2012.
Alisema watahiniwa waliojiandikisha wanajumuisha makundi maalum yenye uoni hafifu, ambao ni 89 na wasioona 93.

Mchome alisema umuhimu wa mtihani huo ni kupima kiwango cha maarifa na ujuzi alioupata mwanafunzi kutokana na mada alizojifunza katika kidato cha kwanza na cha pili.
Pia alisema mtihani huo unatoa changamoto zinazosaidia wanafunzi, walimu, wizara na wadau wa elimu kutambua mapungufu yaliyopo katika ufundishaji ili yaweze kufanyiwa marekebisho kwa lengo la kuboresha elimu.
chanzo. mwananchi.co.tz
Wanafunzi 2,446 hawapati chakula cha WFP

IMEELEZWA kuwa wanafunzi 2,446 waliopo katika shule za msingi za
wilayani Bahi, mkoani Dodoma, hawapati chakula kinachotolewa kwa msaada
na Shirika la Chakula Duniani (WFP) kutokana na shule hizo kukosa
majengo ya kuhifadhi chakula.
Hayo yalibainishwa jana na Ofisa Elimu wa Shule za Msingi Bahi, Mary Mathew.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Mary alisema
ukosefu wa majengo unatokana na wazazi kutokuwa tayari kujitolea
kujenga.
Alisema msimamo wa WFP uko wazi kwamba hawako tayari kutoa chakula kwenye shule zisizo na majengo ya kuhifadhiwa chakula.
Alieleza kuwa katika Wilaya ya Bahi, kuna shule za msingi 72 na kati ya
hizo shule saba hazipati chakula cha mchana kutokana na wazazi
kutoitikia mwito wa kujitolea.
Ofisa Elimu huyo alisema hali ya kukosekana kwa huduma ya chakula kwenye shule hizo imesababisha utoro kwa wanafunzi.
Shule ambazo hazipati chakula cha mchana ni pamoja na Nholi, Bakolo, Chikopelo Nhinyila, Tinai, Mgondo na Bahi Misheni.
Chanzo. Marafiki wa elimu dodoma

IMEELEZWA kuwa wanafunzi 2,446 waliopo katika shule za msingi za wilayani Bahi, mkoani Dodoma, hawapati chakula kinachotolewa kwa msaada na Shirika la Chakula Duniani (WFP) kutokana na shule hizo kukosa majengo ya kuhifadhi chakula.
Hayo yalibainishwa jana na Ofisa Elimu wa Shule za Msingi Bahi, Mary Mathew.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Mary alisema ukosefu wa majengo unatokana na wazazi kutokuwa tayari kujitolea kujenga.
Alisema msimamo wa WFP uko wazi kwamba hawako tayari kutoa chakula kwenye shule zisizo na majengo ya kuhifadhiwa chakula.
Alieleza kuwa katika Wilaya ya Bahi, kuna shule za msingi 72 na kati ya hizo shule saba hazipati chakula cha mchana kutokana na wazazi kutoitikia mwito wa kujitolea.
Ofisa Elimu huyo alisema hali ya kukosekana kwa huduma ya chakula kwenye shule hizo imesababisha utoro kwa wanafunzi.
Shule ambazo hazipati chakula cha mchana ni pamoja na Nholi, Bakolo, Chikopelo Nhinyila, Tinai, Mgondo na Bahi Misheni.
Chanzo. Marafiki wa elimu dodoma
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)