Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Ijumaa, 15 Machi 2013

Ukeketaji mkoa wa Mara

                            




                   UMEWAHI KUSIKIA JUU YA UKEKETAJI

                          MKOA WA MARA NDIYO HUU

Mtoto akifanyiwa unyama wa ukeketaji

ukeketaji ni moja ya mila na tamaduni za baadhi ya wakazi wa mkoa wa Mara hasa maeneo ya Tarime ,Serengeti  na baadhi ya maeneo ya jirani na wilaya tajwa hapo juu.

makabila ambayo yamejikita zaidi katika suala la ukeketaji ni wakurya ambao wameienzi hii mila tangu miaka mingi.

mara nyingi wamebaki wakiamini na kuaminisha kwamba kumkeketa mwanamke ndo kukamilika kwa mwanamke na kufikia wakati mwingine kukataza hata vijana wao kuoa mwanamke ambae aja keketa 

Juma mohammed ni mkazi wa mkoa wa mara na msanii wa filamu anazungumzia suala hili kama ni uelewa mdogo wa baadhi ya wazee wa mila pia anabainisha kuwa wakurya uamini kwamba mwanamke ambae ajakeketwa ana mikosi na astahili kuonekana kama mwanamke mbele za watu.

upande mwingine Amosi Taratasi mkazi wa butiama kazungumza na mwandishi wa blog hii na kusema kwamba suala la ukeketaji limejikita kwenye makabila yao ya wakurya tangu enzi na analizungumzia kwa mapana na kusema kwamba thamani ya mwanamke iko pale pale akeketwe au asikeketwe

pia anasema si suala la ukeketaji tu bali kuna mambo na vitendo vingi vinavyoashiria kumnyima mwanamke uhuru wake wa kuwa mwanamke kamili 

wadau wa blog hii wengine wamejikita zaidi kwa kusema kwamba kuna upungufu mkubwa wa elimu juu ya ukeketaji na kuonelea kwamba wakeketaji(mangariba) wapewe elimu ya kutosha juu ya matatizo yanayowapata wanawake waliyokeketwa na si kuishia kusema ni kosa kukeketa bila kumpa mtu elimu ya kutosha.

marafiki wa elimu tunaamini kwamba kumkeketa mwanamke ni mila zilizopitwa na wakati na azistahili katika jamii tuliyonayo tutaendelea kutoa elimu hii katika blog hii pamoja na mikutano ya marafiki wa elimu mkoa wa Mara