Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumanne, 10 Septemba 2013

MTIHANI DARASA LA SABA


SERIKALI mkoani Singida imesema haitasita kuwachukulia hatua wazazi watakaobainika kuwashawishi watoto wao kufanya vibaya katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu.

Inadaiwa kuwa baadhi ya wazazi hususani wale wa makabila ya wafugaji wamekuwa wakiwaambia watoto hao kuchora picha za ng’ombe kwenye mtihani badala ya kuandika majibu ili wasifaulu na kuchaguliwa kuingia Sekondari kwa ajili ya kuchunga mifugo na wasichana kuolewa.

Katika kipindi ambacho wanafunzi wa madarasa mengine wako majumbani kwa ajili ya likizo fupi, maandalizi yote muhimu kwa wale wanaofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi yamekwisha kamilika.

Hata hivyo licha ya kuwaandaa vyema wanafunzi wao, baadhi ya walimu wanaonekana kuwa na hofu ya kufaulisha kutokana na kuwepo tuhuma za wazazi kutotaka watoto wao waingie Sekondari.

Katika moja ya mikutano ya hadhara kuhimiza shughuli za maendeleo, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama anakiri kuwa tatizo hilo limekuwa sugu na kuathiri kiwango cha elimu mkoani Singida.

Pamoja na kukemea Mkuu huyo wa wilaya ya anatoa msimamo wa Serikali juu ya wazazi wa aina hiyo.
Singida ni moja ya mikoa ambayo imefanya vibaya katika matokeo ya darasa la saba kwa miaka mitatu mfululizo baada ya kufaulisha chini ya asilimia 50, pamoja na mambo mengine moja ya sababu ikitajwa kuwa baadhi ya wazazi kutopenda wala kujua umuhimu wa elimu kwa watoto wao.