Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Alhamisi, 12 Desemba 2013

Wananchi wadai uwajibikaji mkubwa wa wabunge Wananchi wengi Tanzania Bara waunga mkono madai hayo na vifungu vingine muhimu katika rasimu ya katiba






Tarehe 4 Desemba 2013, Dar es Salaam: Zaidi ya theluthi moja (36%) ya Watanzania Bara wameshiriki
katika marekebisho ya katiba kupitia mikutano ya jamii, SMS, mahojiano, barua na barua pepe. Idadi
kubwa walishiriki kupitia mikutano ya jamii iliyoandaliwa na Tume ya Kurekebisha Katiba (CRC). Pia,
karibu nusu ya Watanzania Bara wanaweza kuelezea Katiba ni nini.
Matokeo haya yalitolewa na Twaweza katika utafiti uitwao: Kurasimu Sheria Mama ya Nchi: Tafakari ya
Wananchi wa Tanzania Bara kuhusu Rasimu ya Katiba. Msingi wa utafiti huu mfupi ni taarifa kutoka
Sauti za Wananchi, utafiti wenye uwakilishi kitaifa, uliotumia simu ya mkononi, ngazi ya kaya katika
Tanzania Bara.
Taarifa zinaonyesha viwango vya juu vya ufahamu wa Katiba na ushiriki katika mchakato wa mapitio. Pia,
karibu watu saba kati ya kumi (67%) ya Watanzania Bara wanafahamu kuwa rasimu ya Katiba
ilizinduliwa, ingawa chini ya robo (23%) walijua jinsi ya kupata nakala ya Rasimu ya Katiba.
Moja ya maeneo makuu ya mjadala ni hali Muungano kati ya Bara na Zanzibar. Juu ya mada hii, utafiti
umegundua kuwa maoni yamegawanyika, nusu (51%) wakikubali na nusu (48%) wakikataa kuanzishwa
kwa Serikali tatu. Hata hivyo, walipoulizwa zaidi, idadi ya waliounga mkono Serikali tatu kwa Watanzania
wa Bara, ililingana na waliounga mkono Serikali moja, wote ni 19%. Sauti za Wananchi pia iliweza
kulinganisha matokeo haya na ya utafiti uliofanywa na Afrobarometer katika nchi nzima (pamoja na
Zanzibar) mwaka 2012. Mwaka 2012 karibu nusu (47%) ya Watanzania Bara walikataa mabadiliko yo
yote katika masuala ya Muungano, hata hivyo katika mwezi wa Julai mwaka 2013, robo (26%) ya
Watanzania Bara walikataa mabadiliko. Kinyume chake, moja kati ya kumi (8%) waliunga mkono
kuongezeka kwa uhuru wa Zanzibar mwaka 2012 wakati theluthi mmoja ya watu waliunga mkono jambo
hili mwaka 2013. Utafiti wa Sauti za Wananchi unafanyika Tanzania Bara tu, kwa hiyo uchambuzi huu
hauhusishi tawimu toka Zanzibar.
Kumekuwa na vifungu kadhaa katika rasimu ya katiba ambavyo vimekuwa vikijadiliwa kwa mapana
katika vyombo vya habari. Wananchi kwa kiasi kikubwa walikubaliana na rasimu katika yote haya. Karibu
wote (91%) ya Watanzania Bara wanataka kuwa na uwezo wa kumwondoa Mbunge wao kwa kushindwa
utendaji, hiki ni kielelezo cha wazi cha kutaka uwajibikaji; na ni hali iliyofanya kifungu hiki kupendwa
zaidi katika rasimu. Maeneo mengine ndani ya rasimu yaliyopata uungwaji mkono mkubwa toka kwa
wananchi ni:
Mgombea urais lazima awe na umri zaidi ya miaka 40 (84% wanakubaliana)
Mawaziri na Manaibu wao wachaguliwe na Rais na kupitishwa na Bunge (77% wanakubaliana)
Bunge lazima liundwe na wajumbe 75, wawili kutoka kila mkoa wa Tanzania Bara, wawili kila
mkoa wa Zanzibari (76% wanakubaliana)
Spika na Naibu Spika, wanapaswa wasiwe viongozi wa vyama vya siasa kwa miaka mitano kabla
ya kugombea nafasi hii (72% wanakubaliana)
Mawaziri na Manaibu wao wanapaswa wasiwe madiwani, wabunge au wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi (70% wanakubaliana)
Wabunge wanapaswa kuwa katika ofisi kwa miaka isiyozidi 15 (70% wanakubaliana)
Wagombea huru waweze kuwania nafasi ya Urais na Ubunge (67% wanakubaliana)
Kuwe na tume Huru ya Uchaguzi, iliyoteuliwa na Rais (65% wanakubaliana)
Sauti za Wananchi pia iliwauliza Watanzania Bara kama waliunga mkono rasimu ya katiba. Pamoja na
kuwepo makubaliano ya jumla katika masuala muhimu, wengi wao wangepigia kura rasimu ya sasa.
Pamoja na hayo, theluthi mbili (65%) wanaamini kwamba Uchaguzi Mkuu ujao utafanywa kwa kutumia
Katiba mpya.
Rakesh Rajani, Mkuu wa Twaweza, alisema “Kimsingi, katiba inapaswa kuandikwa kutokana na maoni
na amali za wananchi. Utafiti wa Sauti za Wananchi ni moja ya nyenzo muhimu inayotumika kupata
maoni ya wananchi kwa njia madhubuti na ya kisayansi. Ni matumaini yetu wale waliopewa jukumu la
kuandaa rasimu ya katiba watayasikiliza kwa makini.”
---- Mwisho ----
Kwa maelezo zaidi:
Risha Chande
Meneja Mawasiliano, Twaweza
e: rchande@twaweza.org | t: (255) (0) 656 657 559
Maelezo kwa Wahariri
Taarifa hii na data zilizomo zinaweza kupatikana www.twaweza.org, au www.twaweza.org/sauti
Twaweza ni jitihada ya miaka kumi zinazowalenga wananchi juu ya mabadiliko mapana katika
Afrika Mashariki. Twaweza anaamini kwamba mabadiliko ya kudumu yanahitaji kuanzia ngazi za
chini kwenda juu, na inataka kujenga mazingira na kupanua fursa za njia ambazo mamilioni ya
watu wanaweza kupata taarifa na kufanya mabadiliko kutokea katika jamii zao moja kwa moja
na kwa kuiwajibisha Serikali.
Unaweza kufuatilia kazi za Twaweza kupitia:
Mtandao: www.twaweza.org Facebook: Twaweza Tanzania Twitter: @Twaweza_NiSisi