Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatatu, 25 Agosti 2014

Hatimae shule ya kigera mbunge nyerere asema itajengwa kabla ya disemba mwaka huu

majengo ya shule ya kigera yaliyobomolewa na diwani bila kufuata utaratibu
hatimae Mbunge wa musoma mjini Mheshimiwa Vincent Nyerere katoa ahadi jana kwenye mkutano wa kuelezea mafanikio aliyofikia kwa miaka minne kuwa,
shule ya msingi Kigera iliyobomolewa na diwani wa kata hiyo ndugu Gabriel Ocharo Aenda kwa kile kilichogundulika kuwa ni kutokufuata utaratibu na kupelekea wanafunzi kukosa pahala pa kusomea ,

mbunge wa musoma mjini jana kamsimamisha Meya wa manispaa ndugu Alex Kisurura kujibu sakata la shule hiyo na kueleza kwamba ifikapo mwezi disemba shule hiyo iliyobomolewa vyumba sita vya madarasa na kupelekea wanafunzi kurundikana madarasani vitakuwa vimekarabatiwa tena kwa kiwango cha juu na kuahidi kuwa licha ya ukarabati pia watapeleka madawati mapya katika madarasa hayo.

sakata la kubomolewa madarasa hayo sita  mpaka sasa bado linaendelea mahakamani baada ya diwani huyo kufunguliwa kesi kwa kosa hilo la kobomoa madarasa hayo.

akizidi kuelezea waliyoyafanya kwa miaka minne ya uongozi wake mhe Nyerere kasema wamegawa computer 5 na projector kwa shule 3 wametengeneza madawati 1902  pamoja na mipango mingine mingi sana ikiwa ni pamoja na kujenga maabara ya kisasa shule ya sekondary bweri makatani na kujenga madarasa karibu kila shule ya sekondary