Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatano, 24 Aprili 2013

SERIKALI INAWEKEZA KWA ELIMU YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM ?

Rafiki wa elimu Juma Richard akiwa na wanafunzi wa shule ya msingi Mwisenge

Tanzania ni moja ya nchi zenye watoto wenye mazingira magumu wenye ulemavu nk.
mara nyingi watoto wenye mahitaji maalum hawapewi kipaumbele cha kwanza mfano mzuri ni shule ya msingi Mwisenge.
 Shule hii ni shule yenye watoto wenye mahitaji maalum hivi karibuni wana blog hii walipokuwa wanahojiana na watoto hawa wanakiri wazi kuwa vifaa vya kujifunzia ni changamoto kubwa sana kwao.
shule hii ina watoto wenye mahitaji maalum kama wenye albinism na mara nyingi watoto wa jinsi hii wanahitaji mazingira ya kuwafanya waone kwa ukaribu hasa pale mwalimu anapoandika ubaoni

Lakini pia shule hii ina watoto wenye ulemavu wa macho nk.
wanafunzi wote hawa wanabainisha upungufu wa vifaa vya kujifunzia pia wanaomba mwenye mapenzi na shule hii achangie upatikanaji wa vifaa.

marafiki wa elimu musoma tunatoa wito kwa wote wenye mapenzi ya dhati na shule hii ya Mwisenge aliposoma Mwalimu Nyerere  wachangie  kwa hali na mali kuhakikisha wanafunzi hawa wanapata mahitaji haya

kila mtoto ana haki ya kupata elimu awe na mahitaji maalum au asiwe na mahitaji maalum na jamii pia tunayo nafasi ya kuwasaidia watoto wetu kuhakikisha wanapata elimu bora.
Marafiki wa elimu Tunawasihii sana wana Musoma na Tanzania nzima kusaidia shule ya Mwisenge .

Shirika la HAKI ELIMU limejitolea na kujenga maktaba ya kisasa  kabisa shuleni hapo sasa ni jukumu letu na sisi wana Musoma kuiboresha shule yetu ya Mwisenge.


NYUMBA YA MWALIMU SHULE YA MSINGI MWISENGE HAPA NDIPO ALIPOSOMA MWALIMU NYERERE


Picha inayoonekana hapo juu ni moja ya nyumba za walimu wa shule ya msingi mwisenge, hapa ndipo aliposoma Mwalimu Nyerere na hii ndiyo hali halisi ya nyumba za walimu zilivyo kwa sasa.

Lazima tutafakari na kujiuliza kwa pamoja kama tutaendelea kuisubiri serikali izikarabati au tutachukua jukumu sie wenyewe.
kwa namna moja au nyingine serikali imejitahidi sana kwa upande wa madarasa kwani kidogo madarasa ya shule hii ni ya kisasa na yanaridhisha .
lakini tunapozitazama nyumba za walimu wa shule hii inatia huruma sana kwanza ni nyumba za tope pili ni nyumba za muda mrefu sana na zimechakaa.

Hapa hakuna sababu tena ya  kuisubiri serikali ni lazima kamati ya shule ibuni mbinu mbadala ya kuisaidia shule yao.
lakini pia kuna viongozi wengi sana nchi hii  wamesoma shule ya msingi mwisenge na wana nyadhifa mbalimbali serikalini je wanaifikiriaje shule hii?

ni jukumu letu marafiki wa elimu wanajamii wazazi kamati za shule kuhakikisha tunafanikisha ujenzi wa nyumba za walimu wa shule ya msingi mwisenge na si mwisenge tu bali shule zote za wilaya ya musoma mjini
Marafiki wa elimu tunaanza kampeni sasa tutafahamishana muda si mrefu juu ya kampani yenyewe
kama umeguswa na taarifa hii tafadhali wasiliana na marafiki wa elimu musoma kwa e-mail jmrchrd@yahoo.com  tutakuunganisha na kamati ya shule ya msingi mwisenge tujitolee kusaidia shule hii kwani ni mfano wa taifa.