Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatano, 10 Septemba 2014

kila la heri wanafunzi wa darasa la 7 kwa mitihani yenu ya kumaliza elimu ya msingi

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Jenista Mhagama
Jumla ya watahiniwa 808,111 wanatarajia kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi leo, huku kati ya hao wavulana ni 378,470 sawa na asilimia 46.84 na wasichana ni 429,641  (asilimia 53.16).

Aidha, katika mtihani huo, watahiniwa 783,223 watafanya mtihani kwa lugha ya Kiswahili, watahiniwa 24,888 watafanya mtihami kwa lugha ya Kiingereza.

Kwa upande wa wasioona walioandikishwa kufanya mtihani ni 86 , wavulana 54 na wasichana 32, na watahiniwa wenye uoni hafifu wanaotarajiwa kufanya mtihani huo ni 714, kati yao  wavulana ni 371 na wasichana 343.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Jenista Mhagama, alisema maandalizi yote kwa ajili ya mtihani yameshakamilika ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa karatasi za mitihani, fomu maalum za OMR za kujibia mitihani pamoja na nyaraka zote muhimu zinazohusu mtihani huo.

Mhagama alisema mtihani mtihani huo ni muhimu kwa taifa, wazazi na jamii kwa ujumla na kwamba masomo yatakayotahiniwa ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na Maarifa ya Jamii  mtihani ambao utafanyika kwa siku mbili mfululizo.

Alitoa wito kwa kamati za mitihani za mikoa na wilaya kuhakikisha taratibu zote za mitihani zinazingatiwa ipasavyo na kuwataka wasimamizi, walimu, wananchi na wanafunzi  kutoshiriki katika vitendo vya udanganyifu na kwamba atakayebainika atachukuliwa hatua kali za kisheria.