Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatano, 28 Agosti 2013

watoto wadogo nchini tanzania wanafanya kazi migodini

Shirika la kutetea haki za kibinadam la Human Rights Watch, limefichua ushahidi zaidi kuhusu unyanyazaji wa watoto nchini Tanzania, baadhi yao wenye umri wa miaka minane ambao wanafanya kazi kwa zamu, katika migodi ya madini iliyoko chini ya ardhi, kwa saa ishirini na nne.
Shirika hilo limesema watoto hao wanakabiliwa na tishio la kuvuta hewa ya sumu inayotokana na uchimbaji wa madini ya dhahabu na wakati mwingine kuuawa wakati migodi hiyo, inapoporomoka nyingi zikiwa hazina leseni.
Tanzania ina sheria kali inayozuia watoto kufanya kazi katika machimbo ya madini lakini shirika hilo limesema, serikali ya rais Jakaya Kikwete ni sharti iimarishe juhudi zake za kuhakikisha sheria hizo zimetekelezwa.

shule aliyosoma obama picha kutoka kwa rafiki wa elimu (jakarta)

Shule aliyosoma Obama Jakarta picha kwa hisani ya rafiki wa elimu boniventure godfrey