Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatatu, 8 Aprili 2013

Bi Neema Mafuru mratibu wa marafiki wa elimu musoma mjini


Neema Mafuru rafiki wa elimu musoma na mratibu wa shughuri za marafiki wa elimu

MARAFIKI WA ELIMU WAKIFANYA UTAMBULISHO KWENYE MKUTANO WA WANANCHI WA KATA YA KIGERA


Juma Richard na bi. Perus masokomya walipokaribishwa na uongozi wa erikali ya mtaa wa kigera kwenda kutambulisha rasmi harakati za marafiki wa elimu

harakati za marafiki wa elimu ni harakati za mashirika, taasisi na watu wanaojali wenye nia ya kuboresha elimu na demokrasia nchini Tanzania, kubadilishana mawazo na maoni yao katika masuala ya elimu na kuchukua hatua kwa ajili ya kuleta mabadiliko. harakati zitachangia kubadili mifumo ya shule ziweze kutoa elimu bora kwa kuzingatia misingi bora ya utawala na haki za binadamu

njoo tupaze sauti zetu pamoja