Watanzania tunaiona elimu ya MEMKWA kama haina msaada kabisa kwetu lakini ifike mahali tukumbuke kwamba mwalimu Nyerere alipigana kufa na kupona kuhakikisha tunafuta ujinga nchini na mbinu kubwa aliyotumia ni kuhakikisha walikosa elimu wanapata elimu bila kujali umri wao na akafanikiwa kwa kiwango kikubwa sana.
tofauti iliyopo sasa serikali na wanajamii hawaichukulii elimu hiyo kama ukombozi wa kututoa kwenye ujinga tena na mwisho wa siku tunaendelea kuzalisha taifa la wasiojua kusoma na kuandika
kwa pamoja tupaze sauti na kusema TUKIWEKEZA KWENYE ELIMU YA MEMKWA TUTAFUTA UJINGA NCHINI
harakati za marafiki wa elimu musoma wasiliana nasi kwa namba +255755 650 075 au +255786 650 075 ni jukumu letu kuboresha elimu
HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni