harakati za marafiki wa elimu musoma wasiliana nasi kwa namba +255755 650 075 au +255786 650 075 ni jukumu letu kuboresha elimu
HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Jumanne, 29 Julai 2014
ZAIDI YA WANAFUNZI 860 WA SEKONDARI WILAYANI KILINDI WAMEACHA SHULE.
Wanafunzi zaidi ya 860 wa shule mbali mbali za sekondari wilayani Kilindi wameacha shule kwa sababu mbali mbali ikiwa ni pamoja na baadhi ya wazazi wao kuwaozesha huku wengine wakiwekwa kinyumba na baadhi ya makundi ya vijana.
Mkuu wa wilaya ya Kilindi bwana Selemani Liwowa amesema hayo katika kikao cha baraza la madiwani ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Dr . Jakaya Kikwete kuwataka viongozi wa mkoa wa Tanga kuhakikisha kuwa watuhumiwa waliosababisha tatizo hilo wanakamatwa na kufunguliwa kesi katika vyombo vya sharia.
Akielezea mikakati waliyojiwekea na hatua zitakazochukuliwa mkuu huyo wa wilaya amesema kwanza wanataka wawarejeshe watoto hao kwa wazazi kisha watawakamata wazazi na watuhumiwa waliowakatisha masomo kwa ajili ya kuwachukulia hatua kali za kisheria zoezi ambalo linaanza utekelezaji wake baada ya sikukuu ya eid kumalizika.
chanzo ITV
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni