Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Ijumaa, 15 Aprili 2016

marafiki wa elimu musoma wasaidia jamii

kutokana na uhitaji wa jamii marafiki wa elimu musoma tumeona ni nafasi nzuri kujichangisha na kuweza kusaidia wanafunzi vifaa vya shule tazama picha za matukio pale marafiki tulipojumuika na jamii kuchangia tulichokuwa nacho
rafiki wa elimu Juma okumu akielezea dhana ya marafiki wa elimu

mwenyekiti wa mtandao wa marafiki wa elimu musoma Bi perus Masokomya akikabidhi vifaa hivyo







picha ya pamoja marafiki wazazi na wanafunzi




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni