Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatatu, 25 Januari 2016

shule ya msingi Mwisenge B yafanikiwa kupata darasa la tehama

darasa la tehama shule ya msingi Mwisenge B
wakati serikali ikiwa imetangaza na kuanza kutekeleza mpango wake wa kutoa elimu bure nchini shule ya msingi Mwisenge B ni moja kati ya shule zilizopata bahati nyingine tena ya kuweza kuboresha kiwango chake cha elimu kwa kuendana na mfumo wa kisasa zaidi wa kutumia computer tofauti na shule nyingi za msingi manispaa ya musoma mjini.
baadhi ya wanafunzi wakiwa kwenye chuma cha tehama
awali shirika lisilo la kiserikali la Haki Elimu liliweza kuichukua shule ya Mwisenge A na B na kuiingiza katika mipango yake na kuifanya shule ya mfano na kuweza kujenga Maktaba ya kisasa kabisa shuleni hapo pamoja na kukarabati madarasa ya awali (chekechea ( kwa kutoa vifaa vya kufundishia na kujifunzia pamoja na kuwapeleka walimu wa madarasa ya awali mafunzo.
mwalimu wa tehama shule ya msingi Mwisenge B
licha ya hayo shirika hilo pia limekuwa likitoa motisha kwa baadhi ya wanafunzi wanaofanya vizuri shuleni hapo hasa katika mpango uliouanzisha shuleni hapo wa vilabu vya masomo,ambapo vilabu hivyo vya masomo vimekuwa vikisaidia sana kuhakikisha vinamaliza kabisa tatizo la wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika shuleni hapo.
baada ya jitihada kubwa za shirika la Haki Elimu hivi karibuni wadau wengine wa elimu wamejitokeza na kuweza kuisaidia shule hiyo kwa kuipatia computer 17 pamoja na projector 3 na kuifungia shule hiyo huduma ya internet ya uhakika  jambo linaloonyesha nia ya kuitoa shule hiyo ilipokuwepo na kuipaisha zaidi kitaaluma .hivi karibuni kumekuwepo na mipango mbalimbali ya kuifanya shule hiyo kuwa kituo cha tehama kwa shule za msingi musoma mjini ,jambo litakalo kuwa zuri ikizingatiwa kuwa shule ya msingi Mwisenge ndipo aliposoma baba wa taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere.pamoja na iongozi wengine wakubwa kama kina jaji Sinde Joseph Warioba.








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni