Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatano, 19 Juni 2013

Elimu kama hii kweli tutayafikia malengo ya elimu bora?

picha na habari kwa toka jamii forums

Shule ya msingi ya Kinyambwiga iliyopo kata ya Guta wilayani Bunda, inakabiliwa na uhaba wa madarasa na madawati hali inayowapa wakati mgumu walimu na wanafunzi wa shule hiyo.

Kutokana na hali hiyo wanafunzi wanalazimika kusomea chini ya miti huku wakikalia mawe na wengine wakikalia mabanzi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni