Shirika la kutetea haki za kibinadam la Human
Rights Watch, limefichua ushahidi zaidi kuhusu unyanyazaji wa watoto
nchini Tanzania, baadhi yao wenye umri wa miaka minane ambao wanafanya
kazi kwa zamu, katika migodi ya madini iliyoko chini ya ardhi, kwa saa
ishirini na nne.
Shirika hilo limesema watoto hao wanakabiliwa na
tishio la kuvuta hewa ya sumu inayotokana na uchimbaji wa madini ya
dhahabu na wakati mwingine kuuawa wakati migodi hiyo, inapoporomoka
nyingi zikiwa hazina leseni.
Tanzania ina sheria kali inayozuia watoto
kufanya kazi katika machimbo ya madini lakini shirika hilo limesema,
serikali ya rais Jakaya Kikwete ni sharti iimarishe juhudi zake za
kuhakikisha sheria hizo zimetekelezwa.
harakati za marafiki wa elimu musoma wasiliana nasi kwa namba +255755 650 075 au +255786 650 075 ni jukumu letu kuboresha elimu
HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni