Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatatu, 14 Oktoba 2013

Serikali yashauriwa kuruhusu walimu wa jumuiya ya Afrika Mashariki ili kukabiliana na upungufu wa walimu

Serikali  imeshauriwa kufungua milango kwa walimu wanaotoka katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kufanya kazi nchini kwa masharti nafuu.

Hali hiyo imeelezwa kuwa itachagiza kasi ya kukabiliana na upungufu wa walimu uliopo nchini na  hivyo kuboresha sekta ya elimu.

Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari ya Brilliant ya jijini Dar es Salaam, Jasson Rweikiza, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa mahafali ya tatu ya shule hiyo.

Rweikiza ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba Vijijini (CCM), alisema pamoja na jitihada za uboreshaji wa elimu nchini, bado uhaba wa walimu umekuwa tatizo sugu linalokwamisha azma hiyo.

 “Tunaweza kuboresha mazingira yote katika sekta ya elimu, lakini kama hatutakuwa na walimu wa kutosha, ni dhahiri kwamba ufundishaji utakwama na azma ya kupata matokeo bora ya wanafunzi haitafikiwa,” alisema.  Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Mbunge wa Sengerema (CCM), William Ngeleja.

Rweikiza alisema mazingira yaliyopo sasa yanakabiliwa na vikwazo katika kupata vibali kwa walimu hasa wanaotoka nchi za EAC kufanya kazi nchini.  Kwa mujibu wa Rweikiza, gharama za kibali kwa mwalimu mmoja kutoka nje, zinakadiriwa kufikia Shilingi milioni mbili.

Akizungumza katika halfa hiyo, Ngereja, pamoja na mambo mengine alisema wakati umefika kwa serikali kutilia mkazo namna bora za kukabiliana na changamoto zilizopo katika sekta ya elimu.

Alisema changamoto hizo ikiwamo wa ukosefu wa walimu, zinakwamisha ama kurudisha nyuma jitihada za maendeleo ya nchi na raia wake.

Alitoa mfano kuwa hata ufanisi katika kufikia Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) utapatikana ikiwa sekta ya elimu itaboreshwa na kuwezesha kupatikana kwa wataalam.

ippmedia.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni