Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatatu, 4 Novemba 2013

Big results now itafanikiwa kuongeza ufaulu lakini itaua ubora wa elimu

kwa mara ya kwanza leo Marafiki wa elimu musoma tumeweza kuzungumza na baadhi ya wanafunzi kuhusu mtihani wa taifa wa kidato cha nne, majibu tuliyoyapata kwa wanafunzi yanatia matumani sana kati ya wanafunzi 70 wa shule 5 tofauti hapa musoma tuliowahoji jinsi wanavyouona mtihani wanafunzi 65 wamesema mtihani ni rahisi wanafunzi wanafunzi 5 tu wamesema mtihani ni mgumu hii inaonyesha mwelekeo wa matokeo yajayo yanaweza kuwa mazuri zaidi ikilinganishwa na alama za ufaulu jinsi zilivyolegezwa marafiki wa elimu tunawatakia wanafunzi waendelee na mtihani na wazidishe bidii wapate division 1 maana ndio yenye unafuu kwao

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni