kwa mara ya kwanza leo Marafiki wa elimu musoma
tumeweza kuzungumza na baadhi ya wanafunzi kuhusu mtihani wa taifa wa
kidato cha nne, majibu tuliyoyapata kwa wanafunzi yanatia matumani sana
kati ya wanafunzi 70 wa shule 5 tofauti hapa musoma
tuliowahoji jinsi wanavyouona mtihani wanafunzi 65 wamesema mtihani ni
rahisi wanafunzi wanafunzi 5 tu wamesema mtihani ni mgumu hii inaonyesha
mwelekeo wa matokeo yajayo yanaweza kuwa mazuri zaidi ikilinganishwa na
alama za ufaulu jinsi zilivyolegezwa marafiki wa elimu tunawatakia
wanafunzi waendelee na mtihani na wazidishe bidii wapate division 1
maana ndio yenye unafuu kwao
harakati za marafiki wa elimu musoma wasiliana nasi kwa namba +255755 650 075 au +255786 650 075 ni jukumu letu kuboresha elimu
HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni