Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumapili, 1 Desemba 2013

Serikali kusaidia mikakati ya taasisi zinazosaidia elimu

Naibu Katibu Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Zuberi  Samatama, amesema serikali itasaidia mikakati inayoibuliwa na taasisi mbalimbali za kiserikali katika kuboresha elimu ya msingi nchini.
 
Samatama alisema hayo, wakati akizindua kampeni ya uboreshaji wa elimu ya msingi Manispaa ya Ilala jijini Dar es salaam, inayofahamika kama Mnazi mkinda.
 
Alisema kampeni hiyo ambayo lengo lake kubwa ni kuhakikisha wanafunzi wanakuzwa vipaji walivyozaliwa navyo, ni jambo la kuigwa kwani itawafanya watoto kuhudhuria masomo kwa muda wote.
 
Alisema serikali itahakikisha inaanzisha tuzo maalum kwa walimu wabunifu kwa ajili ya kuwapa moyo na kuwatambua.
 
"Kitu hiki mlichokibuni kitasaidia sana katika kuhakikisha wanafunzi wanapenda kusoma kwa sababu watatambua kile wanachokipenda kipo kwenye shule zao," alisema Samatama.
 
Alisema katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN), umesababisha ongezeko la ufaulu kwa wanafunzi wa darasa la saba kutoka kiwango cha asilimia 5.6 hadi silimia 75, mwaka jana.
 
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Mwenda Hasara Maganga, alisema kampeni ya Mnazi mkinda, itawavutia watoto kwa kupenda shule na kuacha tabia ya ukwepaji.
"Kwa ujumla tatizo la machimbo halitakuwepo kwa sababu kila mtoto atapata kile anachopenda," alisema.
 
Baadhi ya vipaji vitakavyokuzwa katika kampeni hiyo ni pamoja na Hisabati, Sayansi, Teknohama, Dini na Sanaa ya maigizo, ngoma, muziki na sarakasi.
 
Afisa Elimu ya Msingi wa Manispaa hiyo, Elizabeth Thomas, alisema kampeni ya Mnazi mkinda imesambazwa kwenye shule zote pamoja na kuandaa kituo maalumu cha ukuzaji vipaji katika shule ya msingi Mnazimmoja.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni